Skip to main content

WANAWAKE WAKULIMA WA MWANI PEMBA WAMALIZA MAFUNZO YA KUOGELEA

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANAWAKE wanaolima na kilimo cha mwani cha kina kirefu, wa kijiji cha Tundaua shehia ya Kilindi wilaya ya Chake chake Pemba, wamesema baada ya kumalizika kwa mafunzo ya siku 15, sasa wanajiamini kuogelea, hadi urefu wa uwanja wa mpira wa miguu bila ya kupumzika.

Walisema, mafunzo hayo, yamewajengea uthubutu wa kuogelea na hata kuokoana, pindi ikitokezea ajali wakati wa kwenda ama kurudi kwenye shughuli yao ya kilimo cha mwani, kwenye maji yenye kina kirefu.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, kwenye bahari ya Tundaua walikokuwa wakifundishwa, walisema kwa sasa wamejitoa woga na wanajiamini kogelea hadi mita 100 (urefu wa uwanja wa mpira wa miguu), bila ya kumpunzika.

Walieleza kuwa, wazo lililoibuliwa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar kipitia Idara ya Mazingira chini ya mradi wa ‘SAPPHIRE’ umekuja kuwapa uhakika wa kazi zao.



Mmoja kati ya wanufaika wa mafunzo hayo ambae ni mkulima wa mwani wa kina kirefu, Hassina Seif Baki, alisema hakuwa na ndoto katika maisha yake, kwamba siku moja engeweza kujua kuogelea.

‘’Pamoja na kwamba mafunzo haya yatanisaidia wakati wa kuendesha shuguli zangu za kilimo cha mwani maji makubwa, lakini kujua kuogelea itanisiaida hata kuokoa wenzangu,’’alieleza.

Nae Raya Abdalla Rashid, alisema pamoja kwamba alikuwa akiendesha shughuli mbali mbali zinazohusiana na habari, lakini hakua anajua namna ya kuogelea.



Alieleza kuwa, kwa sasa anauwezo kwenda nusu na robo ya masafa ya uwanja wa mpira wa miguu bila ya kuchoka, jambo ambalo hapo kabla hakuwaliza katika maisha yake.

Nae mnuafika wa mafunzo hayo Fatma Suleiman Sinei, alisema kilichobakia kwa sasa, ni kupatiwa vifaa maalum kama vile viatu na nguo maalum za kuogelea, ili kupata urahisi wa shughuli zao.

Mwalimu wa mafunzo hayo Kaije Said Bakari, alisema wanawake hao awali walikuwa na woga na wasi wasi mkubwa wa hata kuingia baharini, ingawa baada ya mafunzo hayo, sasa wako vizuri.

‘’Nimeshahitimisha wanawake 45 ambao wameshapata mafunzo ya siku 15, baada ya kumaliza mafunzo kama hayo kisiwa cha Fundo,’’alieleza.






Hata hivyo mwalimu huyo, alisema suala la kugoelea haliwahusu wakulima wa mwani pekee, bali kila mtu anayeishi katika mzungumko wa visiwa.

Mapema Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Alawi Haji Hija, aliwataka wanufaika wa mafunzo hayo, kuhakikisha wanawapa na wenzao.

‘’Lengo la serikali, ni kuona mafunzo hayo yanawafikia wanawake wote wanaojishughulisha na kilimo cha mwani, kiwe cha maji kidogo au wale wa kina kirefu,’’alieleza.




Aidha aliwaeleza kuwa, huo ni mwanzo mzuri kwa wakulima hao, na hasa vile suala la kupatiwa vifaa na zana za kilimo cha mwani, utaratibu wa wizara husika unaendelea.

Katika hatua nyingine, Kaimu huyo wa Idara ya Mazingira Zanzibar, alimpongeza mwalimu huyo kwa ujasiri wake, wa kuacha familia zake na kuwafundisha wanawake wenzake, jinsi ya kuogelea.

Alieleza kuwa, mradi huu kwa sasa unatekelezwa zaidi kisiwani Pemba, katika ukanda wa mkondo wa Pemba PECA, ambapo maeneo hayo yameshaathiriwa, na kukosekana kwa mapato kwa wakulima wa mwani wanaolima maji kidogo.

Mratibu wa mradi huo Aisha Abdalla Rashid, alisema wakulima walikuwa wakilima mwani katika maji madogo, na yanapotoka huathiriwa na pia kuwa na mavuno kidogo.




‘’Kwa changamoto hiyo, ndio Idara ya Mazingira ilipotafuta mradi maalum, ili kulima eneo dogo lenye mavuno makubwa, na hasa baada ya kukamilisha mafunzo ya kuogelea,’’alieleza.

Hata hivyo Mratibu huyo, alimpongeza mfukufunzi wa mafunzo hayo, kwa kuongeza idadi ya wanawake waliopatiwa mafunzo hayo, kutoka 40 hadi 45, katika shehia za Fundo na Kilindi kisiwani Pemba.

                                  Mwisho  

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch