Skip to main content

WIZARA YA AFYA YAPEWA NENO KUFANYAKAZI NA WAANDISHI WA HABARI

 



Na Nafda Hindi@@@@

 

Wizara ya Afya imeombwa kutoa mashirikiano mazuri kwa waandishi wa habari kwa lengo la kuleta mabadiliko katika jamii.

 

Akizungumza wakati wa uwasilishaji ripoti  ya elimu ya Afya ya Uzazi kwa wasichana na wanawake wa mjini na vijijini katika ukumbi wa Kificho Mwanakwerekwe Mkurugenzi wa chama cha waandishi wahabari wanawake Tanzania Zanzibar Dk. Mzuri Issa amesema watendaji wa Wizara husika kuepuka tabia ya usiri wa kutotoa taarifa muhimu zinazogusa maisha ya watu.

 

“ Kuna usiri wa taarifa kwa baadhi ya watendaji hivyo tunaiomba Wizara ya Afya iendelee kutoa mashirikiano mazuri kwa waandhishi wahabari kwa sababu masuala ya kinchi nay a kijamii ni lazima yasikike kupitia vyombo vya habari,’ Dk Mzuri Issa, Mkurugenzi TAMWA,ZNZ.

 

Dk Mzuri amesema  masuàla yànayohusu nchi pàmoja na jamii lazima yasikike kupitia vyombo vya habari kwa wananchi kupaza sauti zao

 

“ Ni haki ya kila mtu kupata taarifa na uhuru wa kujieleza na katiba zote mbili zimeeleza ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ya Zanzibar na hata kidunia tumesaini mikataba  mbali mbali ya Kimataifa ikiwemo Africa Charter, Dk Mzuri Issa.

 

Mapema akiwasilisha ripoti hiyo Afisa Tathmini na Ufatiliaji Abdul Mohamed kutoka TAMWA ZNZ amesema ripoti hiyo imengunduwa mapungufu kadhaa kama vile ukusanyi wa takwimu zà uhakika pamoja na umri zinazohusu wanawake na wasichana zinazoonesha vifo wakati wa kujifunguwa.

 

“Baadhi ya mafungufu ni kutokuwepo takwimu sahihi za vifo na umri kwa wanawake na wasichana, tunaomba Wizara ya husika lifanyie kazi”, Abdul Mohamed.

 

Nae Afisa mradi wa kuendeleza utetezi kwa vyombo vya habari kwa wasichana na wanawake kutoka TÀMWA ZNZ Zaina Abdalla Mzee amesema lengo la mradi huo ni kuibuwa changamoto zinazowakuta kundi hilo pamoja na  vituo vya Afya na kuzitafutia ufumbuzi kwa wahusika.

 

“Tulianza kwa kufanya utafiti na kugunduwa waandishi wengi hawana uelewa juu ya masuala ya Afya ya uzazi hivyo tuliandaa mafunzo ya kuwajengea uwezo na sasa wanaripoti vyema habari hizi na wanasaidia jamii kupata huduma stahiki,” Zaina Mzee.

 

Nao watendaji kutoka Wizara yà Afya Zanzibàr wamekiri kuwepo kwa baadhi ta changamoto katika sekta hiyo ikiwemo bajeti ndogo ukilinganisha na mahitaji ya wananchi.

 

Hata hivyo wàndishi wahabari waliopatiwa mafunzo kupitia mradi huo wamesema wanakabiliwa na changamoto wakati wa kuandaa habari pamoja na vipindi kwa bàadhi ya wandendaji wa Wizara hiyo kutotoa mashirikiano.

 

“ Changamoto zinakuja kwa baadhi ya watendaji kutupiga danadana wakati wa kukusanya hizi taarifa kwa hivyo inatuwia vigumu kuzipata kwa muda sahihi na nyengine hazipatikani kabisa,” Waandishi wa habari.

 

 

Mradi wa kuendeleza utetezi wa haki ya elimu ya Afya ya uzazi kwa vyombo vya habari kwa wasichana na wanawake  unaotekelezwa na TAMWA ZNZ ulitowa mafunzo kwa waandishi wa habari 71 na wahariri 23 kwa Unguja na Pemba ambapo ulioanza Octobet 2022 na kumalizika October 2023 ulitekelezwa kwa Wilaya ya Magharibi "B" na Kati kwa Unguja na Wilaya ya Chake Chake kwa Pemba.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch