Skip to main content

MWENGE WA UHURU WATUA PEMBA, WAANZA WILAYA YA WETE UFUNGUZI WA MIRADI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MWENGE wa uhuru umewasili kisiwani Pemba, ukitokea Mkoa wa kaskazini Unguja, tayari kwa ajili ya kukimbizwa katika wilaya nne za Pemba, samba mba na ufunguzi wa miradi kadhaa, ikiwemo ya maendeleo kisiwani humo.

Mwenge huo umepokelewa jana, katika uwanja wa ndege wa Karume Pemba, ambapo wananchi wa mikoa miwili ya Pemba, wakiongozwa na Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba, Salama Mbarouk Khatib, wamejumuika.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa kaskazini Unguja Ayoub Mohamed Mahamoud, alisema mwenge huo ukiwa mkoa mwake, ulizindua miradi minane ya maendeleo na program nne, yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 14.4.

Alisema wakimbiza mwenge, walitoa ujumbe kwa wananchi, ukiwemo suala la uhifadhi na utunzaji wa mazingira, lishe na kupinga rushwa na kisha kuchunguza afya kwa wananchi.

Mkuu huyo wa Mkoa, alisema katika kipindi hichi, walipanda miti 120,000, ingawa katika shamra shamra za mwenge wamepanda miti 2,500.

‘’Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba, napenda nikukabidhi mwenge wa uhuru ukiwa unang’ara, na wakimbiza mwenge wakiwa na afya njema,’’alieleza.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa Abdalla Shaib Kaimu, alisema wameridhishwa na usimamizi wa miradi ya maendeleo, katika mkoa wa kaskazini Unguja.

Alieleza kuwa, umoja uliopo, mshikamano na upendo ndani ya mkoa wa kaskazini, umesaidia kuwepo kwa utekelezaji mzuri wa ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025, na kuwepo kwa miradi mikubwa ya maendeleo.



Aidha aliwataka wakuu wa wilaya, kuwepo kwa nyaraka mahasusi ya miradi, vipimo vya kupimia ubora wa baadhi ya miradi pamoja uwepo wa wataalamu husika kwenye miradi itakayopitiwa na mwenge.

Mara baada ya kupokea mwenge huo, mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, alisema mwenge utayapitia miradi 10 na program 10, yenye thamani ya shilingi bilioni 18.428.

Alieleza kuwa, miradi hiyo ipo katika wilaya ya Micheweni na Wete, ambapo imo ile ya maendeleo, kama ya kiwanda cha kusarifu mwani Chamanagwe, upandaji miti eneo la Kangagani.

 Akisoma risala kabla ya zoezi la uzinduzi wa upandaji miti, katika kambi za chuo cha Mafunzo Kangagani eneo la Mashindeni, mpiganaji Abrahman Mwinyi Chumu, alisema ekari 792.05 zimetengwa kwa shughuli mbali mbali, ikiwemo upandaji miti.

Alisema, wameamua kupanda miti hapo, ili kulirejeshea hadhi yake eneo hilo, kufuatia uharibifu uliofanyika kwa muda mrefu, hali iliyopelekea, kuwepo kwa jangwa.



Alieleza katika eneo hilo, wanatarajia kupanda miti aina ya Mivinje 1,500 na kufanya idadai ya miti yote ambayo wataipanda hapo baadae kufikia 9,000.

‘’Katika zoezi hilo, shilingi milioni 14.175 zilikadiriwa kutumika, lakini zimeokolewa, kwa kule wapiganaji kujitolea na kutumika shilingi 13.5 kwa ununuzi wa miche,’’alieleza.

  Mkuu wa wilaya ya Wete Dk. Hamad Omar Bakar, alisema mikono ya wananchi, isitumike kupelekea athari kwa jamii, kwa kule kukata miti ovyo.

Alieleza kuwa, ujio wa mwenge huo katika eneo hilo, limesababisha upandaji wa miti 9000, ya aina mbali mbali ikiwemo mivinje na mikeshia.

‘’Hata baada ya kuondoka mwenge, zoezi la upandaji miti katika kambi za Chuo cha mafunzo, litakuwa endelevu, kwani tayari pameshaharibika,’’alieleza.

Mapema mkimbiza mwenge wa uhuru Zinab Hemed Mbetu, akitoa ujumbe wa mwenge, aliwataka wananchi kuendelea kutunza mazingira, hasa eneo la vyanzo vya maji.

Akisoma taarifa ya kitaalamu, Mkurugenzi mkuu Kampuni ya mwani Zanzibar Massoud Mohamed Rashid, wakati mwenge huo wa uhuru ulipofika, kwenye kiwanda cha kusarifia mwani Chamanangwe, alisema ujenzi wa kiwanda hicho umefikia hatua nzuri.



Alisema ujenzi huo ambao unajengwa na Kikosi maalum cha Kuzuia Magendo Zanzibar ‘KMKM’ uko katika awamu ya kwanza, kati ya zile tatu hadi kukamilika kwake.

Alifafanua kuwa, awamu ya kwanza inajumuisha ujenzi wa jengo kuu la kiwanda, ujenzi wa ghala pamoja na uzio maalum kwa ajili ya kulihifadhi eneo hilo.

‘’Awamu pili utajumuisha ujenzi wa maeneo ya bustani, ufungaji wa mitambo husika na awamu ya tatu ni kuanza uzalishaji bidhaa zitokanazo na mwani,’’alifafanua Mkurugenzi huyo.

Aidha alieleza kuwa, hadi sasa tayari ujenzi huo wa awamu ya kwanza umeshafikia asilimia 86, na ukitarajiwa kutumika shilingi bilioni 8.2 ingawa wameshatumia shilingi bilioni 4.024 na utakapomalizika wote, utagharimu shilingi bilioni 13.

‘’Mradi huu wa kiwanda, utakapomalizika utakuwa na uwezo wa kusarifu mwani tani 30,000 kwa mwaka, ambapo umiliki wake kwa asilimia 55 utakuwa serikalini na asilimi 45 utakuwa wa kampuni ya Nutri-san.        

Mwenge wa uhuru leo, utakuwa wilaya ya Micheweni kwa kuzindua miradi mbali mbali, kisha kukabidhiwa kwa uongozi wa wilaya ya Chake chake na Mkoani, ambapo ujumbe wa mwaka huu ‘Tunza mazingira ukoa vyanzo vya maji kwa ustawi wa viumbe na uchumi wa taifa’.

                 Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch