Skip to main content

WANAWAKE WANAOZALISHA BIDHAA ZA CHAZA LULU MAKOMBENI WALA HASARA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANAUSHIRIKA wa ‘tujikombowe’ wa shehia ya Mkombeni wilaya ya Mkoani Pemba, unaojisghulisha na ufugaji wa chaza lulu, wamepata hasara ya zaidi ya shilingi 600,000 baada ya bidhaa zitokanazo na rasilimali hiyo, kukosa wateja.

Bidhaa hizo aina herini pea 25, ambazo moja ni shilingi 25,000 wamelazimika kuzibakisha ofisini kwao, baada ya kukosa wateja kwa muda mrefu sasa.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, walisema awali walikuwa na changamoto ya ukosefu wa mashine ya kusarifia bidhaa hizo, ingawa baada ya kuipata sasa changamoto ni soko la bidhaa hizo.

Walisema, kwa mara ya kwanza walizalisha herini hizo na kuziuza kwa thamani ya shilingi 300,000 ingawa kwa msimu mwengine walikosa wateja wa bidhaa hizo.

Mwenyekiti wa ushirika huo Faida Faki Kombo, alisema kwa sasa hawajui herini hizo pea 25 wazifanye nini bali wanachoshuhudia ni kuendelea kuchakaa na kupoteza thamani.

Alieleza kuwa, soko la wateja wao kwa sasa limepotea na kusababisha kupata hasara, jambo ambalo wanafikiria namna ya kujitangaaza.

‘’Ni kweli bidhaa za magamba ya chaza lulu ambazo ni herini pea 25, zimeganda ndani hazina wateja kwa muda mrefu, jambo ambalo limetuvunja moyo,’’alieleza.




Kwa upande wake Katibu wa ushirika huo Asha Nassor Makame, alisema baada ya kuona kwenye mradi wa uzalishaji chaza lulu wamekosa wateja na mashine yao kuharibika, sasa wameelekeza nguvu kwenye kuusarifu mwani.

‘’Kwa sasa tumeamua kutengeneza sabuni, siki na mafuta ya bidhaa za mwani, na si haba matunda yanapatikana, na tunaendesha maisha yetu,’’alieleza.



Hata hivyo alisema changamoto wanayokumbana nayo ni ukosefu wa taalamu ya kutosha juu ya utengenezaji wa bidhaa hizo.

Kuhusu wazo la kuzalisha mwani, alisema ndio mpango wao wa baadae na tayari wameshapeleka maombi serikali kwa ajili ya kuunganishwa ili kupatiwa vifaa.

Alifafanua kuwa, wameona kwa sasa wapumzike kidogo kwenye kilimo cha chaza lulu, na nguvu zao wazilelekeze kwenye kilimo cha mwani.

‘’Tukipata uwelewa wa kilimo cha mwani na tukivuna tunauwezo wa kusarifu wenyewe, matunda yanaweza kuonekana kwa muda mfupi kwenye ushirika wetu,’’alieleza.

Mshika fedha wa ushirika huo wa ‘tujikombowe’ Miza Makame Silima, alisema mradi wa kutengeneza bidhaa za mwani, umekuwa ukiwapatia manufaa.

‘’Kwa mfano mara kwanza tujipatia shilingi 300,000 lakini tulipozalisha tena tukapata shilingi 150,000 ingawa kwa mwaka jana tulijipatia shilingi 500,000,’’alifafanua.

Hivyo, alisema kama watawezeshwa kimafunzo kupanda mwani wenyewe, huku wakiwa na utaalamu wa kuusarifu kwa kutengeneza bidhaa kama mafuta, sabuni na siki wanaweza kupinga hatua.


Kuhusu komba mikopo serikali, walisema kwanza wanajipanga kuhakikisha wanapata mafunzo ya upandaji mwani, ili watakapoomba iwe kazi rahisi ya uzalishaji.

Akizungumzia soko la bidhaa hiyo, alisema sio bay asana ingawa hutegemeana na kipindi maalum, kutokana na mzungumko wa fedha kuwa mdogo.

‘’Sabuni za mwani, mafuta, mafusho pamoja na siki, tunaowateha hadi Unguja, na tukishazalisha hazikai muda mrefu kupata wateja,’’alieleza.




Wateja wa bidhaa za mwani shehiani humo, walisema wamekuwa wakitumia mafuta yatokanayo na bidhaa ya mwani, ambayo ni mazuri kwa tiba ya ngozi.

Khamis Issa Makame anasema, mafuta hayo yanasaidia pia kusafisha ngozi ikiwa mtu anapele sugu au mba wa muda mrefu.

Aisha Othman Haji, alisema amekuwa akitumia siki kwa ajili ya kuongeza uchachu kwenye chakula, jambo ambalo kwa sasa hawezi kuikosa tenda siki hiyo ya mwani.  

Sheha wa shehia ya Makombeni Mwashum Makame Haji, alikiri kuwa ushirika huo, unakabiliwa na changamoto ya soko kwa bidhaa zitokanazo na magamba ya chaza lulu.

Akizungumzia kupatiwa mafunzo ili kuendeleza kilimo cha mwani, alisema amekuwa akizungumza na uongozi wa wilaya na tasisi husika, ili kupatiwa pamoja na vifaa.

‘’Kama kuna wafadhili ambao wanakiu ya kutaka wanawake kuendelea, waje shehiani mwangu, kwani wapo wenye hamu ya kufikia ndoto zao,’’alieleza.

Ushirika wa ‘tujikombowe’ wa shehia ya Makombeni wilaya ya Mkoani Pemba, ambao ulianzishwa mwaka 2007, kwa upandaji wa chaza lulu na utengenezaji wa bidhaa kama herini zitokanazo na magamba yake, una wanachama 25.

                           Mwisho   

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch