Skip to main content

MAOFISA WIZARA YA AFYA PEMBA ROHO KWATU KUFANYA KAZI NA WAANDISHI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MAOFISA wa wizara ya Afya Pemba, wamesema sasa wako tayari kuzidisha ushirikiano kati yao na vyombo vya habari, kwa ajili ya kuwapa taarifa wananchi, juu ya shughuli mbali mbali zikiwemo za haki ya afya ya uzazi.

Walisema, waandishi wa habari, ndio wasemaji wa wasio kuwa na suati, hivyo suala la kuongeza ushirikiano, kwa hilo wako tayari wakati wowote na kwa jambo lolote.

Wakizungumza kwenye mkutano wa ufungaji wa mradi wa Haki ya afya ya uzazi, uliofanyikwa ofisi ya Chama cha waandishi wa Habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba, walisema ni vyema, waandishi wakawafika wanapowahitaji kwa kutengena Habari mbali mbali.

Walisema kupitia mradi huo, waandishi wa Habari walisaidia mno kuharakisha upatikanaji huduma, kama za afya ya mama na mtoto,  huduma za kuchuunguza afya hasa kwa virusi vya Ukimwi, jambo ambalo limewasaidia wananchi

Daktari wa wilaya ya Chake chake ‘DMO’ Sharif Hamad Khatib, alisema kwa mfano suala la kukatika kwa huduma ya maji safi na salama kituo cha Afya Wesha, ambalo liliibuliwa na waandishi wa Habari, limesaidia mno.

‘’Kwa huduma ya maji safi na salama sasa imerejea, na wanaokwenda kujifungua, ingawa hakutakiwa kupeleka maji, lakini kwa ujumla huduma imerejea, baada ya timu ya Waandishi wa Habari, iliyoratibiwa na TAMWA, kwenda kuibua changamoto hiyo,’’alisifia.

Aidha Daktari huyo alisema, kimsingi na kiafya hata hospitali ikose huduma ya maji safi na salama, hatakiwi mzazi ama mgonjwa mwengine, kupeleka huduma ya maji, na badala yake wizara ndio yenye jukumu hilo.

Mratibu wa Kitengo Shirikishi cha Afya ya Mama, mtoto na Lishe Pemba Mkasha Hija Mkasha, alisema waandishi wamekuwa wakisaidia mno, ili kuhakikisha hakuna anayejifungulia nyumbani.

‘’Waandishi wa Habari karibuni ofisini kwetu, kufanya makala, vipindi na habari nyingine, juu ya haki ya afya ya uzazi kwa mama na mtoto, kwani haya ndio ambayo jamii, wanapaswa kuyajua,’’alieleza.


Kwa upande wake, Mratibu kitengo Shirikishi Ukimwi, Kifua kikuu, Homa ya Ini na Ukoma Pemba Dk. Khamis Hamad, alisema kupitia mradi huo kwa upande wa Unguja, kuliibuliwa uhaba wa vifaa vya kuchunguuzia virusi vya Ukimwi, jambo ambalo liliwasaidia kupatikana kwake.

‘’Sisi ilikuwa tunajua kuwa baadhi ya vituo vya afya vifaa hivyo ‘HIV kits’ havipo, lakini ile habari ilipotoka, hakuna aliyelala ofisini, kwa sasa vifaa hivyo vimesharejea, hivyo mliwasaidia wahitaji,’’alieleza.

Akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano huo, Mratibu wa TAMWA ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said, alisema mradi huo umekuja, baada ya jamii na waandishi wa habari kutokuwa na uwelewa mpana wa haki ya afya ya uzazi.

 ''Kuanzia mwezi Aprili hadi Juni mwaka huu, TAMWA ilifanya utafiti katika vyombo vya habari, na kugundulika kuwa, waandishi hawana uwelewa wa kutosha, juu ya haki ya afya ya uzazi,’’alifafanua.


Mratibu wa mradi wa haki ya afya ya uzazi kutoka TAMWA-Zanzibar Zaina Abdalla Mzee, alisema mradi huo wa majaribio, kwa sasa unaelekea kufikia ukingoni, kwa vile ulikuwa ukitekelezwa kwa mwaka mmoja.

‘’Mradi huu, ulikuwa unatekelezwa katika wilaya ya Chake chake kwa Pemba na wilaya ya Magharibi ‘B’ na Kati kwa Unguja, na jamii imefikiwa, maana vipo vipindi 24 vya redio makala zaidi ya 35 pamoja na zaidi ya habari mchanganyiko 50 kwenye mitandao ya kijamii zilizoandikwa,’’alifafanua.


Hata hivyo Mratibu huyo, alisifia wazo la maofisi hao wa wizara ya Afya la kuwakaribisha waandishi wa habari katika ofisi zao, kwani moja ya changamoto zilizoonekana katika utafiti mdogo, ni ushirikiano unaolega lega baina ya pande hizo.

Akiwasilisha ripoti ya utekelezaji wa mradi huo, Afisa Ufuatiliaji na Tathmini kutoka TAMWA Zanzibar Abdull-rahman Mohamed, alisema inaonesha uwepo wa mafanikio kwa jamii, baada ya waandishi wa habari kuandaa vipindi na makala.


Alieleza kuwa, lengo hasa la mradi huo, ilikuwa ni kuwajengea uwezo waandishi wa habari, ili waandike kwa uweledi juu ya haki ya afya ya uzazi, ambao walengwa wakuu ni wasichana na wanawake.

Waandishi wa Habari akiwemo Essau Saimon Kalukubila wa redio jamii Micheweni na Sheikh Rashid Seif wa Shirika la Utangaazaji Zanzibar ZBC, waliahidi kuendelea kuwaelimisha wananchi.

Maradi huo wa majaribio wa mwaka mmoja, uliendeshwa katika wilaya za Magharibi ‘B’ na Kati kwa Unguja na wilaya ya Chake chake kwa Pemba.

Ambapo mradi unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya TAMWA-Zanzibar na wenzao wa Tanzania bara, unafadhiliwa na Shirika la Wellspring Philonthropic fund la Marekani

Shabaha kuu ya mradi huo ni kuwajengea uwezo waandishi wa habari, ili kuripoti kwa ufanisi, juu ya haki ya afya ya uzazi kwa wanawake na wasichana walioko mjini na vijijini.

Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch