Skip to main content

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya.

Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee.

Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo.

Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana.

Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vyema anapotiwa hatiani, hukumu yake ni kunyongwa hadi kufa.



Nae mshiriki Sharif Hamad Iddi, alisema serikali iondoe fungu la huruma kwa wanaoingiza aina yoyote ya dawa za kulevya, kwani madhara yake ni makubwa.

Nae Nasfa Abdalla Abdi, alieleza kuwa kupitia kongamano hilo, amejifunza mambo kadhaa, ikiwemo mbinu chafu za wasafirishaji dawa za kulevya na wajibu kama jamii.





Akilifungua kongamano hilo, Afisa Mdhamini Afisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ Pemba, Thabiti Abdalla, aliwataka wanafunzi hao, kuzitumia simu zao, ili kujifunza masuala ya sheria.

‘’Kama ambavyo ujumbe wa mwaka huu unaelezea, tumia teknologia kurahisisha upatikanaji wa haki, hivyo nanyi msiwe nyuma, katika kufikia hilo,’’alieleza.

Aidha Afisa Mdhamini huyo, ameisisitiza haja kwa jamii, kujifunza pole pole masuala ya sheria, kupitia wasaidizi wa sheria waliomo majimboni mwao, ili kujua haki na wajibu wao.

‘’Suala la kujifunza mambo ya kisheria ni wajibu wa kila mmoja, kwani hakuna kinga, kwa kisingizio cha kutokujua sheria,’’alifafanua.

Akizungumza kwenye kongamano hilo, Meneja Mawasiliano na Ushirikiano wa kutoka ‘LFS’ Jane Matinde, alisema taasisi yao itaendelea kufanyakazi kwa karibu na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, ili kuisaidia jamii kupata haki.





Alieleza kuwa, wamekuwa wakiisaidia Idara hiyo, kusudi iwasaidie na kuwawezesha wasaidizi wa sheria, ambao wanafanyakazi moja kwa moja na jamii husika.

Akizungumzia wiki ya msaada wa kisheria, alisema ni siku maalum kabla ya kilele, ili taasisi za watoa msaada wa kisheria, kukutana na makundi kuyaelimisha.

Mwanasheria kutoka Afisi ya Mwanasheria mkuu Zanzibar ofisi ya Pemba Safia Saleh Sultan, alisema dhana ya utoaji wa msaada wa kisheria, imo ndani ya katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.






Kwa upande wake Afisa Ustawi wa Jamii Rashid Said Nassor, aliwataka wanafunzi hao, kuwafichua wanaoendesha vitendo vya usafirishaji haramu, wa binaadamu.

Akiwasilisha mada ya athari za dawa za kulevya, afisa kutoka Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na dawa za Kulevya Pemba, Ahmed Khamis Kombo, alisema sheria mpya nambari 8 ya mwaka 2021 imeongeza makali zaidi.

‘’Kwa mfano dawa za kulevya zikikutikana ndani ya nyumba, kisheria inataifisha, hata chombo mfano gari, piki piki, mashua inakuwa mali ya taifa,’’alieleza.

Akilifunga kongamano hilo, Afisa Dhamana wa Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ tawi la Benjamin Walliam Mkapa Pemba, Idrissa Khamis Sabour, alisema kongamano hilo, limewaamsha walio wengi, kupata uwelewa wa kisheria.




Wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar ilizinduliwa Juni 24, 2024 na Waziri wa Nchi Afisi, Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Zanzibar, Haroun Ali Suleiman.

Hii ni wiki ya tano wa Msaada wa Kisheria Zanzibar, ambapo ujumbe wa mwaka huu ni ‘tumia teknologia kurahisisha upatikanaji wa haki’’ na mgeni rasmi wa kilele hicho anatarajiwa kuwa Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi.

                                Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan