Skip to main content

SKULI MPYA YA GHOROFA MWAMBE, KUPUNGUZA UFINYU WA NAFASI KWA WANAFUNZI?

 

 


 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

ILIKUA kama ndoto, kwa siku ya kwanza kati ya zile 360 zinazounda mwaka, kwa waalimu, wanafunzi, wazazi, walezi wa Mwambe, kunawa uso mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi.

Sio tu kunawa uso, kwa maji kama ilivyozeeleka, wao walinawa kwa kumalizika skuli ya msingi ya ghorofa mbili eneo hilo la Mwambe.

Hapa wazazi, walezi, wanafunzi na waalimu, maji kwenye upindo wa kucha ya mtoto mchanga, yalitosha kuwakogesha mwili mzima.

Furaha yao, sio tu kuamka wakiwa wazima siku hiyo ya Januari 1, mwaka 2023, lakini ni pale waliposhuhudia jengo la kwanza la ghorofa katika eneo la Mwambe, na bahati nzuri sio la mtu binafsi, bali likiwa la serikali.

WANANCHI MWAMBE

Haji Omar Kheir, anasema aliposikia ahadi ya rais wa sasa wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, juu ya ujenzi wa skuli ya ghorofa, hakuamini akilini mwake.

‘’Si unajua baadhi ya wanasiasa wakitaka jambo lao, watakuahidi jambo hata ambalo yeye hajawahi kuliona wala kuliskia,’’anasema.

Kisha kwa Januari mwaka huu, akasema sasa anakubali kuwa Dk. Mwinyi, anachokiahidi anakitekeleza, akatolea mfano skuli hiyo ya ghorofa mbili Mwambe.

Asha Muhsini Mohamed, anasema sasa baada ya kusimama kwa jengo hilo, ni wajibu wao kuwahimiza watoto kusoma, badala ya kukimbilia baharini kuchokoa pweza na kaa.

Is-mail Hamdu Mjaka, anasema jengo hilo, alitarajia lijengwa mjini Chake chake au mjini Unguja, lakini kwa uungwana wa Rais wa sasa Dk. Hussein Ali Mwinyi, amewapelekea wao.

‘’Kwa hakika ile Mwambe wa miaka 50 iliyopita sasa imeshatoweka, na hii ya sasa ni kama ilivyo mjini Chake chake au Unguja, kwa kuwepo kwa jengo la kisasa,’’anasema.

WANAFUNZI

Kazija Omar Haji na mwenzake Asha Haji Ussi wanasema, sasa ni kazi ya kamati, washirikiane na wazazi ili kutimiza ndoto zao za kupata elimu.

Makame Mcha Kheir na Abubakar Mohamed Machano, wao wanasema watasoma kwa ushindani na skuli nyingine, hasa baada ya kupatiwa jengo la kisasa.

Wanafunzi wanakumbuka, wakati ule walipokuwa wakiingia mikondo mitatu, wakisema hawakuwa na mtiririko mzuri wa kujifunza.

RAIS WA ZANZIBAR

Januari hiyo 1, mwaka huu Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, alikwenda mwenyewe, kuifungua skuli hiyo mpya ya ghorofa mbili.

Kwenye hutuba yake fupi na iliyojaa kila kitu, alianza na kuipa agizo wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, ishirikiane kwa karibu na Idara ya Utumishi, ili kuajiri waalimu nchini.

Akasema, changamoto ya uhaba wa waalimu anaijua kuwa ipo, lakini ni vyema kwa wizara husika, kuongeza kasi ya kuajiri waalimu, na kipaumbele, iwe ni wale ambao walishajitolea siku za nyingi.

Wakati serikali ikijenga skuli mpya zikiwemo za ghorofa, na kuzifanyia ukarabati zile za zamani, lazima na suala la kuajiri waalimu, nalo liangaliwe kwa haraka, alisisitiza Dk. Mwinyi.

‘’Kama walionesha moyo wa kujitolea kwa taifa lao, kwa kuwatumikia wananchi wenzao, sasa wakati ukifika nao kuajiriwa, wapewe kipaumbele kwa wenye sifa,’’akasisitiza.

Lakini, kubwa na la kufurahisha kwa eneo hilo la Mwambe, ni pale Dk. Mwinyi, alipoahidi kujenga skuli nyingine ya ghorofa, ili kukabiliana na uwingi wa wanafunzi uliopo.

Akaeleza kuwa, ameshtushwa na idadi ya wanafunzi wanaoendelea kuandikishwa wa darasa la kwanza kwa mwaka huu, ambapo walifikia 970 kwa wakati huo.



‘’Kwa hili, lazima niwaahidi wananchi wa Mwambe na vijiji jirani kuwa, serikali itajengwa tena skuli nyingine ya ghorofa, ili kuondoa hata mikondo miwili,’’anaeleza.

Tena hapa akagongomelea msumari kuwa, bado serikali ya awamu ya nane, itaendelea kuona kuwa, elimu ndio kipaumbele cha kwanza, na azma ya kujenga skuli za kisasa na vifaa vya kufundishia ipo.

‘’Ndio maana zipo skuli 24 za zamani kwa Unguja na Pemba, zinaendelea kufanyiwa matengenezo makubwa, ambapo kwa wilaya ya Mkoani, ni skuli za Mauwani Kiwani, Chambani na Maendeleao Ngwachani.

Kumbe ndani kipindi cha mwaka mmoja, serikali imeshajenga madarasa 143, kati ya hao 95 yalianzishwa kwa nguvu za wananchi na 48 ndio mapya, samba mba na ujenzi wa vyoo 318 kwa skuli za maandalizi, msingi na sekondari mkoani humo.

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI

Mwenye dhamana kuu ya elimu ya Zanzibar Leila Mohamed Mussa ambae ni Waziri wa wizara hiyo, anasema, kwanza amevutiwa mno na kasi ya Dk. Mwinyi ndani ya wizara hiyo, akisema imesaidiai kutatua changamoto tofauti, zikiwemo za maakazi kwa wanafunzi.

Kumbe, sio Mwambe pekee, lakini kila wilaya ya Unguja na Pemba, ameshaacha alama, kwa kuhakikisha kunajengwa skuli za kisasa na za ghorofa, kuingiza na samani zake kamili.

Waziri huyo wa Elimu akaenda mbali zaidi, pale alimpongeza Dk. Hussein kwa kuwapatia fedha shilingi bilioni 68, kwa ujenzi wa skuli na kutia samani.

Hata ununuzi wa vitabu, sambamba na kukamilisha ujenzi skuli 25 za maandalizi Unguja na Pemba, ikiwa ndio msingi wa elimu ya sekondari.

Kwake anaona, kukamilika kwa skuli hiyo ya ghorofa mbili Mwambe, kama vile amemalizka changamoto kubwa hasa eneo hilo.

Katibu Mkuu wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Khamis Abdalla Said, akiutaja ujenzi wa skuli ya ghorofa ya Mwambe, akasema baada ya kumalizika, sasa umejumuisha madarasa 46, yakiwemo 25 ya zamani.



Lakini pia, akazigeukia fedha za sherehe ya Mapinduzi ya Zanzibar za miaka 59, shilingi milioni 450, zitawasaidia kwa ununuzi wa samani na vitabu katika skuli mbali mbali za Unguja na Pemba.

 ‘’Skuli hii yenye ghorofa mbili na moja ya chini (ground) ni ya kwanza kwa Zanzibar, ambayo itapunguza changamoto ya makaazi kwa wanafunzi wa Mwambe,’’alieleza.



Wizara, tayari imeshaingiza viti, meza mpya na za kisasa ndani ya skuli hiyo, na sasa iko tayari kwa ajili ya kuhamiwa.

Afisa Mdhamini wizara ya elimu na mafunzo ya Amali Pemba Mohamed Nassor Salim, anasema matayarisho ya kuongoeza idadi ya waalimu skulini hapo, yameshakaa vyema.

 

VIONGOZI WENGINE

Mattar Zahor Massoud ndie mwenye mkoa wa kusini Pemba, baada ya kulishuhudia ghorofa likiwa limesimama wima, akawakumbusha wananchi wa Mwambe, kuilinda miundo mbinu ya skuli hiyo.

‘’Hii ni hazina ya urithi wa elim na shilingi bilioni zaidi 3.5 zimeshatumika hadi kukamilika, sasa lazima na sisi wananchi tuthamini jambo hili,’’anasema.

Kumbe ndani ya mkoa huo, vipo vyumba vya madarasa 1,116 ikijumuisha hivyo 42 vya skuli ya ghorofa ya Mwambe. 

Mwakilishi wa Jimbo la Kiwani ilipo skuli hiyo ya Mwambe, Mussa Foum Mussa, akaigeukia serikali kuhakikisha kuwa, inaongeza idadi ya waalimu, ili kwenda sambamba na idadi ya wanafunzi.

‘’Hapa pana waalimu 49 tu, kwa wanafunzi 4,234 sasa lazima tuone hiyo changamoto, baada ya kupata makaazi sasa ni ajira kwa waalimu,’’alikumbusha.

 Hata Mwalimu mkuu wa skuli hiyo, Ali Mohamed Omar, anasema ujenzi wa skuli hiyo, umetoa mwanga mpya wa kupata elimu.

Anaona kuwa, sasa kilichobakia ni jukumu la wazazi na walezi, kuwahimiza wanafunzi wao ili, uwepo wa jengo hilo la ghorofa mbili, thamani yake iaendane na kasi ya kupata elimu.

ILIKOTOKA SKULI YA MWAMBE NA SASA

Skuli ya msingi Mwambe, iliasisi mwaka 1973 ambapo kwa wakati huo, ikiwa na wanafunzi wasiozidi 100, na ilianza ikiwa na madarasa ya kusomea 25.

Kisha skuli hiyo katika miaka ya 2000, baada ya idadi ya wanafunzi kuongezeka, mtindo wa kuingia mikondo mitatu skulini hapo, ulianza.

Hadi mwaka 2022, ndipo ilipoanza ujenzi wa skuli ya kisasa ya ghorofa moja ya chini (ground) na ghorofa mbili za juu.

Sasa zikijumuisha vyumba 21, na ukijumlisha vyumba vya zamani, skuli hiyo itakuwa na vyumba 46, vikibeba wastani wa wanafunzi 45 kwa chumba kimoka kutoka 86 kwa zamani.

Skuli hiyo kwa sasa, ina jumla ya vyoo 30, na kila ghorofa kuwepo kwa ofisi tatu za waalimu, achia mbali ile ya mwalimu mkuu.

Lakini wapo wanafunzi 4,234 ikijumuisha na ile skuli kwa madarasa ya zamani, huku ile mpya pekee, ikiwa na uwezo wa kubeba wanafunzi 1,890 kwa mikondo miwili.

Ambapo hapo wanafunzi 945, wataingia asubuhi na wengine mchana, wakitumia vyumba 21 kwa wastani wa wanafunzi 45 kila darasala moja.

Kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo, skuli ya msingi Mwambe, wapo wanafunzi 820 walifanya mitihani ya taifa, lakini ni wanafunzi sita tu wa michepuo na wawili wa kipawa maalum.

Na ile ya sekondari, nao kwa kipindi hicho hadi mwaka 2021, hawajapata mwanafunzi aliyepata ufaulu wa daraja la kwanza ‘division one’.    

Skuli hiyo ya ghorofa mbili ya msingi ya Mwambe wilaya ya Mkoani Pemba, ujenzi wake umechukua mwaka mmoja, umejengwa na kampuni na Mwamba kwa shilingi bilioni 3.571 fedha za UVIKO 19, kupitia Shirika la Fedha Duniani ‘IFM’.

                     Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch