Skip to main content

WAVUVI WA DAGAA WESHA WATAKIWA KUZINGATIA HILI KWANZA.................



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WAVUVI wa dagaa wa shehia ya Wesha wilaya ya Chake chake Pemba, wamekumbushwa kujiwekea mazingira ya usafi, kuanzia nguo wanazovaa, madau yao pamoja na vyombo vyingine wanavyotumia, ili kuliongezea thamani dagaa lao.

Ushauri huo umetolewa leo Disemba 6, 2023  na Mratibu wa Mradi wa Kuimarisha Jamii kwa kuzingatia Ikolojia na shughuli za kijipatia kipato, kwa wavuvi wadogo katika eneo la hifadhi ya mkondo wa Pemba ‘’SAPPHIRE’ Aisha Abdalla Rashid, alipokuwa akifungua mafunzo, kwa wavuvi hao, yaliyofanyika ukumbi wa Manispaa ya Chake chake.

Alisema, kwa sasa ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar kupitia Idara ya Mazingira, chini ya mradi huo wa ‘SAPPHIRE’ imeamua kukutana na wavuvi na waanika dagaa, ili kujengea uwezo kwa lengo la kuongeza thamani.





Alieleza kuwa, moja ya jambo hilo ni usafi wa wavuvi, kuanzia nguo wanazovaa wakati wanapokwenda kwenye shughuli zao za uvuvi, madau yao na ndoo wanazotumia.

‘’Usafi wa bidhaa ya dagaa kavu au bichi, huanzia kwa mvuvi mwenyewe, na kisha usafi huo, uendelee kwa mkaushaji ama mchemshaji wa dagaa kabla ya kulipelekea sokoni,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Mratibu huyo wa mradi wa ‘SAPPIRE’ alisema mradi huo, ambao unafadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa na Uhifadhi wa Mazingira ‘UNEP’ moja ya malengo yake, ni kuandaa mpango shirikishi wa rasilimali bahari.

‘’Lengo jingine ni kuendeleza uhifadhi wa eneo la Mkondao wa Pemba PECCA, pamoja na kusaidia shughuli mbadala za kujipatia kipato kwa waanikaji na wavuvi wa dagaa,’’alifafanua.

Mapema Kaimu Afisa Mkuu Idara ya Maendeleo ya Uvuvi na Mazao ya Baharini Pemba Mayasa Hamad Ali, wakati akitoa mada ya njia ya bora za uanikaji dagaa, alisema ziko njia mbali mbali, moja wapo ni utumiaji wa moshi.




Alisema, njia hii hutumia magamba ya miti isiyokuwa na sumu, ambayo dagaa huwekwa juu, na moshi mwepesi mwepesi kupenya kwenye dagaa, na kukauka taratibu.

‘’Na njia hii hasa wakati mwingine, hutumika sana kipindi cha mvua, kwa kuhofia dagaa lisiharibike kwa kukosa jua, tena wapo wateja wanalipenda zaidi hili, kuliko la kukausha kwa jua,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, mtoa mada huyo alieleza kuwa, njia nyingine ambazo zinakubalika katika uanikaji wa dagaa, ni kuchemsha kwa maji na chumvi na kisha kulianika kwa jua.

‘’Njia hii ni nzuri, lakini lazima waanikaji wazingitie usafi, ikiwemo kabla kulikosha vyema na kuondoa taka taka na chango za wadudu, ili likishakauka, lipendeze kwa mlaji,’’alieleza.

Hata hivyo alifafanua kuwa, haishariwi kulianika dagaa kwenye sakafu chafu na inayongia mavumbi na kuruhusu wanyama waharibifu, kwani hupoteza thamani kwa wateja.

‘’Hakuna uhusiano wowote, kati ya dagaa kavu na kujaa mavumbi mavumbi kwani, baadhi ya wateja hupendelea kula kama lilivyo, hivyo lazima tuwalinde wateja wetu,’’alifafanua.

Mwanikaji dagaa Salim Juma Omar, alisema moja ya sababu za dagaa kuanza kuharibika na kupoteza thamani, ni wavuvi kulichelewesha kulipeleka sokoni.

‘’Wakati mwingine, baadhi ya wavuvi hilichanya dagaa walilolivua saa kadhaa zilizopita na jipya, hapo ndio athari huanza kujitokeza na kusababisha athari kwa wateja,’’alieleza.

Kwa upande wake, mfanyabiashara wa dagaa Sabra Massoud Ali, alisema changamoto kubwa inayowakabili, ni ukosefu wa wateja wa uhakika, ambapo wakati mwingine, hukaa na dagaa zaidi ya miezi mitano bila ya kuliuza.



Mafunzo kama hayo, tayari wameshapewa wavuvi na waanikaji dagaa wa shehia ya Ndagoni wilaya ya Chake chake, pamoja na kukabidhiwa vifaa kama vile chanja za kisasa za kuanikia dagaa, ndoo na vyombo maalum ya kuchemshia dagaa.

                                Mwisho


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch