Skip to main content

MWENGE WA UHURU 2024, WATUA PEMBA UKITOKEA DAR- ES- SALAAM

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MWENGE wa uhuru wa kitaifa, umewasilileo Mei 13, 2024  katika mkoa wa kusini Pemba, kwa ajili ya kutembezwa katika wilaya za Mkoani na Chake chake, ukitokea mkoa wa Dar-es Salaam Tanzania bara.

 

Mwenge huo, umepokelewa katika uwanja wa ndege wa Pemba, na kupokelewa na wakuu wa mikoa ya kusini na kaskazini Pemba, wakuu wa wilaya nne za Pemba, maafisa wadhamini, viongozi wa Chama cha Mapinduzi, ‘CCM’ wa mikoa ya Pemba, wafanyakazi wa serikali na wananchi wengine.

 



Kabla ya Mkuu wa mkoa wa Dar-es Salaam Albert Chalamila kumkabidhi Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba, Mattar Zahor Massoud mwenge huo, alisema aliupokea ukitokea mkoa wa Pwani ukiwa salama.

 

Mkuu huyo wa mkoa alisema, mwenge huo ukiwa ndani ya mkoa wake ulitembezwa urefu wa kilomita 427.7 kwa siku tano, na ulizindua miradi 39 yenye thamani ya shilingi bilioni 479.6.

 

Alieleza kuwa, pamoja na uzinduzi huo wa miradi, mwenge huo ulisababisha wananchi 994, kujitokeza kuchunguuza afya zao, wakiwemo wanawake 456 na wanaume 538, na wananchi sita kati yao, waligundulika na virusi vya ukimwi, wakiwemo wanawake wanne na wanume wawili.

 

Aidha alieleza kuwa, wananchi wa mkoa wa Dar-es Salaam, kutoka wilaya zote, wapatao 272 walijitokeza kuchunguuza afya zao, kuangalia homa ya malaria, wakiwa wanaume wakiwa 88 na wanawake 184, waliogundulika walikuwa watatu, wote wakiwa ni wanaume.

 


‘’Mwenge wa uhuru kwa mwaka huu, umesaidia sana wananchi wa mkoa wangu wa Dar-es Salaam, maana wamepata ushauri, kuchunguuza magonjwa bila ya malipo na kisha kupewa ushauri nasihi,’’alieleza.

 

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Mkoa wa Dar- es Salaam, alisema wakimbizwa mwenge wa uhuru kitaifa, wamefanyakazi kubwa wakiwa mkoani humo, kwa kutoa ujumbe wa mwenge kwa upana.

 

Mapema kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa Godfrey Eliakimu Mnzava, alisema wamejifunza mambo kadhaa, walipokuwa mkoa wa Dar-es Salaam, ikiwa ni pamoja na umoja na mshikamano kwa watendaji wote.

 




Katika hatua nyingine, aliutaka uongozi wa mkoa wa kusini Pemba, kuhakikisha wanapata taarifa za miradi mapema, kabla ya kuanza ukaguzi na uzinduzi, ili kujiridhisha.

 

Alieleza kuwa, jingine ni kuhakikisha kila mradi wanawekewa wataalamu husika, ambao wanataarifa za ndani na za uhakika, juu ya mradi husika, ili kazi ya uzinduzi iwe rahisi.

 

‘’Ile miradi ambayo imepangwa mwenge wa uhuru uyapitie, ni vyema kwa wakuu wa wilaya na watendaji wingine, kujipanga na taarifa zipatikane mapema, samba mba na kuwekwa kwa wataalamu husika,’’alisisitiza.

 

Mara baada ya mkuu wa mkoa wa kusini Pemba, Mattar Zahor Massoud kuupokea mwenge huo, na watembeza mwenge sita, alisema utatembezwa katika wilaya za Mkoani na Chake chake, kabla ya kuukabidhi mkoa wa kaskazini Pemba.

 


Alisema, miradi kwa upande wa wilaya ya Mkoani, ipo tisa ikiwa ni pamoja na kilimo cha umwagiliaji maji bonde la Mlemele, mradi wa mazingira Pujini, barabara eneo la Mauwani Kiwani.

 

Mradi mwingine ni ushirika wa wajasiriamali shehia ya Kukuu, kisima cha maji shehia ya Stahabu, ujenzi wa dakhalia skuli ya Michenzani, ujenzi wa nyumba za daktari hospitali ya Abdalla Mzee, pamoja na ugawaji wa vyandarua kwa watoto waliochini ya umri wa miaka mitano na utoaji matone ya vitamin ‘A’.

 

Mkuu wa wilaya ya Mkoani Khatib Juma Mjaja, alisema atahakikisha mwenge huo pamoja na watembeza mwenge wake, watakuwa na amani wakati wote wakiwa wilayani humo.

 


Mwenge wa uhuru wa kitaifa kwa mwaka 2024, ulizinduliwa na waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa Majaliwa Aprili 2, 2024 uwanja wa chuo kikuu cha Ushirikia Moshi Tanzania bara.

                                                       Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...