Skip to main content

WAKULIMA WA MBOGA WAONESHWA NJIA KUKUZA KIPATO CHAO

 

ASHA ABDALLA, PEMBA @@@@



WAKULIMA wa Mbogamboga na Matunda  wameshauriwa kusindika Matunda na kuusarifu Mchicha lishe ili kuimarisha Afya na  kujiongezea kipato katika soko na kuweza kuimarisha uchumi wa nchi .




Ushauri huo ulitolewa na Warld vegetable centre kwa kushirikiana na ZEA chini ya mradi wa AID-I unaofadhiliwa na USAID, wakati walipokua wakipewa  Mafunzo ya nadharia na vitendo ,huko Pujini  katika kiwanda cha usindikaji  wilaya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba. 




Mradi huo  ulisema unalengo la kuhakikisha wanatoa Elimu   kwa  wakulima  wadogowadogo kupitia katika mashambani mwao na darasani ili waweze kujua namana  gani wanaweza kuusarifu mchicha lishe na kusindika matunda ili kuboresha na kuongeza thamani ya mazao ya siweze  kupotea.




Munira Rashid khamis ambae nimsimamizi wa masuala ya lishe na afya kutoka katika Mradi wa Warld vegetable centre aliesema kuwa ipo haja kubwa kwa wakulima wa mbogamboga na matunda  kupata uwelewa zaidi juu ya upotevu wa mazao na mbogamboga baada ya mavuno kua ni ukosefu wa Masoko ,miundombinu ya vitendea kazi, Majokofu  ya asili ya kuhifadhia na vyungu vya udongo. 




"Wakulima tunapovuna mboga zetu na matunda tujitahidi kuzifanyia maboresho ya kuzihifadhi katika sehemu salama ili yaweze kukaa kwa muda mrefu bila ya kuharibika na kupoteza thamani  ya zao hilo" alifafanua. 



Aidha alifafanua kuwa mbegu za  mchicha lishe nimuhumi  sana  kuzisarifu kwa kuzichanganya na nafaka nyengine, zikiwemo mtama ,choroko,mbegu za mboga, kwa ajili ya kutengeneza unga wenye virutubisho sahihi vyenye 
 kujenga mwili  na kuwapa watoto kuanzia6, wajawazito, na watuwazima pamoja na wagonjwa .



 Hatahivyo aliwaomba wakulima hao kupitia Mafunzo hayo ya kusindika unga wa mchicha lishe na kusarifu mazao   waliopewa wende wakawe walimu kwa kwa kuwafundisha  wakulima wenzao ili Elimu hiyo ipate kuzidi kuendelea nakuimarika zaid Zanzibar na Tanzania kwa ujumla. 





"Mradi wetu wa Warld vegetable centre kwa kushirikiana na ZEA  tunalengo la kuwawezesha wakulima kwa kuwapa hii Teknolojia ya kisasa kwenye huu usindikaji wa Mchicha lishe pamoja na Mazao mengine zikiwemo tungule kwakutengeza Tomato past na viungo ili Wajasiriamali kuweza kukuwa kimaendeleo zaidi" alifafanua. 



Kwaupande wake Muezeshaji food technolojikalis ambae ni Meneja Kituo cha kuleya na kukuza Wajasiriamali Zanzibar Ahmed Nasour Masoud aliwapa Elimu  wakulima hao wanapovuna mazao yao wayafanyie usindikaji kwa yale ambayo yanahitaji kusindikwa ili mkulima apate kujiongezea kipato na kuongeza  bidhaa kuwa bora na kuondoa upotevu wa Mazao.



" Tunapo weza kusindika mazao  yetu ambayo yaliharibika kama tungule kuifanyia Tomato past au Nyanya paket au kusindika kwakuanika tukapata unga wa tungule tukatumia kwamatumizi mengine tuna weza kupunguza upotevu wa Mazao nakuweza kujiongezea  soko na kupata kipato  kizur." Alifafanua. 





Hata hivyo aliwashauri wakulima hao kuandaa mazingira safi na salama wakati wanapotaka kufanya usindikaji na kuweka vifungashio ambavyo vinaweza kuendana na muda uliopo mfumo wa  utamaduni na ukuwaji wa Teknolojia  ya kisasa na pia kurahisisha kulinda bidhaa isiharibike kwa haraka. 




Nae Nadra Suleiman Haji kutoka katika mradi wa Warld vegetable centre  alisema kua mradi huu  ni wa miaka miwili na madhumuni makubwa  katika Mafunzo hayo nikufikia Wajasiriamali 120 katika vikundi kumi na mbili ambavyo wataweza kuunda viwanda tofauti kwa wale ambao wamepatiwa Mafunzo na kuwafundisha wengine .





Aidha alieleza kuwa Mradi huu kwa kushirikiana na ZEA kupitia mafunzo haya yaliotolewa kuhusiana na  mchicha lishe  hayataishia hapa bali yataendelea kwa usindikaji wa tungule, usindakaji wa viungo tofauti na kuviimarisha viwanda kwa kuwapatia vitendea kazi  Wajasiriamali hao. 



Hatahivyo  aliwaomba wajasiriamali wayachukuwe Mafunzo hayo waliopewa nakwenda kuyafanyia kazi ,kwani hiyo nifursa pekee kwa akina mama ambayo itawasaidia kukuza bidhaa zao ambazo watazalisha hapa  nakuondokana  kutumia  bidhaa zinazozalishwa nchi nyengine. 



Nae Kaumu mkuu wa Idara ya Mafunzo na miradi ya uwezeshaji kutoka Wakala wa uwezeshaji Wananchi kiuchumi ZEA Ali MohamedAli amewaomaba wajasiriamali hao kuyachukuwa mafunzo  hayo kwa umakini na iwe nimuendelezo mzuri kwawe gine ambao wanatamani kua wajasiriamali na kuzalisha bizaa kama hizo za kusindika unga wa mchicha lishe ambao una virutubisho  na mazao ili kujipatia kipato kikubwa  kwenye soko .





Nae Afisa Maendeleo ya kilimo Wilaya ya Mkoani  Said Ali Hassan  alisema kuwa Mradi wa Warld vegetable centre ni msaada mkubwa katika kisiwa cha Pemba kwa kupewa hii taaluma kwa wakulima hivyo aliwaomba wakulima hao wayatumie vizuri mafunzo waliopewa  kwavitendo ili kulifikia lile lengo ambalo lilikusudiwa katika kuboresha bidhaa zenye ubora .





Nao baadhi ya washiriki wa Mafunzo hayo Rabiya Ali Hamim aliushukuru mradi wa Warld vegetable centre kwa kushirikiana na ZEA kwa kuwapa hii taaluma ambayo walikua hawana uwelewa nayo  Ä·uhusu huo Mchicha lishe na upotevu wa mazao baada ya mavuno, hivyo mafunzo hayo yanaweza kuwapa  fursa mbalimbali na kuweza  kuzitatua changamoto za kimaisha. 



Kwakupitia mradi huo wameahidi watakwenda kuyafanyia kazi nakuwapa ujuzi kwa wale wenzao ambao hawakubahatika kupata mafunzo hayo ili wajasiriamali waweze kuongezeka siku hadi siku.



Mafunzo yalioandaliwa na Warld vegetable centre kwa kushirikiana na ZEA chini ya mradi wa AID-I unaofadhiliwa na USAID  ni  ya miaka miwili kwa sasa yaliofanyika siku3 na  yamejumuisha wakulima na wajasiriamali 220 kwamafunzo yana nadharia  na wajasiriamali 30 kwa vitendo .



Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan