Skip to main content

WANAKONGAMANO: ‘’TUITUMIENI TUME YA KUREKEBISHA SHERIA KUTOA MAONI KWA SHERIA MUITAKAYO’

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANANCHI kisiwani Pemba, wameshauriwa kuitumia Tume ya Kurekebisha sheria wanapokuwa na vikao vyao vya kupokea maoni, ya kutaka kurekebishwa sheria, ili kuwa na sheria zinazoendana na dunia ya sasa.

Ushauri huo umetolewa na wanakongamano la siku moja, la kuelekea siku 16 za kupinga ukatili na udhalilishaji, lililoandaliwa na Jumuiya ya wasaidizi wa sheria, wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’, na kufanyika ukumbi wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba.

Walisema, ni vyema wananchi wanapokutana na Tume hiyo, kuacha jazba na kuzitolea maoni sheria, ambazo zimeshapitwa na wakati, ili kueleza wanavyotaka ziwe, kwa mujibu wa mazingira ya sasa.

Mjumbe wa Jumuiya ya TUJIPE Pemba, Sheikh Abdalla Nassor Maulid, alisema utoaji wa maoni katika tume hiyo, ni njia muhimu kwa jamii kuwa na sheria rafiki.

‘’Tume ya kurekebisha, hupita katika maeneo yetu, sasa sisi wananchi tuitumieni ili kutoa maoni, juu ya sheria ambayo tunaihisi imeshapitwa na wakati,’’alieleza.

Kwa upande wake Abdull-atif Abdalla Salim kutoka ofisi ya Mufti Mkuu, alisema moja ya eneo ambalo, linaendelea kuwakosesha haki wanawake na ucheleweshaji wa mirathi.



‘’Ijapokuwa hata sheikh, aliyepo mtaani anaweza kurithisha, lakini ni vizuri zaidi kuitumia Kamisheni ya Wakfu, kwa ajili ya kurithishwa maana huko hupata waraka ambao unaondoa migogoro,’’alieleza.

Kiongozi wa dini ya kikiristo Robart Migua Ndalami, alisema ili uhalifu ukiwemo wa wizi na udhalilishaji upunguwe, wanaobainika wakijirejea kufanya makosa, waadhibiwe mara mbili.

Akifungua kongamano hilo, Mkuu wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar ofisi ya Pemba, Bakari Omar Ali, alisema CHAPO imo katika kuelekae siku 16 za kupinga ukatili na udhalilishaji, kwa kukutana na viongozi wa dini na wanaharakati wiengine.

Alieleza kuwa, siku hizi ni muhimu kwa jamii na wadau wingine kuangalia mafanikio na changamoto, katika kutomeza vitendo vya ukatili na udhalilishaji.



‘’Kongamano hili ni muhimu mno kwetu, kuona wapi tumefanikiwa na wapi tunahitaji kuongeza nguvu, ili kuhakikisha kundi la wanawake na watoto, linabaki salama bila ya vitendo hivyo,’’alieleza.

Mkurugenzi wa Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, alisema nguvu za pamoja bado zinahitajika katika jamii, ili kuona matendo hayo yanakoma.

Hata hivyo ameikumbusha jamii, kuendelea kuwatumia wasaidizi wa sheria wanapokuwa na changamoto za kisheria, ikiwemo kukwama kwa kesi Polisi, kuchelewa kuchukuliwa maelezo baada ya tukio kutokea.




Alieleza kuwa, zipo taarifa kuwa, huwenda sheria ya Mila inayohusu mavazi ya hapa Zanzibar ya tokea miaka ya 60, kufanyiwa marekebisho, ili kuona inaendana na mazingira ya sasa.

Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini wa CHAPO Kassim Ali Omar, alisema malezi ya pamoja kwa jamii, ndio msingi mkubwa wa kurejesha heshima na nidhamu kwa watoto.

Hata hivyo, aliwakumbusha wananchi kila mmoja kuwa mlinzi kwa mwenzake, juu ya mjanga yaliomo ndani ya jamii, ikiwa ni pamoja na dawa za kulevya na vitendo vya ukatili na udhalilishaji.

Mapema Masaidizi wa sheria Jimbo la Chake chake Riziki Ali Hamad, alisema wakati umefike sasa, kuwepo kwa kamati maalum ya kuhamasisha urithishwaji mara baada ya kifo kutokezea.

Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba CHAPO, inaendelea na mikutano na makongamano yake, ya kuelekea siku 16 za kupinga ukatili na udhalilishaji, ambapo inakutana na makundi mbali mbali.

                                    Mwisho   

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch