Skip to main content

WAZAZI, WALEZI WAWAPA TANO WAALIMU CONNECTING, KAZI IENDELEE

 









NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WAZAZI na walezi wenye watoto wao skuli ya sekondari ya Connecting Continent ya Mgogoni wilaya ya Chake chake, wamesema wameridhishwa na juhudi binafsi za waalimu, katika kuwafundisha wanafunzi skulini hapo.

Wakizungumza kwenye mkutano maalum uliofanyika skulini hapo, wenye lengo la kupokea matokeo ya muhula wa kwanza, wazazi na walezi hao, walisema kutokana na ugumu wa wanafunzi ulivyo, wanaridhishwa na juhudi zao.

Walisema, wengi wao wamekuwa wakikosa muda wa kuwauliza watoto wao juu ya maendeleo ya elimu, lakini waalimu hao, wamekuwa wakibuni mbinu za kuwaendeleza wanafunzi.

Wazazi hao walieleza kuwa, kwa muhula huu kwanza, wameridhishwa na matokeo hayo, ambayo kwa yale ya darasa la 12, kama yengekuwa ndio ya mitihani ya taifa, kusingekuwa na mwanafunzi aliyefeli.

Mmoja kati ya wazazi hao Omar Mjaka Ali, alisema kama sio juhudi za waalimu hao na mbinu mbali mbali za kuwalazimisha wanafunzi kusoma, matokeo ya muhula wa kwanza, yasingekuwa mazuri.

‘’Mimi niseme kuwa, jinsi wanafunzi walivyojiingiza kwenye harakati mbali mbali kama michezo isiyowahusu, leo hii tusingekuwa na matokeo mazuri kama haya,’’alieleza.

Mzazi Ali Yussuf Ali, alisema matokeo hayo ya muhula wa kwanza, yanaashiria kuwa, waalimu wanafundisha kwa bidii na ukomavu wa hali ya juu.

Nae mzazi Hidaya Mjaka Ali, alisema kama waalimu wanaendelea kufanya juhudi hizo, sasa ni jukumu lao wazazi kufuatilia nyenendo za watoto wao.

‘’Waalimu wanaendelea kuonesha juhudi zao, sasa na sisi wazazi na walezi, tuwasaidie waalimu, maana mtoto analelewa na nguzo zaidi ya moja,’’alishauri.

Kwa upande wake mazazi Mgeni Seif Mohamed, alisema pamoja na mazuri yaliojitokeza kwenye muhula wa kwanza, lakini lazima mkazo uwekwe kwa masomo ambayo hajakupasisha vizuri.

‘’Masomo ya fizikia na hesbati, lazima waalimu kwa kushirikiana na sisi wazazi, tuangalie namna bora ya kubuni mbinu nyingine, ili sasa mwakani ufaulu uongezeke,’’alishauri.

Hata hivyo mzazi Rashid Mjaka Mkuu, amependekeza wanafunzi kuongezewa kazi za kufanya, hasa kwa masomo ya yanyoambatana na hesabu, kwani ndio msingi wa masomo kadhaa.

Mwalimu mkuu wa skuli hiyo Mwache Juma Abdalla, alisema wazazi, wataendelea kuwa mwalimu nambari mbili, katika kufikia ndoto za mwanafunzi.




Alieleza kuwa, mwalimu pekee hata kama anaujuzi na uwelewa kiasi gani, kama mzazi hakushughulika kwa nafasi yake, ufaulu wa mwanafunzi utakuwa mashakani.

‘’Ingawa niwapongeze baadhi ya wazazi na walezi, wamekuwa wakifuatilia kwa karibu maendeleo ya watoto wao, na njia hii sisi inatupa ari zaidi ya kufundisha,’’alieleza.

Akizungumzia kwa wanafunzi walioko kambini, alishauri kuwepo kwa mavazi maalum, ili kupunguza mrundikano wa nguo, kwenye makaazi yao.

Mwenyekiti wa bodi ya skuli hiyo Dk. Said Mohamed Ali, aliwakumbusha wazazi na walezi, juu ya ulipaji wa ada kwa wakati, ili kuto nafasi ya mtiririko mzuri wa usomeshaji.

‘’Kila mzazi wakati anamleta mtoto wake skulini hapa, alijua kuna mchango wa masomo kila mwezi, sasa inakuaje wanafunzi wafikie miezi 20 au 30 wanadaiwa, hili halivumiliki,’’alifafanua.

Msimamizi wa kambi ya wanafunzi skuli hapo, Mwalimu Haji Othman Haji, alisema changamoto zaidi ni kwa wanafunzi wa kiume, ambao bado hakujakuwa na usimamizi madhubuti.

Akiwasilisha muhutasari wa matokeo hayo, mwalimu wa skuli hiyo Fadhila Rashid Khamis, alisema kwa upande wadarasa la tisa, kulikuwa na wanafunzi 35, waliofeli ni wanne pekee.

Alieleza kuwa, kwa upande wa darasa la 12, waliofanya mitihani ni 58 wakiwa wanawake na wanaume idadi sawa, ingawa waliofeli ni 43 sawa na asilimi 75.4.



Hata hivyo mwalimu huyo, alisema kwa upande wa somo lililopasiha wanafunzi wengi zaidi ni kemia, bayolijia, Kiswahili na fizikia kwa darasa la tisa.

Kwa upande wa darasa la 12, somo la uraia liliongoza, likifuatiwa na lugha ya kiiengereza, jiografia, historia, pamoja na kemia.

Skuli ya sekondari ya Connecting Continent ambayo ina mdarasa kuanzia la tisa hadi 12, ilianzishwa mwaka 2006 kwa sasa inawafaunzi 320, wakiwemo wanawake ni 175 na wanaume ni 145.

                                Mwisho        

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch