Skip to main content

PEGAO, TAMWA YATOA RAI KUEPUKA VYETI 'FEK'

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WAKALA wa usajili na matukio ya kijamii Zanzibar, wilaya ya Chake chake, imekumbushwa kuwatumia waandishi wa habari na wadau wengine wa haki za binaadamu, ili kufikia jamii kwa lengo la kuielimisha na kuepukana na vyeti na vitambulisho vyenye mgogoro miongoni mwao.

Wito huo ulitolewa leo Oktoba 17, 2023 na Mkurugenzi wa mradi wa kuihamasisha jamii kudai haki zao za uongozi, siasa na demokrasia ‘SWIL’ kutoka Jumuiaya ya Utetezi wa Mazingira na Jinsia ‘PEGAO’ Hafidh Abdi Said, kwenye mkutano wa kuwasilisha kero, zilizoibuliwa na wahamasishaji, uliofanyika ofisi ya TAMWA Mkanjuni Chake chake.

Alisema kuwa, kutokana na jamii kutokuwa na ufahamu wa kutosha juu ya vielelezo hivyo, kumepelekea kuwepo kwa tatizo kubwa ambalo linahitaji kufanyiwa kazi, ili liweze kuondokana nav yeti bandia na vitambulisho vye mgogoro.

Alieleza kuwa, tatizo hilo limekuwa ni la muda mrefu katika jamii, hivyo ni wakati sasa Wakala wa usahili na matukio ya kijamii kufanyaka kazi zao kwa karibu na vyombo vya Habari, ili jamii itambue kasoro zao.

Mkurugenzi huyo alieleza kuwam jambo hilo sasa limekuwa kubwa na kwamba ni kosa linalosababisha athari kubwa, ikiwemo watu kucheleweshewa kupata haki zao, kukosa mikopo, safari za kimatibabu kutokana na kasoro iliyomo kwenye nyaraka hizo.



‘’Niwaombe sana wenzetu wanaoshughulikia vitambulisho, vyeti vya kuzaliwa, takala, ndoa na nyaraka nyingine za serikali, kuanzisha mpango maalum na endelevu ili kuhakikisha jamii inapata uwelewa wa kutosha,’’alishauri Mkurugenzi huyo.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi wa mradi huo Hafidh Abdi Said, alieleza kuwa ujio wa mradi huo umekuwa ukisaidia kuibua changamoto nyingi kwa jamii, ikiwemo vyeti na vitambulisho vyenya kasoro, ukosefu wa huduma za kijamii Pamoja na jamii kulalamikia utaratibu mbovu kwa vaadhi ya tasisi za serikali.

Mratibu wa Chama cha waandishi wa Habari Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hiya Mussa Said, alisema kuwa mradi huo wa SWILL unahamasisha na kuwawezesha jamii, katika kupata haki zao stahiki, bila pingamizi zozote na sio kwenye nafasi za uongozi pekee, kama ilivyozoeleka kwa baadhi ya watu.

Hivyo waandishi wa habari na wadau wengine kuona kwamba kuna umuhimu mkubwa kwao, kuifikia jamii kuwapa elimu juu ya haki mbali mbali za jamii.




‘’Mradi huu umekuja kuibua changamoto ambazo kwa njia moja ama nyingine zinamsahaulisha mwanamke kugombea, kudai haki zake za kisiasa na kijamii,’’alifafanua.

Mapema akiwasilisha changamoto zilizoibuliwa na wahamasishaji jamii, juu ya kudai haki zao za uongozi demokrasia na siasa, mtoa mada Khalfan Amour Mohamed alieleza kuwa, bado jamii inatatizo la uelewa mdogo juu ya haki yao ya vyeti vya kuzaliwa na vitambulisho vya mzanzibari mkaazi.

‘’Imebainika kuwa, kuna utamaduni kwa baadhi ya watu kuwatuma wengine kuwafuatilia zao, hivyo kama kuna kasoro inakuwa vigumu kubaini na kisha kurudi kwenye mamlaka husika,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, amewakumbusha wazazi na walezi, kuwa makini wakati wanapowasilisha taarifa za watoto wakati wa kuandikishwa skuli, kwani taarifa hizo hutumika hata baada ya kumalizika kwa masomo.




Hata hivyo aliwataka wananchi wasikubali kuwatumia wasiokuwa wafanyakazi wa mamlaka husika, katika maeneo mbali mbali wanayokwenda kutaka huduma za umma.

Nae Afisa Elimu na Mafunzo ya Amali mkoa wa kusini Pemba, Mohamed Shamte Omar, amezitaka taasisi husika zinazosajili matukio ya kijamii, kuondosha vikwazo pale inapotokezea changamoto mbali mbali, ili jamii isikate tamaa na ofisi hiyo.

Mapema Afisa kutoka Wakala wa Usajili na Matukio ya Kijamii wilaya ya Chake chake Yussuf Iddi Faki, alisema lawama zinazoelekezwa kwao sio sahihi, kwani wao wamekuwa wakiandika taarifa wanazopewa na mlengwa.

‘’Sisi taarifa ambazo zimo kwenye vitambulisho, vyeti vya kuzaliwa, vyeti vya kifo, ndoa na talak azote hupewa na jamii husika na uthibitisho wake wa kina, sasa ikitokezea kuna shida ya jina ni mwananchi mwenyewe ndio muhisika,’’alieleza.

Nao waandishi wa habari kutoka vyombo tofauti Salimu Ali Mselem na Essau Saimon Kalukubila, walieleza kuwa, watakuwa wajumbe kwa jamii, kuona wanaelimisha juu ya madhara ya kuwa na vielelezo visivyorasmi wakati wa kutengeneza nyaraka za serikali.

 Mwisho   

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch