Skip to main content

ACT-WAZALENDO CHAKE CHAKE CHAPATA VIONGOZI WAPYA

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANACHAMA wa Chama cha ACT-Wazalendo mkoa wa Chake chake kichama, wamekamilisha uchaguzi wao mkuu, baada ya kuwapata viongozi wapya, watakaokiongoza chama hicho, kwa miaka mitano ijayo.

 Katika uchaguzi mkuu huo, umemrejesha tena kwenye nafasi ya Katibu, aliyewahi kuwa Mwakilishi wa majimbo ya Vitongoji na Wawi wakati huo, Saleh Nassor Juma, baada ya nafasi yake kukosa mpinzani.

Ambapo katika uchaguzi huo, uliofanyika Gombani Chake chake Pemba, alijizolea kura 65, kati ya kura 73 zilizopigwa, huku kura mbili zikiharibika na kura sita zikimkataa.

Aidha Msimamizi wa uchaguzi huo Rashid Ali Abdalla, alimtangaaza Yussuf Salim Khamis, kuwa ndie Mwenyekiti wa Chama hicho kwa kipindi cha miaka mitano ijayo, baada ya kupata kura 39 na kumshinda mpinzake Mohamed Juma Khatib aliyepata kura 34.

Katika uchaguzi huo, ulimchagua Khadija Ali Abeid kuwa Mshifa fedha wa Mkoa wa Chake chake kwa kura 36, baada ya kumuangusha mgombea mwenzake, Khadija Anuwar Mohamed, kumpita kwa kura moja.

Viongozi wengine kwa ngazi ya mkoa, waliochaguliwa na wajumbe wa mkutano huo wa mkoa ni Katibu wa Mipango na Chaguzi, ambapo aliyeibuka mshindi ni Mohamed Ali Salim, aliyepata kura 55 na kumshinda mpinzani wake, Mbarouk Mohamed Omar aliyeangukia kura 16.




Aidha Msimamizi huyo wa uchaguzi, alimtangaaza Khamis Abied Mohamed kuwa ndie Katibu wa Habari, Uenezi wa Mawasiliano ya Umma, baada ya kupata kura 44 na kumshinda mpianzani wake, Ayoub Yussuf Mgeni aliyepata kura 28.

Kwa upande wa wajumbe wanne ngazi ya mkoa, ambao lazima wanawake na wanaume idadi sawa, waliochaguliwa ni Salma Mohamed Ali aliyepata kura 50, Salma Hamad Hassan kura 44, Hamad Khamis Mwalimu kura 48 na Maulid Issa Salim kura 43.

Nafasi ya Mwenyekiti ngome ya vijana mkoa kupitia chama cha ACT-Wazalendo, aliyechaguliwa ni Yunus Abrahman Salim, wakati Katibu wake ni Salim Haji Makame, huku ngome ya wanawake Mwenyekiti akiwa ni Jamila Ali Mohamed na Katibu ni Hazina Ali Saleh.

Wakati huo huo, Msimamizi huyo wa uchaguzi alimtaangaza Mohamed Abdalla Massoud kuwa ndie Mwenyekiti ngome ya wazee na Katibu wake ni Faki Saleh Faki, ambao hao watajumisha katika uongozi wa mkoa wa chama hicho.




Mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi huo, Mwenyekiti wa mkoa Chake chake aliyetetea kiti chake Yussuf Salim Khamis, aliwataka wanachama wote sasa kuvunja makundi na kuungana.

Alisema, sasa macho na masikio wayaelekezwe uchaguzi mkuu wa chama taifa, kisha warudi kwenye matawi, jimbo na mkoa kwa ajili ya kukijenga chama, ili kurudi kwenye ushindani kupitia uchaguzi mkuu.

Kwa upande wake Katibu wa chama Mkoa Saleh Nassor Juma, aliwaahidi wanachama wa ACT-Wazalendo mkoa wa Chake chake, kufanya juhudi kubwa kuhakikisha, wanaongeza idadi ya wanachama wapya.

‘’Kwa hili tushirikiane kwa karibu mno, maana mtaji mkuu wa chama chetu ni kuwa na wanachama wengi tunaoaminiana, kuwa kitu kimoja na kufanya uamuzi wa pamoja,’’alisema.




Kwa upande wake Mweyekiti wa ngome ya wanawake Mkoa wa Chake chake Jamila Ali Mohamed, aliwataka wanawake, kufanya kila juhudi, kuwavuta wanawake wa vyama vyingine, ndani ya chama chao.

Awali mkutano huo mkuu maalum, ulifunguliwa na Mjumbe wa Kamati kuu ya ACT-Wazalendo Isihaka Mchinjita, ambae aliwaeleza kuwa wajumbe wa mkutano huo, ndio wenyejukumu la kuwapata viongozi watakaoshirikiana na wale ngazi ya taifa, katika kukijenga chama.




Alieleza kuwa, ikiwa watafanya makosa kwa kumchagua kiongozi kwa sifa za juu juu pekee, wanaweza kukipa wakati mgumu chama, wakati kinapoingia kwenye chaguzi mbali mbali.

                Mwisho

  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch