Skip to main content

‘KINJE KUKU’ UTAMADUNI WA MICHEWENI UNAOWAHUSU WATOTO WA KIKE PEKEE

 




NA MARYAM SALUM, PEMBA@@@@

UTAMADUNI wa uvaaji kanga ya shingoni, ama kwa lugha Micheweni ‘kinje kuku’ umepotea kwa kasi.

Kizazi cha sasa cha Micheweni, na hasa watoto wa kike ambao ndio walengwa wa utamaduni, wameanza kuupa kisigo.

Wakionekana, kuachana na vazi hilo, na sasa wakivaa nguo nyingine ambazo wanaona zinawastiri hasa sehemu ya kifuani.

 Hiyo ni kutokana na karne ya sasa na utandawazi jinsi ulivyokua, ndipo watoto wa kike wa Micheweni takribani kwa asilimia kubwa kuacha utamaduni huo.

Vazi hili lilikua linavaliwa sana na watoto, wengi wao wanaishi vijijini, lengo hasa la kinje kuku, ni kuwastiri watoto hao wa kike sehemu ya kifuani, hasa wakianza kutanuka kifua.

Vipo vijiji vyengine vingi katika Mkoa huo  ambavyo watoto wa kike walikua wanavaa vazi hilo kama utamaduni wao, lakini mwandishi wa makala hii aliamua kwenda kwenye kijiji cha Kwale Wilaya ya Micheweni kuzungumza na wazee.

 Wilaya ya Micheweni ni Mkoa unaoongoza kwa masuala mbali mbali ya utamaduni ikiwemo vazi la kanga ya shingo yani kinje kuku, upishi wa maandazi ya kombo alawi na mengine mengi.

Hayo si maneno ya mwandishi wa makala hii bali ni maneno ambayo yalitoka kinywani mwa mama Saada Said Kombo miaka 70 mkaazi wa Kwale shehia ya Majenzi Wilayani humo.

Anasema kuhusu suala la vazi la kanga ya shingo kwa jina jengine kwa baadhi ya vijiji ‘kinje kuku’ ni miongoni mwa utamaduni wao ambao ulikua na kipaumbele kwa jamii ya Kwale na Micheweni kwa ujumla.

VAZI HILI WALIPATA WAPI

Anasema kwamba vazi la kanga ya shingo kwa mtoto wa kike ni urithi kutoka kwa wazazi wao, na kwa wakati huo, ulikuja kutokana na kuwepo kwa uhaba wa nguo za kuvaa hapo zamani.

Aneleza kuwa kutokana na kulikua na uhaba wa mavazi (nguo) hapo zamani ndio maana, ikapelekea wazazi kuwalazimisha watoto wao wa kike kuvaa vazi hilo ili waweze kujistiri.

Maana hapo zamani vazi hilo kwa watoto wa kike katika kijiji chao, lilikua ni vazi la lazima na hakukua na mtoto yeyote aliyekuwa akithubutu kukataa kuvaa vazi hilo.

Kwani kwa wakati huo, kije kuku lilikua ndilo vazi lenye stara  zaidi kuliko vazi jingine lolote, kwa watoto wa kike.

Aisha Makame miaka 60 nae anasema kuwa zamani watoto wa Micheweni kwa ujumla vazi hilo ndio vazi pekee ambalo likivaliwa na rika kwa watoto wa kike walio na umri mdogo.

Anaeleza kuwa Micheweni na vijiji vyake vyengine jirani vya wilaya hiyo, anasema ilikuwa lazima kumuona mtoto wa kike hakuvaa vazi hilo.

‘’Usipovaa vazi hilo kwa wakati huo, ukionekana kama unatembea uchi, hata kama umevaa kanga bei bui na vazi jingine, lakini vazi la heshima lilikuwa kanga ya shingoni,’’anasimulia.

Anaeleza kuwa lengo jengine katika uvaaji wa kanga ya shingo kwa mtoto wa kike jamii ya Micheweni, ni pale tu anapoanza kuota maziwa (machuchu) kujistiri kwa vazi hilo, ili kifuani wengine wasijue kinachoendelea.

“Mtoto wa kike wa jamii yetu ya Micheweni hapo zamani, alikua hana hiari katika kuvaa vazi hili, ilikua ni amri na sio ombi,’’anasimulia.

Anaeleza kuwa kutokana na kuacha asili yao ya kuvaa vazi hilo na mambo mengine mbali mbali ya utamaduni wa jamii zao ndipo kupelekea mambo mbali mbali ya ushawishi ambapo mwisho wa siku hupelekea hata kubakwa.

 “Vazi la kanga ya shingo kwa mtoto wa kike kwa sasa vijana wanadai kwamba si vazi zuri la kuvaa, haliendani na hadhi iliyopo sasa katika ulimwengu wetu tulionao wa kimtandao, sasa mambo yamekua ni tofauti na hapo zamani,’’anasema.

 Sharif Massoud Hamad mkaazi wa Majenzi Micheweni mwenye miaka 60 anaeleza kuwa kutokana na kupotea kwa vazi hilo kumekuwa na utofauti mkubwa kwenye suala la kujistiri.

“Utofauti upo baada ya vazi la kanga ya shingo kupotea, moja ni kutokana na vijana wetu wa kike kuonekana kirahisi kwa baadhi ya maungo yao ikiwemo kifua baada ya kutoa chuchu (maziwa),’’anasema.

“Ingawa kulikua na uhaba wa upatikanaji wa nguo kwa kizazi cha zamani, lakini hata kwa wale waliokuwa wakipata nguo hakuna aliyekua akithubutu kuvaa kanga ya kiuno, kutokana na kuonekana kua ni tabia mbaya,”anaeleza sharif.

Kama hujaolewa mtoto wa kike yoyote wa jamii ya Micheweni hakithubutu kuvaa kanga kiunoni, hadi pale atakapofika kwa mume wake.

Anasema kuwa kwa sasa vazi hilo limepotea kabisa, sasa mtoto akiachishwa tu huanza kuvaa kanga ya kiuno ncha kabisa na hakuna ambae ataweza kumrejesha ama kumrekebisha.

 SABABU YA KUPOTEA KWA UTAMADUNI HUO

 Mayasa Haji Hamad anasema kupotea kwa uvaaji wa kanga ya shingo, kama utamaduni wa wazaliwa wa wilaya ya Micheweni, kwanza ni vijana wenyewe kujenga dhana mbaya juu ya vazi hilo.

Anasema wazazi wa sasa kushindwa kusimamia utamaduni huo kama ilivyo kwa maeneo mengine mbali mbali, jambo ambalo linasabisha athari.

 “Sasa hivi kumeonekana kabisa kupotea kwa amlezi ya pamoja kwa watoto kama ambavyo yalikuwepo zamani, sasa hivi kila mtu na mwanawe hakuna kusaidiana ulezi,” anasema.

NINI KIFANYIKE KUREJESHA UTAMADUNI HUO?

Wazazi na walezi wa Micheweni wanasema kwanza kuwepo na ushirikiano wa pamoja katika suala la malezi, hapo ndipo jamii itaweza kubaki na kuendeleza yale mambo yao mengi ya asili ikiwemo mavazi.

Wanasema wazazi wakubali kuwa, malezi ya pamoja yana umuhimu wake katika kuwalea vijana wao, kwani hapo zamani kulikua na malezi ya ushirikiano na ndio maana hata wao wakafikia pahala pazuri.

 Hamad Mbwana Shaame mkaazi wa Kwale shehia ya Majenzi Wilaya Micheweni miaka 60, anasema wazazi wawaelezea vijana wa sasa umuhimu wa vazi hilo.

‘’Inawezekana vijana wa leo hawajui, faida kama vile stara, sasa tukichukua nafasi ya kuwaelisha huwenda uatamduni huo ukarejea Micheweni,’’anashauri.


 VIJANA WANAZUNGUMZIAJE JUU YA VAZI HILI

Fatma Juma na Time Khamis Mwinyi wa Micheweni wanasema kuwa vazi hilo lilikua linavaliwa hapo zamani, kutokana na uhaba wa nguo.

Kwa sasa wanasema, wamelipa kisogo maana nguo na mavazi mengine yamekuwa mengi, mno na suala la kujistiria inategemea na mtu mwenyewe.

 Wanaeleza lakini kwa sasa vazi hilo limeonekana kupotea kabisa hii ni kutokana mambo yalivyokuwa, kwani sasa hivi hakuna mzazi anaeweza kumwambia kijana wake avae vazi hilo

WIZARA YA HABARI

Waziri wa Habari, Vijana na Utamaduni na Michezo Zanzibar Tabia Maulid Mwita, wakati akiwasilisha bajeti ya fedha ya  mwaka 2022/2023, Baraza la Wawakilishi, anaeleza kuwa wizara inaendelea kuhifadhi, uendelezaji na ukuzaji wa utamaduni.

Upande mwengine anaeleza kuwa, miongoni mwa vipaumbele kwa mwaka ujao wa fedha ni pamoja na utoaji mafunzo kwa watendaji, wajasiriamali wa shughuli za kiutamaduni na wasanii.

Katika kukuza na kuendeleza utamaduni, wizara imefanikiwa kuandaa tamasha la 26 la utamaduni wa mzanzibari kwa Unguja na Pemba.

Eneo jingine ni kuimarisha huduma za utamaduni na sanaa kwa kujenga nyumba ya Sanaa kwa lengo la kutoa mafunzo, kuongeza ajira, kukuza, kuhifadhi na kuendeleza utamaduni, Sanaa na ubunifu kwa jamii ya Zanzibar.

                     MWISHO.

 

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch