Skip to main content

WANAWAKE WAWAONESHA WENZAO NJIA KUINGIA KWENYE SIASA, CHANGAMOTO ZIGEUZENI FURSA SAFARI IENDELEE

 

 


NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR@@@@


UONGOZI ni haki ya kila mtu, awe mwanaume au mwanamke.

Tena hapa tunajifunza kuwa, hata kundi la watoto wa kike ama wakiume, wanaweza kuwa viongozi kwa aina yao na sehemu waliyo ndani ya jamii yao.

Jamii imeshazowea kuona mwanaume ndio anaeweza kuwa kiongozi na kusimamia nchi katika hali zote, kuliko wanawake na hii kutokana na mitazamo yao isijengwa kimamtiki.

Ingawa mtazamo huu, unaweza ukaondoka kwasababu mwanamke ameweza kuongoza familia na kuweza  kusimama imara,  kwahivyo hatoshindwa kuisimamia nchi nzima.

Mfano hai na wa kweli kwa sasa ndani ya taifa la Tanzania, rais anayewaongoza wananchi wastani wa milioni 60 ni Dk. Samia Suluhu Hassan (mwanamke), na kila mmoja ni shahidi hajatetereka kwenye nafasi hiyo.

Tena anasimamia vyema familia yake, pamoja na wananchi wake na kutatua changamoto mbalimbali zinazotokea katika nchi na mengi yameongelewa kuhusu yeye bali hakukata tamaa.

KWA NINI WANAWAKE HAWAONEKANA KWENYE SIASA?



Asiata Said Abdallah ambae ni mueka hazina wa Kanda ya Unguja katika Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA,  anasema amejiunga katika siasa mwaka 1994 katika chama  hicho na kugombea katika nafasi ya vijana na hakubahatika kuipata.

"Nilipojiunga katika chama, nikaona nigombanie katika upande wa vijana, mkoa wa Kilimanjaro ila sikubahatika kupata, na sikukata tamaa nikaendelea kugombania tena mwaka mwingine pia sikubahatika kupata," anasema.

Anataja moja ya vikwazo vilivyopelekea kushindwa kwanza ni elimu ya kutosha kuhusiana na siasa, kutokuwa na mahusiano na vijana wengine pamoja na kutokuwa na uwezo wa kuwashawishi vijana.

"Mume wangu wa mwanzo alikuwa hapendi nijihusishe kwenye siasa, na baada ya muda ndoa kuvunjika, nilindeleza ndoto zangu na nikabahatika mume mwengine nashukuru ananipa nguvu katika kushiriki siasa,"anaeleza.

Anaona kwenye sisa zipo fursa mbali mbali, iwapo wanawake watatuliza akili zao, ikiwemo kujenga uhusiano na wananchi pamoja na kujipima kiuongozi kwa kule kugombea na wanaume mbali mbali.

" Miaka ya nyuma ilikuwa tunaona mwanamke wa kiislamu hawezi kusimama katika jamii kutokana na imani yetu, lakini sasa hivi viongozi wa dini nao wanatuelimisha,"anafafanua. 



Sababu iliyopelekea kuingia kwenye siasa ni kurithi nyayo za mama yake  kwasababu yeye ni mwasisi wa chama cha chadema maulidah Anna komu

Aidha alisema miongoni mwa sambabu zinazopelekea wanawake kuwa kidogo katika siasa ikiwemo kutojiamini, woga, kutokuwa na moyo wa ujasiri, ambapo haya yalishajiengwa na wanaume tokea asili.

Mgeni Ali Haji ambae amegombae nafsi ya uwakilishi wa viti maalumu nafasi za wasomi katika chama cha Mapinduzi CCM mwaka 2020, na kutobahatika kupata na kuelezezea sababu mbalimbali zilizopelekea kutopata fursa hiyo.

 "Sababu iliyonifanya nikose kubwa ni kukosa matayarisho yangu binafsi, ikiwemo wapiga kura kutonielewa kwa undani pamoja na kukosa uwezo wa kufanya kampeni,’’anaeleza.

Lakini anaona wapiga kura wakati mwengine hawataki kubadili mgombea mwingina hata kama yule waliyenae hawajatekeleza ahadi zao ambazo aliwatangaazia wakati wa kampeni.

 Sambamba na hayo alisema sababu nyengine  kura hazikutosha kushinda nafasi hiyo na kubahatkika kupata kura 36 na mwezangu alipata kura zaidi ya 100.

 Aidha alisema hatua mbalimbali amechukua baada ya kushindwa, kuingia katika siasa ikiwemo kuzidi kujifunza katika masuala ya uongozi na kushiriki katika mambo ya kijamii.

"Kwavile jamii ndiyo husika katika uongozi, ndiyo wanaweza kukufahamu kwahiyo nimeona nifanye hivyo pia kuongeza elimu nalo kiupande changu ni jambo muhimu sana,’’anasema.

Licha ya yote hayo aliyopitia mpango wake wa badae, ni kuja kugombania tena uongozi na kupata matumaini ya kuja kushinda kwasababu ameshapata taaluma ya uwongozi.

Anaona kuwa, wanawake wanaopate fursa ya kugombea ni lazima wapewe elimu ya kutosha, kwanza kuyajua mazingira ya siasa, pili kuelimishwa kuwa unapoomba unaweza kupata au kukosa, ambapo ni sawa na asiyeomba ana hakika ya kukosa.

‘’Wapo wanawake wanadhani kama vile hawana haki ya kugombea, na wanaona kuna familia ama watu maaluma ndio wenye haki ya kugombea, jambo ambalo sio sahihi,’’anasema.

"Nasaha zangu kwa wanawake wanzangu waliopo madarakani  wawashajiishe wanawake wengine, ili nao waweze kugombania na kuondoa hofu, na waendelee kufanya vizuri katika majukumu yao kwasababu itawasaidia  kuwepo kwa  wigo kwa wanawake wegine,’’anasema.  

"Wanawake tukiwa wengi katika uongozi tutapata fursa ya kutoa mawazo na ushauri kuhusiana na maswali yanayowahusu wanawake na watoto na jamii kwa ujumla kina mama ni lazima tubadilike uongozi ni tunu gombea uongozi uwe mtetezi wa wanawake wengine,’’anaeleza.

 Mwakilishi wa Jimbo la Konde Pemba, Zawadi Amour Nassor, anasema ametumia njia mbalimbali ya kuweza kutatua vikwanzo ambavyo amepitia kwa lengo la kuwa kiongozi.

"Kwanza sikukata tamaa, wakati nilipokuwa nagombania, maana kwa vile nilishawafuata walionitangulia, waliniambia ambayo yanawezakujitokeza katika safari yangu ya siasa,’’anasema.

Profesa Issa Haji Zidi, alifafanua kuwa dini ya kuislamu haijakataza kuwepo kwa kiongozi mwanamke isipokuwa mwanamke anatakiwa kufata taratibu na sheria za kiislamu.

Anaeleza kuwa katika enzi za Mtume Muhammad (S.A.W ) mwanamke alikuwa kiongozi katika vita na mambo mengine tofauti na kote aliweza kufanikisha.

"Mwanamke wa mwanzo aliyeshika na kukubaliwa wadhifa wa ushauri kwa Mtume (SAW) alikuwa mama yetu mkubwa, Sayyidatuna Khadija binti Khuwayld (RA), ambaye alikuwa mshauri wake mkuu,’’anafafanua.

 Hapa Mratibu  wa kuinua wanawake katika uongozi kutoka chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania  (TAMWA Zanzibar), Mariyam Ame, anasema wanatoa elimu mbalimbali, kwa wanawake ambao wanahitaji kuwa kiongozi, ili wajitambua na kutatua changamoto za kiuongozi.

"Nahii inawapa hamasa na kuweza kutambua haki zao za kidemokrasia, ikiwemo haki ya kupata elimu afya pamoja na miundombinu .

Maryam anasema hadi sasa zaidi ya wanawake 172 wamepatiwa mafunzo ya uwongozi kutoka Unguja na Pemba, pamoja na kutambua vikwazo na namna ya kukabiliana navyo.

Aidha aliwanasihi wanawake wanaotaka kuingia kwenye uongozi kutokuwa na hofu, kama Katiba inavyosema katika serikali zote mbili inavyoelezea pamoja na mikataba mbalimbali ya kitaifa na kikanda pamoja na kuwa karibu na chama chake.

                         MWISH0

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch