Skip to main content

MJUE MWANAMKE ANAYEZIPENDEZESHA FUKWE KWA USAFI

 



NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR@@@@

Maisha ya binaadamu huwa  salama na ya afya njema kama mazingira yanayomzunguka yapo safi na salama na yanapokuwa yameharibika huwa hatarishi kwake, wanyama, wadudu na mimea.

Hali hii ndio inayopelekea kusikia kila kukicha  wizara ya afya  kwa kupitia wataalamu wake mbali mbali inasisitiz umuhimu wa kuweka mazingira safi ndani na nje ya nyumba zetu, mitaani, vijijini na katika maeneo ya biashara kama masoko au ya kuuza na kununua chakula.

Mwanamke amekuwa akionesha uongozi mzuri kwenye jamii zetu kwa kuanzia kwenye familia na kutokana na jamii yetu, katika miaka ya karibuni kutotilia maanani sana usafi wa mazingira kumepelekea kujitokeza watu kuongoza jamii kufanya marekebisho yanayohitajika.

Miongoni mwa wana jamii waliojitokeza  kuwa mstari wa mbele kuongoza juhudi za kutunza mazingira ni mwana mama anyeiingoza Kikundi cha Ulinzi wa Mazingira, Siwema  Mshenga  Issa, kutoka Sheiha ya Bubwini Makoba.

Yeye na wenzake walianzisha kikundi hicho kwa lengo la kuwaelimisha wanawake katika eneo hilo njia nzuri za kulinda mazingira na kupambana na magonjwa ya mripuko ambayo chanzo chake ni kuruhusu kuzungukwa na mazingira machafu.

Wakati huo magonjwa ya mripuko yalikuwa yameshamiri katika eneo lao na yote hii kutokana na kuzungukwa na mazingira machafu.

"Tulianzisha kikundi kwa ajili  ya kulinda familia zetu na jamii . Watoto walikua hawawezi kwenda skuli  sababu ya magonjwa ya tumbo na saa hali kidogo imebadilika, " alisema.

Kikundi kilikuwa na kamati mbili, moja iliyoshughulikia kufanya usafi maeneo ya juu na ya pili pwani.

‘’ Tulianza  na wanachama 30, lakini sasa tumebaki 26, wanawake 10 na wanaume 16. Upungufu huu umesababishwa  sababu mbali mbali ikiwemo wengine kufariki ." anasema

Kikundi kilianza na kazi ya kusafisha maji machafu na mitaro ya kwenye majaa  kwa kushirikiana na madaktari na wasimamizi wa afya.

Kazi za kwanza zilikuwa kuchimbia mashimo ili kuhakikisha wananchi hawatupi taka ovyo na katika maeneo ya pwani, waliweka doria kwa kushirikiana na wavuvi. Juhudi hizi zililenga kuzuia uharibifu wa mazingira ya bahari.

NDOTO YAKE   KUWA  KIONGOZI WA MAZINGIRA

Tangu  mdogo alipenda kuongoza wenzake wakati akisoma skuli ya msingi kwa kuhakikisha anasimamia wanafunzi wenzake katika kusafisha mazingira ya skuli. Ndoto yake ilikuwa kuwa kiongozi katika serikali.

Katika kikundi chao wanakutana na changamoto nyingi, moja wapo ikiwa kutopata mapokezi mazuri wanapokwenda majumbani kutoa elimu na mara nyingi wanaowapa usumbufu ni wanaume.

"Bado wanajamii wengi wanamchukulia mtoto wa kike kama chombo cha starehe.Hii ni changamoto kubwa  tunapo watuma mabinti zetu wa kazi watembee majumbani kutoa elimu." Alieleza.

Vile vile wapo baadhi ya watu wanaoendelea kutupa taka na kukata miti ovyo, lakini juu ya hivyo yamepatikana mafanikio, ikiwa pamoja na kusaidia kuondokana na maradhi ya mripuko.

Aliviomba vyombo vya serikali kushirikiana nao kikamilifu na kuwapa vitendea kazi vizuri ili kuzilinda afya zao wapofanya usafi.

 Sheha wa eneo hilo,  Khamis Subuhi, alionesha kufurahishwa na kazi ya kikundi hicho na zaidi kwa kumuona mwanamke anasimamia kukiongoza vizuri katika kazi zake za kila siku.



Hata hivyo, alisisitiza umuhimu wa kuendelea kuipa jamii elimu juu ya umuhimu wa kuwa na mazingira safi ili kujiepusha na maradhi na kupata mafanikio mazuri zaidi katika maisha ya kila siku.

Alisikitika kuona ufukwe wa pwani umegeuzwa eneo la  kutupa  taka na jamii kusahau kuwa huko ndiko  watoto wao wanapopendelea kwenda kucheza na  wazee huenda kufanya mazoezi.

Alisema  inafurahisha kuona maeneo yaliyo karibu na hoteli za kitalii yanawekwa katika hali ya usafi, lakini wana wakijiji bado wapo nyuma katika kuweka mazingira safi.

Mwenyekiti wa Kamati ya Uvuvi Bumbwini Makoba ,Othman Ussi Machano,ambaye ni mvuvi wa muda mrefu alifurahishwa na kuwepo kwa kikundi hicho cha ulinzi wa mazingira ya pwani.

Mwakilishi wa Viti Maalumu Mkoa wa Kaskazini Unguja, Panya Ali Abdallah, alisisitiza umuhimu wa kuweka mazingira safi ya bahari kwani mbali ya kusaidia upatkanaji wa samaki pia kutavutia watalii.

"Tukiimarisha fukwe zetu, itatusaidia kupata ongezeko la wageni katika nchi yetu na itapelekea kupata maendeleo," aliongeza.

Mmoja wa wana kijiji wa hapo, Fatma Ali Kiroboto,  alisema wanafurahi kuwepo kwa kiongozi mwanamke ambae anahamasisha usafi, kwani mwanamke ndio anaetunza mazingira ikiwa ya nyumbani hadi ya ufukweni.

Mkuu  wa Idara Huduma za Jamii Mazingira na Mipango Miji Baraza la Magharibi A, Tatu Hussein Abdallah, alisema mwanamke anapaswa kuwa kiongozi kwani ndiye mlinzi mkubwa wa mazingira.



Alisema anawajua viongozi wanaopambana kuhakikisha jamii inazingatia umuhimu wa kuwa na mazingira mazuri na Siwema ni mmoja kati yao wanaofanya kazi hio kwa uadilifu katika sheiha yake.

Aliitaka jamii kushirikiana naye kuendeleza juhudi za kikundi chake cha kuwa na mazingira mazuri katika shehia yao.

MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch