Skip to main content

MAADHIMISHO SIKU YA UHURU WA HABARI DUNIANI, RC KUSINI PEMBA ASEMA NENO

 



NA ZUHURA JUMA, PEMBA @@@@ 

WAANDISHI wa habari kisiwani Pemba wametakiwa kufuata maadili ya kazi zao, ili kuepuka kuingia kwenye makosa.   

Akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa maadhimisho ya siku ya uhuru wa habari, leo Mei 18, 2024 uliofanyika ukumbi wa Chuo cha Samail Gombani Chake chake Pemba, Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, alisema mwandishi wa habari aliesomea fani ya habari hawezi kuvunja miiko na maadili.  


Alisema kuwa, tasnia ya habari sasa imevamiwa na watu ambao hawakusomea fani hiyo, jambo ambalo linaweza kusababisha migogoro katika jamii na kushusha hadhi ya tasnia, hivyo ipo haja kwa waandishi wa habari kuzingatia maadili wakati wa kazi zao ili kuepuka changamoto zinazoweza kujitokeza. 


"Siku hii ya uhuru wa habari ni muhimu kujitafakari kwamba tunafanya kazi kwa kiasi gani, tuna uhuru kiasi gani, vikwazo gani tunavyopitia na kupanga mikakati ya kuweza kutatua," alisema Mkuu huyo. 


Mkuu huyo aliwataka waandishi hao kuibua changamoto za wananchi na kuzisemea, ili ziweze kupatiwa ufumbuzi, kwani sauti ya mwandishi ndio inayosaidia katika kuleta mabadiliko na maendeleo katika nchi. 


Aidha aliwataka waandishi kuelimisha jamii juu ya kuhifadhi mazingira, ili yawe safi na kuweza kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ambayo yamekuwa yakiathiri maisha ya wananchi. 


Kwa upande wake Afisa Mdhamini Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Pemba Mfamau Lali Mfamau alisema, waandishi wa habari wana wajibu wa kuwatumikia wananchi, hivyo wafike vijijini kuibua kero zinazowakabili. 


"Tufanye kazi kwa bidii na kudumisha nidhamu, pia nawaomba waandishi wenye online TV na blogi wajisajili na kutafuta kadi ya uandishi, kwani kuna baadhi ya watu wanatumia mwamvuli wa waandishi kujifanya mwandishi," alisema Mdhamini huyo. 

Mapema Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Pemba (PPC) Bakar Mussa Juma alisema, waandishi wa habari katika Klabu hiyo wanafanya kazi vizuri na kuzingatia maadili ya uandishi wa habari, hivyo wanaomba jamii na viongozi mbali mbali kuendelea kuwapa ushirikiano ili wapate habari na kuzisemea. 


Alisema kuwa, Klabu ina malengo makubwa ya kuanzisha radio na television ili waajiri waandishi wao, ambapo kwa sasa wameanza na blogi ambayo inawapatia mafanikio makubwa katika tasnia hiyo. 


Nae akiwasilisha mada katika maadhimisho hayo mwandishi wa habari na Mjumbe kutoka PPC Gaspar Charles alisema, waandishi wa habari wana jukumu la kulinda na kuelimisha jamii kuhifadhi mazingira ili kudhibiti athari za mabadiliko ya tabianchi. 


Maadhimisho hayo ya siku ya uhuru wa habari yamefanyika katika Ukumbi wa Samael Gombani Chake Chake ambayo yameandaliwa Klabu ya Waandishi wa Habari Pemba (PPC) kwa ufadhili wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC).


                        MWISHO.





Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan