Skip to main content

HAMA HAMA WATUMISHI WA UMMA, IPA YAGUNDUA JAMBO

 

 
NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

CHUO cha Utawala wa Umma Zanzibar ‘IPA’ kimegundua sababu mbali mbali, zinazowafanya watumishi wa umma, kuhama sehemu moja kwenda nyingine, ikiwemo mabadiliko ya sayansi na teknolojia.

IPA imegundua sababu nyingine kuwa ni, miundo ya kiutumishi, maslahi na ndoa kwa watumishi wanawake na wanaume, kwa kumfuata mwenzake sehmu alipo kimakaazi.

Hayo yameelezwa leo Disemba 8, 2023, na Mkuu wa Divisheni ya Utafiti na Ushauri Elekezi kutoka ‘IPA’ Haji Jumbe Haji, wakati akizungumza kwenye uwasilishaji wa matokeo ya awali wa tafiti nne walizozifanya, kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa Chuo, hicho mjini Chake chake.

Alisema, sababu hizo na nyingine, zinazowafanya watumishi wahame kutoka sehemu moja kwenda nyingine, wakati mwingine huathiri mtiririko mzuri wa kazi za sekta ya umma.




Alisema, tafiti hizo ambazo walizifanya katika mwaka wa fedha wa 2020/2021, zilichukua takriban miezi sita hadi kukamilika kwake, ambapo watendaji mbali mbali wa sekta za umma za Unguja na Pemba, walihojiwa.

‘’Hama hama ya watumishi wa umma, imekuwa ikijitokeza kwa kasi kadiri pia mabadiliko ya kiutendaji yanavyowekwa mazingira rafiki, ikiwemo vifaa vya kisasa,’’alifafanua.

Alizitaja tafiti hizo kuwa ni ‘uanzishwaji na utekelezwaji wa mifumo ya kielektroniki katika utumishi wa umma, usalama na utunzaji kumbu kumbu za serikali, uwezo wa serikali za mitaa, katika kutoa huduma kwa jamii na kuangalia sababu za watumishi wa umma kuhama kutoka sehemu moja kwenda nyingine.

Akifungua hafla hiyo, Afisa Mdhamini wizara ya Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Pemba, Halima Khamis Ali, alisema hakuna kitu ambacho, kinaweza kuleta mageuzi pasi na kufanyika utafiti.





Alisema, kikao hicho ni muhimu kwa wadau hao wa Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar ‘IPA’ kupata kusikiliza utafiti huo na matokeo ya awali na kisha, kutoa maoni yao, kwa ajili ya kuimarisha zaidi.

Alieleza kuwa, moja ya kazi kubwa ya IPA, ni kuishauri serikali kuu, juu ya uimarishaji katika sekta ya umma, ili kuhakikisha mifumo iliyopo inakuwa rafiki, kwa watumishi wa umma wa kada zote.

‘’Utumishi wa umma ni rasiliamali muhimu ndani nchi yetu, na ndio maana IPA, kimepewa jukumu la kuhakikisha wanachoona hakiendi sawa, ni kuishauri serika na kufanyiwa mapitio ya haraka,’’alieleza.

Alifahamisha kuwa, mifumo ya serikali kama ya ukusanyaji mapato, uendeshaji wa shughuli za kila siku ‘e-government’, zan-malipo, uhifadhi wa kumbu kumbu, zinahitajika kuangaliwa kila baada ya muda.

Hata hivyo, Afisa Mdhamini huyo, aliupongeza uongozi wa IPA, kwa kutekeleza majukumu yao mbali mbali, licha ya changamoto zinazowakabili.

Aidha aliwataka wadau hao, kutoa maoni yao ambayo yatasaidia kuimarisha utafiti huo, ambao baadae utawasilishwa serikali kuu kwa ajili ya kufanyiwa kazi.





Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar ‘IPA’ tawi la Pemba Juma Haji Juma, alisema uwasilishaji wa matokeo hayo ya awali, na maoni ya wadau hao, yatasaidia kuongeza ufanisi katika utafiti wao.

                               Mwisho  

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch