Skip to main content

ACT-WAZALENDO CHAKE CHAKE: 'CHAGUWENI VIONGOZI WATAKAOKIVUUSHA CHAMA 2025'

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANACHAMA wa mkutano mkuu maalum wa chama cha ACT-Wazalendo, mkoa wa Chake chake kichama, wametakiwa kuwachagua viongozi wenye uwezo na nia thabiti, ya kukivuusha chama katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2025.

Ushauri huo,Januari 14, 2024 umetolewa na Mjumbe wa Kamati kuu taifa ya chama hicho, Isihaka Mchinjita, wakati akiufungua mkutano huo, uliofanyika ukumbi cha Chuo cha Samail Gombani Chake chake Pemba.

Alisema, wajumbe wa mkutano huo mkuu maalum, ndio wenyejukumu la kuwapata viongozi watakaoshirikiana na wale ngazi ya taifa, katika kuelekea uchaguzi mkuu ujao.

Alieleza kuwa, ikiwa watafanya makosa kwa kumchagua kiongozi kwa sifa za juu juu pekee, wanaweza kukipa wakati mgumu chama, wakati kinapoingia kwenye chaguzi mbali mbali.

Alifahamisha, ili chama kiwe na nguvu, mwelekeo, dira inayotekelezeka, lazima kuwepo kwa viongozi imara kuanzia tawi, jimbo, mkoa na kisha taifa.

‘’Wajumbe wa mkutano huu mkuu maalum wa ACT-Wazalendo hapa mkoa Chake chake, nyinyi mnaangaliwa na wanachama wote wa mkoa, mkifanya makosa mtajuta,’’alieleza.

Akizungumzia suala la makundi, wakati wa kuelekea uchaguzi wa chama, alisema ni jambo lisiloepukika, lakini linatakiwa kuzima mara moja, baada ya matokeo kupatikana.







Alieleza kuwa, mara mshindi anapotangaazwa, huwa ni kwa ajili ya wanachama wote, na hapo hutakiwa kuungana pamoja, ili kukipatia chama ushindi.

‘’Makundi katika uchaguzi na chama chochote huwa hayaepukiki, lakini kinachotakiwa kuepukwa ni kuendeleza makundi hata nje ya uchaguzi,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, Mjumbe huyo wa Kamati kuu ya ACT-Wazalendo taifa, Isihaka Mchinjita, aliwataka viongozi watakaochagauliwa, mara baada ya matokeo kutoka, kusahau makundi yao.

‘’Niwaombe sana, viongozi ambao leo (jana) mtachaguliwa, msijemkaendeleza makundi, bali muyavunje na sasa iwe ni kazi yenu kushirikiana na wanachama, na viongozi wa juu kukijenga chama.

Aliongeza kuwa, kila chama cha siasa huwa na majukumu mawili makuu, ikiwemo kuongoza serikali ama kuikosoa, kuiuliza na kuipongeza wakati inapofanya vizuri chama kinachoongoza.

Mapema Mwenyekiti wa cha chicho mkoa kichama Chake chake Yussuf Salim Khamis, alisema wanachama wanayohaki ya kumchagua kiongozi wamtakae, ambae ana maono ya kukijenga chama.




Aliongeza kuwa, wakati wa kupanga safu ya uongozi kupitia mikutano mikuu ndio sasa, hivyo si busara mwanachama kujilaumu, kwa kumpa kura kiongozi asiyemtaka.

Hata hivyo, alisema kazi kubwa imefanywa na viongozi waliopita, licha ya kukabiliwa na changamoto ya rasilimali fedha kwa kutokua na chanzo cha mapato.

Mapema Katibu wa ACT-Wazalendo mkoa huo, Saleh Nassor Juma, alisema kwa sasa wanaendelea na changuzi ngazi ya mkoa baada ya kuhitimishwa kwa chaguzi ngazi ya wilaya.

Mjumbe wa Kamati ya uongozi wa ACT-Wazalendo mkoa wa Chake chake Khamis Abeid Haji, alisema katika uchaguzi huo, watakaochaguliwa ni pamoja na Mwenyekiti, Katibu mkoa.




Wengine watakaochaguliwa ni Katibu wa mipango mkoa, Katibu wa habari na uenezi, mshika fedha nafasi iliyogombewa na wanachama wawili wawili, samba mba na wajumbe wanne wa kamati ya uongozi mkoa, wenye uwiyano sawa kati ya wanawake na wanaume.  

Alisema kuwa, wajumbe wingine watakaochaguliwa kwa nafasi za ukatibu na mwenyekiti ni ngome za wazee, wanawake na vijana.

‘’Nafasi nyingine ni mshika fedha wa ngome mkoa, katibu wa mipango, katibu wa habari na uenezi wa ngome pamoja na wajumbe wanne wakiwemo wanawake na wanaume wenye idadi sawa,’’alifafanua.






  Hata hivyo, amesema ushindani kwa baadhi ya nafasi umekuwa mkubwa, kwa kule wanachama wao kuhamasika kuomba nafasi mbali mbali.

Viongozi hao watakaochaguliwa kwa nafasi mbali mbali, watakiongoza chama hicho, kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

                Mwisho

  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch