Skip to main content

WAANIKAJI DAGAA NDAGONI WAPIGWA MSASA

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WAANIKAKAJI dagaa wa shehia ya Ndagoni wilaya ya Chake chake Pemba, wameshauriwa kuzitumia njia nzuri za uanikaji, ikiwemo kutumia chanja za miti zilizoinuka ‘chanja’ ili kuepusha vumbi na taka taka, zinzoweza kupunguza thamani ya bidhaa hiyo.

Walielezwa kuwa, njia nyingine ambayo ni nzuri kwa uanikaji na kutumia sakafu iliyasafi, ambayo ni vyema ikazungumshiwa kinga maalum, ambayo itazuia taka taka na wanyama kuliharibu wakati wa uanikaji.

Hayo yamelezwa na Kaimu Afisa Mkuu Idara ya Maendeleo ya Uvuvi na Mazao ya Baharini Pemba Mayasa Hamad Ali, wakati akitoa mada njia ya uanikaji bora dagaa, kwa waanikaji na wavuvi wa shehia ya Ndagoni, mafunzo yaliyofanyika ukumbi wa Manispaa ya Chake chake.

Alisema, njia nyingine ambayo waanikaji wanapaswa kuitumia ni kutumia wavu, ambao kitaratibu hutakiwa kuwekwa juu juu, ili kuhakikisha dagaa haliingii wadudu na taka taka.



Alieleza kuwa, njia hizo pamoja na ile ya kutumia moshi kwa magamba ya miti maalum, ndio ambazo zinasaidia kulitia thamani dagaa, wakati linapopelekwa kwa wateja.

‘’Niwaombe sana kuwa, kwa wale ambao watatumia chanja, ni vyema zikawa za miti, na sio zile za vyuma kwani zikipata unyevu hutoa maji maji ‘kutu’ ambazo ni hatari kwa walaji,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Kaimu Afisa huyo Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Uvuvi na Mazao ya Baharini Pemba, Mayasa Hamad Ali aliwataka wavuvi wa dagaa, kujenga utamaduni wa usafi kuanzia nguo na vyombo vyao.

Alieleza kuwa, vyombo kama ndoo wanazobebea dagaa wahakikishe, wazisafishe kila siku, kabla ya kuingiza dagaa jingine, wakifanya hivyo wataepusha uoza wa dagaa lao usiokuwa wa lazima.

‘’Wavuvi waliowengi, wamekuwa hawazingatii usafi, jambo hili husababisha dagaa kupata unyevu unyevu na kupelekewa kuzaliwa minyoo, yanayoharikisha uozaji wa dagaa,’’alifafanua.

Akifungua mafunzo hayo, Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa rais Zanzibar Alawi Haji Hija, alisema mafunzo hayo ni maalum kwa waandikaji dagaa, ili kuongeza mnyororo wa thamani, wa kazi yao.



Alieleza kuwa, waanika dagaa wamekuwa wakikumbwa na changamoto za kutokuwa na thamani ya dagaa lao, jambo lililokuwa, likishusha thamani ya bidhaa zao.

‘’Mafunzo haya ni maalum, kwa ajili ya kuchapuza mnyororo wa thamani, maana sasa serikali kuu inatekeleza kwa vitendo, dhana ya uchumi wa buluu, hivyo haya ni sehemu ya kukuza soko,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, alieleza kuwa waanika dagaa hao, kisha watatakiwa kuwafikishia wenzao elimu hiyo, ili iwafikie wengi zaidi kwa mujibu wa mahitaji yao.

‘’Na mafunzo haya zaidi yamewalenga waanika dagaa kutoka shehia ya Ndagoni, kwani ndio ambao wanakusanya idadi kubwa ya waanika dagaa hao na wavuvi kuliko eneo jingine,''alieleza.

Alifafanua kuwa, mafunzo hayo yatawasaidia kujua mazingira rafiki ya uanikaji dagaa, ili kuepusha taka taka na mavumbi, yanayosababisha kupungua thamani ya dagaa lao.

Hata hivyo alisema, serikali bado inaendelea kuthamini kwa vitendo wavuvi na waanika dagaa, kwani inayodhamira ya kuongeza thamani na pato kwa wananchi, walioekeza kwenye sekta hiyo.

Akiwasilisha kazi za vikundi, muanika dagaa kutoka shehia ya Ndagoni Hakim Hamad Mmanga, alisema changamoto kubwa inayowakabili, ni ukosefu wa vifaa rasmi vya kuanikkia.




‘’Nyingine alisema ni ndege kama Kunguru na wingine wamekuwa wakiharibu dagaa lao, wakati wanapolianika na kusababisha kuingia taka taka,’’alieleza.

Kwa upande wake mshiriki Abdull-hakim Salim Ali wamekuwa wakitumia njia tatu kuu za ukaushaji dagaam ikiwemo kuanika kwa jua, kaunika kwa jua baada ya kuchemshwa na kutumia moshi.

‘’Njia hii ya kukausha kwa moshi, kwanza dagaa hukoshwa, hitiwa viungo kama chumvi, pili pili na kisha kuingizwa kwenye mtambo maalum,’’alifafanua.




Mafunzo hayo ya siku moja, ni muendelezo wa juhudi za serikali katika kuangalia njia bora za kukuza pato la wavuvi na hasa wa sekta ya uanikaji wa dagaa na wavuvi wao.

                                 Mwisho     

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch