Skip to main content

WADAU: ‘WAHANGA WA UDHALILISHAJI WALIPWE FIDIA ZAO

 



NA ZUHURA JUMA, PEMBA

“NILIAMBIWA mahkamani kua, mtoto wangu atalipwa shilingi milioni 1 ya fidia, tangu mwaka jana, mshitakiwa alipotiwa hatiani, lakini sasa ni miaka miwili hajapewa, mpaka mshitakiwa alipoondolewa hukumu kwa madai ya ugonjwa wa akili,’’anasema mzazi mmoja.

Mama huyo mkaazi wa Wingwi Wilaya ya Micheweni ambae mtoto wake wa miaka mitatu (3) alifanyiwa kitendo cha ubakaji na kijana wa miaka zaidi ya 28.

Anaeleza kuwa, alitegemea fedha hizo zitamsaidia kumshughulikia mtoto wake ambae aliathirika kisaikologia na kimwili, ingawa hajaulizwa chochote tangu kesi hiyo ilipopata hukumu mwaka jana.

“Kinachoniumiza zaidi ni kuona yule mshitakiwa alitakiwa kutumikia chuo cha mafunzo miaka 30, lakini haijatimia mwaka, ameshatolewa eti kwa madai kuwa ni mgonjwa wa akili, na amekwenda Unguja Mental”, anaeleza.

Anasema kijana huyo hajawahi kumuona wala kusikia kwamba ana ugonjwa wa akili, isipokuwa wanafanya hivyo ili asifungwe wala alimlipe fidia.

Mama huyo sio peke yake ambae hajapata fidia bali, kuna baba ambae mtoto wake wa miaka 11 alibakwa na hukumu kutolewa mwaka jana, ingawa hajaona fidia iliyotakiwa kulipwa.

Baba huyo mkaazi wa Madungu Wilaya ya Chake Chake anasema, mshitakiwa huyo alitakiwa atumikie chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka saba, na alipe fidia ya shilingi milioni 2, ingawa bado hajalipwa na ameshakata tamaa.

“Sina tamaa ya kulipwa, lakini familia ya kijana huyu huko mtaani wanasema kuwa, hawalipi chochote kwa sababu wanajua kuwa, kitakapomalizika kifungo, ataongezwa tu miezi mitatu ya adhabu kwa kutolipa fidia”, anasema.

Anaiomba Serikali uwepo mfuko maalumu wa fidia ambao utawasaidia waathiriwa wa vitendo vya udhalilishaji, katika kutatua changamoto zinazowakuba watoto wao.

‘’Sio kwamba tunataka watoto wetu wabakwe ili tulipwe fidia, lakini wakati limeshatokea, ni vyema na hawa watoto waliodhalilishwa wakafikiriwa, kwa sababu ningezipata ningemuendeleza kielemu katika eneo jengine’’, anasema.

Wakili wa Serikali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (PP) Ali Amour Makame anasema, katika sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, imeweka adhabu ya kifungo pamoja na fidia, ingawa hakuna fidia iliyowahi kutolewa.

Anasema, hiyo ni kwa sababu washitakiwa wengi wanaotiwa hatiani hawana uwezo wala vyanzo vya kulipia fidia na hatimae waathirika, kukosa haki yao hiyo.

‘’Waathiriwa wengi baada ya kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji wanapata matatizo ya kiafya au kiakili, hivyo ni muhimu wapatiwe hii fidia yao ili zipate kuwasaidia’’, anafafanua.

Wakili huyo anaeleza, kuna haja ya waandishi wa habari kuzisemea sheria zenye kasoro, ili Serikali kuzijua na kuzirekebisha sambamba na jamii kuzifahamu.

Sheria ya Kanuni ya Adhabu Zanzibar nambari 6 ya mwaka 2018, ni Sheria ambayo yamo makosa mengi ya udhalilishaji.

Kifungu cha 3 cha Sheria hiyo kimeeleza makosa ya udhalilishaji kuwa, ni yale yote yalipo katika sehemu ya 14 kwenye vifungu vya 146, 147 na 148 vya Sheria hiyo.

“Kwa kiasi kikubwa Sheria hiyo imekidhi matakwa ya Haki Jinai na Jamii kwa ujumla, ingawa zipo kasoro ambazo zinahitaji kufanyiwa mabaoresho”, anafafanua.

WANANCHI WANASEMAJE

Bakar Suleiman Juma mkaazi wa shehia ya Kambini anasema, kitu kinachosababisha waathiriwa wa vitendo vya udhalilishaji wasipate fidia, ni kukosa uwelewa wa  sheria, hivyo wanashindwa kujua waipate wapi kudai haki yao.

“Wao wanajua hukumu ni ile moja tu ya adhabu ya kifungo na hajui haki yake nyengine, hivyo fursa hiyo wanaitumia wengine kwa maslahi yao, jambo ambalo sio sahihi”, anaeleza.

Asha Ali Hamad mkaazi wa shehia ya Mchanga mdogo anasema, ni vyema kwa Serikali kusimamia hilo, ili kuhakikisha fidia inatolewa na inawafikia walengwa.

“Hili suala la fidia sio la kufumbiwa macho, kwa sababu mtoto akishafanyiwa vitendo vya ukatili anakuwa ameshaathirika kiakili, kisaikologia na kimwili, hivyo atakapopewa haki yake ya fidia itamsaidia”, anafahamisha.

Mkaazi wa shehia ya Shengejuu Fatma Saleh Yussuf anaishauri Serikali kupitia mahakama, itunze kumbukumbu vizuri za mshitakiwa, ili atakapomaliza muda wa kutumikia adhabu ikiwa hajalipa fidia alazimishwe kuilipa.

WARATIBU WA WANAWAKE NA WATOTO WA SHEHIA

Awena Salim Kombo ambae ni Mratibu wa shehia ya Kangagani Wilaya ya Wete anasema kuwa, ni kwamba mahakimu wanapotoa hukumu hawashughulikii tena suala la fidia na ndio maana washtakiwa hawatoi.

“Ingekuwa hili jambo la fidia linashughulikiwa na kufuatiliwa basi naamini washtakiwa na familia zao wangezitoa, lakini kwa vile linakaliwa kimnya ndo maana hawalipi”, alisema .

Anashauri kuwa, mshitakiwa atakapomaliza kifungo chake na ikawa hajalipa fidia, asitolewa mpaka ailipe hata kama atakaa chuo cha mafunzo kwa miaka mengine kumi.

Mratibu wa shehia ya Mzambarao Takao Fatma Hamad Nassor anaeleza kuwa, sababu ya washtakiwa kutolipa fidia ni kwamba familia zao ni masikini na wakati mwengine wao ndio watafutaji.

“Wanasema kuwa hali zao ni za umasikini lakini wengine hawatoi hata kama wanazo, kwa sababu hakuna usimamizi wowote, hii inawaumiza sana waathiriwa wa vitendo vya udhalilishaji”, anasema.

Mratibu huyo anashauri kwamba, ikiwa mshitakiwa atakuwa na kitu chochote cha thamani kitaifishwe, ili ipatikane fedha alipwe fidia muathiriwa.

Mchanga Said Hamad ambae ni Mratibu wa shehia ya Kiungoni Wilaya ya Wete anasema, ili waathiriwa wanufaike na fidia kuna haja ya kuwa itolewe mwanzo kabla ya mshitakiwa kutumikia adhabu.

“Itakapofanywa hivyo atapungua huzuni kwa sababu kwa vile ameshafanyiwa ukatili itakuwa muda wote anafikiria mambo mengi, lakini fidia itamsaidia kutatua baadhi ya changamoto zilizomkumba”, anaeleza.

Sheha wa shehia ya Piki Assaa Khamis Mussa anaishauri Mahakama kusimamia fidia mara tu inapomalizika kesi na kuhakikisha inawafikia walengwa.

“Ni kweli fidia hazitolewi na wakati mwengine eti unatakiwa ufungue kesi ya madai, jambo ambalo ni vigumu kwa sababu umeshapoteza nauli nyingi kufuatilia kesi ya mwanzo na ndio maana familia za wahanga zinabaki njia panda”, anaeleza.

ASASI ZA KIRAIA

Hafidh Abdi Said Mkurugenzi wa ‘KUKHAWA Pemba anasema, kwa vile ipo Wizara ya Ustawi wa Jamii ni vyema iweke utaratibu wa kuwasaidia waathiriwa wa vitendo vya udhalilishaji.

“Hii ni muhimu kwa waathiriwa wa vitendo vya udhalilishaji, kwa sababu ameshaathirika kisaikologia na maisha yake yanaharibika, hivyo Wizara ijipange kuwasaidia wahanga hawa”, anaeleza.

Mratibu wa TAMWA Pemba Fat-hiya Mussa Said anasema, hakuna Sheria malumu zinazosimamia upatikanaji wa fidia kwa waathiriwa na vitendo vya udhalilishaji, bali kuna Sheria tu inayomtaka mshitakiwa alipe fidia au akishindwa atumikie kifungo.

“Na jamii imejijenga kuwa, mshitakiwa akishapelekwa chuo cha mafunzo hana sehemu ya kuipata fidia ya kumlipa muathiriwa hasa kwa vile yeye ndie alitenda lile kosa”, anaelezea.

Anasema, lakini kuna haja ya kuangalia Sheria upya na kuzifanyia marekebisho, ili kuhakikisha kwamba muathirika anafaidika na fidia hiyo na inamsaidia katika kurudisha hali yake ya kisaikologia ambayo imeathirika.

“Mimi nadhani kuwe na utaratibu wa kutolewe fidia ya lazima, kutoka kwa mshitakiwa, kwa sababu hata wakaidai hawaipati na wakati mwengine wanatakiwa wafungue kesi ya madai, jambo ambalo ni changamoto,” anafafanua.

Anashauri kuwepo utaratibu maalum wa kuwalipa wahanga fidia au kuwepo kwa darasa maalumu la saikolojia kwa watoto hao, ambalo litagharimiwa na serikali na wafadhili.

Anasema kuwa kupitia wanamtandao wao wa kupambana na masuala ya udhalilishaji katika Wilaya ya Wete na Mkoani mwaka jana walifuatilia kesi 90, ambazo 16 zipo mahakamani

Kesi nyingine 43 zinaendelea na upelezi, kesi saba (7) zimepata hukumu na 17 ziliondolewa mahakamani kutokana na kukosa ushahidi.

MAHAKAMA

Naibu Mrajis Mahakama Kuu Pemba Faraji Shomari Juma anafafanua, kuna kifungu cha sheria kimeeleza kwamba washtakiwa walipe fidia, ambapo humpa mtu adhabu na kumtaka alipe fidia hiyo sambamba na kumpa adhabu.

“Kwa hivyo inakuwa sio lazima alipe kwa sababu imeweka kwamba akishindwa kulipa fidia, anatakiwa atumikie adhabu ya kifungo kwa muda atakaopangiwa, hivyo akishatumikia hicho kifungo hakuna sababu ya kulipa tena fidia”, anaeleza.

Akitoa mfano alisema, pengine amefungwa miaka 30 na akishindwa kulipa fidia atumikie mwaka mmoja, hivyo anapomaliza adhabu yake ya kifungo anaulizwa kuhusu fidia, ikiwa hana ndo anamalizia adhabu.

“Ile kusema tu utamlipa fidia milioni 1ukishasimama hapo tu, inakuwa katika Sheria kuna shida kidogo, kwa sababu ikiwa hakumlipa je utafanya nini”, anahoji.

Na ndio maana anawashauri mahakimu wao, wanapotoa fidia waseme kuwa, akishindwa kulipa fidia itatokea hivi…, jambo ambalo linasaidia kwani anapoambiwa hivyo, wazee wake watazitafuta.

Anaeleza kuwa, kuhusu ufuatilia wa fidia ni kuhakikisha mshitakiwa analipa, kwani katika hati ya kifungo wanaeleza kuwa… mshitakiwa atatumikia miaka kadhaa na fidia kiasi fulani.

Kwa hiyo kule chuo cha mafunzo wanamlazimisha mshitakiwa alipe na baadae zinafikishwa mahakamani kwa ajili ya kukabidhiwa muathiriwa.

Anataja kuwa, mwaka 2022 mahakama maalumu za kupambana na udhalilishaji Pemba, zilifikishwa kesi 94, ambapo kesi 48 za mkoa wa kusini na kutolewa hukumu kesi 40, huku kesi za mkoa wa kaskazini Pemba zikiwa ni 46 na kutolewa hukumu 33.

Kutokana na mapungufu yaliyomo kwenye sheria za kupamba na udhalilishaji, Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania TAMWA -Zanzibar wameona kuna haja ya kuorodhesha Sheria hizo na kuonyesha kasoro za msingi kutokana na mazingira yaliypo sasa.

Lengo la kuainisha mapunfu katika Sheria hizo ni kuisaidia Serikali na jamii kwa ujumla katika upatikanaji wa haki.

                                        MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch