Skip to main content

ZAWADI AMOUR NASSOR, MWAKILISHI KONDE ALIYEPITIA MENGI KABLA YA KUINASA NAFASI HIYO

 



NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR@@@@

KILA mwanadamu huwa na malengo katika maisha na huhitajika mipango na ujasiri kuweza kuitekeleza.

Ujasiri ni silaha nzito kuibeba, lakini ina faida kama utakuwa na sulubu ya kuibeba.

Neno ujasiri limebeba maana kubwa kwenye tafsiri ya mtu aliefanikiwa katika maisha yake.

Mmoja wa wanawake aliyeweza kupata mafanikio kutokana na kuwa na ujasiri ni Zawadi Amour Nassor .

Mwana mama huyu, ambaye ni mtoto wa kwanza katika watoto tisa wa familia yao,amezaliwa  1978 katika kijiji cha Konde Pemba na kupata elimu yake ya msingi katika Skuli ya Kinyasini, Unguja, mwaka 1991.

Aliendelea na elimu ya sekondari katika Skuli ya Konde mwaka 1994 na kupata elimu ya juu katika chuo cha Zanzibar Muslim College, Mazizini hadi ngazi ya stashahada na shahada.

Vile vile amesomea uwalimu katika Chuo Kikuu Huria Tanzania ‘OUT’.

Alisomesha katika skuli ya msingi za Pangale na Konde"A" kuanzia mwaka 2000 hadi 2020.

Jasiri huyu alianza kuwa mwalimu wa skuli ya msingi ya Konde ‘A’ na kuwa Msaidizi wa Mwalimu Mkuu katika mwaka 2015.

Kuanzia  mwaka 2018 alikuwa karibu na chama cha Wandishi wa Habari Wanawake (TAMWA) na kupata mafunzo ya masomo mbali mbali, ikiwa pamoja na kupiga vita vitendo vya udhalilishaji.

Vile vile alipata  mafunzo ya uongozi kwa mwanamke ambayo yalimjenga hadi kuingiwa ushawishi wa kujiunga na siasa katika mwaka 2019.

" Nilikuwa mjumbe katika Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania –Zanzibar (TAMWA) katika kisiwa cha Pemba.

Nilipata mafunzo mengi, yakiwemo ya kuwa jasiri katika kupigania vitendo vya udhalilishaji,’’ alisema.

Akiwa na TAMWA, Bi Zawadi ambae sasa ni Mwakilishi wa Jimbo la Konde, alisema alipata mafunzo ya uongozi kuanzia mwaka 2019.

Malengo yake baada ya kuiva kiuongozi na kugombea nafasi ya uwakilishi katika Jimbo la Konde, ingawa wapo waliomshawishi agombee viti maalum.

Kwenye kinyang’anyiro hicho walikuwa wagombea 11, kati yao wanawake watatu na katika harakati za kugombea na jina lake lilirudi kuwa mgombea.

Alieleza kuwa wazazi wake hawakupenda aingie katika siasa kwa sababu ya hofu angebadilika kitabia  na mwenendo wake wa maisha.

Hata hivyo, baba yake  alimridhia aingie kwenye siasa, lakini mama yake alikuwa na wasiwasi kwa kuhofia tabia ya kujengeana uadui,"alisema

Hivi sasa Bi Zawadi yupo mstari wa mbele kupinga udhalilishaji na upo wakati aliibua taharuki ya kudhalilishwa wanafunzi wa darasa la sita  wa Skuli ya Msingi ya Konde.

‘’Niliifuatilia kesi ya mwalimu wa madrasa kuwaingia wanafunzi na hapo mwanzo Polisi na baadhi ya wazazi hawakunielewa mpaka kesi ilipofikishwa  mahakamani,’’aliongeza.

Akiwa skuli, Bi. Zawadi alifundisha watoto jinsi ya kujilinda na vitendo viovu na kujitambua.Alifanikiwa kuwapata watoto 35 waliofanyiwa vitendo vya udhalilishaji.

Alipowaibua watoto hao, jamii iligawaika makundi. Wapo waliomuona amefanya jambo jema, na wengine walimtenga na kumsema vibaya, kwa kule kufanya kazi yake vizuri.

‘’Ukifuatilia jambo ovu ili liondoke, wao wataokuunga mkono na wengine kukulalamikia, lakini hayo sikuwajali, maana nilishaelezwa na mwalimu  wa TAMWA-Zanzibar kuwa yatajitokeza,’’ alisema.

ALIPOINGIA KWENYE SIASA

Alipoingia kwenye siasa aliwafuata watu maarufu na magwiji wa siasa kuwaomba wamsaidie na kupata mapokezi tafauti.

‘’Yuko mzee ambae sasa ni marehemu ndio mtu pekee aliyonionesha njia na kuniambia niwe makini kwenye siasa,’’alisisitiza Bi. Zawadi.

ALisema aligundua ni kwamba  wakati mwengine adui wa mwanasiasa ni mwanasia mwenzake, wakati mwengine wa chama, shehia , wadi, jimbo au mkoa mmoja.

Kilichompa nguvu Bi. Zawadi, mbali ya familia yake ni kuona baadhi ya ya marafiki zake wapo pamoja.

ZAWADI NA UWAKILISHI

Alisema mfuko wa jimbo  haukidhi matakwa ya wananchi na hili halieleweki vizuru na jamii.

Alisema anaamini mambo aliyoyafanya katika jimbo lake ni karibu kwa asilimia 90 ya mambo aliyoahidi wakati wa kampeni ya uchaguzi.

Ahadi hizi ni pamoja na kuwapatia waanchi maji safi na salama kwa kuwajengea visima nane.

 

Vile vile alisambaza huduma ya nishati ya umeme,ameshajihisha wanafunzi kuweka kipaumbele katika sekta ya elimu na kuwasaidia kwa kuwapelekea vifaa vya kusomea, kama vitabu  kompyuta.

"Nilikuja na mradi unaosema ‘tokomeza ziro na kuengeza ufaulu kwa kidato cha sita.Nikawapatia mafunzo ya ujasiria mali vijana wa kike 10 katika sekta ya ushoni,’’alieleza.

Aliwapatia vijana 43 mafunzo ya udereva katika chuo cha ‘KST’ Pemba kwa lengo la kuja madereva wazuri, wapo vijana 70 waliopewa mbinu za kujiajiri, kupitia fursa zilizopo  Pemba.

Kwenye afya, Mwakilishi huyo  aliwapelekea daktari wa magonjwa wa moyo katika hospital ya Konde pamoja na gari ya kubeba wagonjwa.

Katika michezo alisaidia kusajili timu 26 katika ligi ya Shirikisho la Kanda Zanzibar (ZFA) na kutumia shilingi milioni 4.4 na kuendelea na matengenezo ya uwanja wa mpira wa Konde.

Bi. Zawadi alisema kinachowakwaza wanawake kutoingia majimboni na kukimbilia viti maalum ni pamoja na hofu ya moyo na kuamini mwanamke akiwa kiongozi anapotosha maadili yake.

Alisema bado dunia imetawaliwa na mifumo dume, ambayo humtenga mwanamke au wakati mwingine kujiona hana haki ya kuingia kwenye safu ya uongozi.

WANAOMFAHAMU ZAWADI

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Bi. Salama Mbarouk Khatib, alisema mkoa huo umebahatika kupata mafanikio makubwa kwa sababu ya kuongozwa na watu kama Bi. Zawadi.

Mkuu wa wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya, alisema mwakilishi wa Konde ni mmoja wa viongozi anaowafuatilia kwa utendaji na kujiamini kwao.

Mbunge wa viti maalum kwa mkoa wa Kaskazini Pemba, Bi. Asia Sharif Omar, alisema Mwakilishi wa Jimbo la Konde, Zawadi Amour Nassor, ni shujaa na jasiri kwenye uongozi.

Maray Haji Khamis wa Vilima Vitatu Konde, alisema sasa wanaendelea kunufaika na huduma ya maji safi na salama, baada ya Jimbo lao kumpata Mwakilishi makini.

‘’Ametusaidia kwenye ujasiriamali, kwanza kwa mafunzo pili kutupatia mtaalamu kutuelekeza namna ya kuzalisha bidhaa bora na zinazokubalika katika soko,’’alisema.

Hivi karibuni, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, DK. Hussein Ali,wakati alipokuwa na ziara mkoa wa kaskazini Pemba, aliwataka wananchi kuendelea kuwaamini viongozi wao.

‘’Tunao wawakilishi na madiwani wachapakazi, sasa hatuna sababu ya kutokuwarejesha tena madarakani kwenye kila uchaguzi,’’alisema Dk. Mwinyi.

                     MWISHO 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch