Skip to main content

WANANCHI PEMBA WASEMA JAMBO FEDHA ZA UVIKO19 KWENYE AFYA

 


  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@@

WANANCHI kisiwani Pemba, wamesema fedha za ahuweni ya UVIKO 19, zilizoelekezwa kwenye miradi ya wizara ya Afya kisiwani humo, zimetumika vyema, na sasa wanaendelea kunufaika nazo.

Walisema, serikali iliweka wazi mgao wa fedha hizo na matumizi yake, ambapo kwa upande wa Wizara ya Afya na hasa kisiwani Pemba, zilizitumia kwa ujenzi wa hospitali za kisasa.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, juu ya kumalizika na kuanza kazi kwa hospitali hizo, walisema majengo hayo yamekuwa ya kiwango cha juu, ujenzi wake.

Walieleza kuwa, sasa wameshaachana na majengo ya zamani, ambayo hayakuwa na nafasi, kwa ajili yao na madaktari wanapotoa huduma kwa wagonjwa.

Maryam Himid Mjaka wa Micheweni, alisema sasa wamekuwa na nafasi kubwa ya kukaa kumsubiri daktari, ikilinganishwa na hospitali yao ya zamani.

Kazija Haji Mshamata wa Konde, alisema sasa wamekuwa na hamu ya kwenda kutafuta huduma kwenye hospitali ya Micheweni ama Kinyasini, kutokana na ubora wake.

Mwananchi Haji Vuai Shella wa Wawi, alisema sasa amekuwa akienda kila anapopata hitifalu ya afya yake, kwani pamoja na uwepo wa majengo ya kisasa, lakini hata huduma zimeimarika.



‘’Sasa dawa unweza kupata zote hata kama ni tano ulizoandikiwa, na ukifika kuna sehemu maalum ya kumsubiri daktari, kwa aina ya ugonjwa unaokusumbua hamchanganyiki kama zamani,’’alifafanua.

Kwa upande wake Thuwaiba Haji Khamis, alisema hata wodi za wazazi sasa zimeimarisha, ambapo kuna vitanda zaidi ya vitatu ambavyo vinaweza kutumika kwa wakati mmoja.

‘’Majengo yale ya zamani, kulikuwa na vitanda viwili, mkiwa wajawazito kuanzia watatu msubiriane, au wakati mwingine, ilikuwa lazima waazime chumba kisichokuwa na kitanda, kwa ajili yao,’’alieleza.

Akizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni, Afisa Mdhamini wizara ya Afya Pemba Khamis Bilali Ali, alisema wizara hiyo kwa Zanzibar nzima, ilipewa shilingi bilioni 80.1 kwa ajili ya uimarishaji wa huduma za afya.

Alisema, kupitia fedha hizo pamoja na miradi mingine, kulijengwa hospitali za kisasa za Kinyasini wilaya ya Wete, Micheweni na Vitongoji kwa wilaya ya Chake chake.

‘’Ujenzi wa hospitali hizi, ambazo kwa sasa zinaendelea kutumiwa na wananchi, ni miongoni mwa juhudi za maksudi, za Rais wa awamu ya nane Dk. Hussein Ali Mwinyi, ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora,’’alieleza.


Katika hatua nyingine, Afisa Mdhamini huyo, alisema wizara pia, imejipanga kuhakikisha inajenga hospitali za rufaa kila mkoa na kisha kujenga moja ya rufaa kwa Zanzibar.

Baadhi ya wananchi akiwemo Muhidin Juma Sharifu wa Kinyasini Mkoani, alisema kasi ya Dk. Mwinyi itawasaidia wao, kupata huduma bora katika vituo vya afya na hospitali kadhaa.

Aisha Mohamed Juma wa Tironi, alisema hata wanawake walioko maeneo hayo, sasa wamepata faraja, baada ya kukabidhiwa kituo kipya cha mama na mtoto.

Akizungumza hivi karibuni, wakati akiweka jiwe la msingi la nyumba za madaktari zilizopo Hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, alisema anakusudia kuona wananchi wanatapa matibabu bora.

Alisema, havutiwi kusikia kuna vifo vya mama na mtoto, vinavyosababishwa na huduma duni za afya, na ndio maana amekuwa akiongeza idadi ya wataalamu, ili kukabiliana na changamoto hiyo.

                Mwisho

  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch