Skip to main content

BARABARA KIPAPO-MGELEMA, WAMBAA KUMALIZIKA KWA LAMI MWAKANI

 

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA::

WIZARA ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Pemba, imesema imejipanga kikamilifu, ili kuhakikisha barabara ya Kipapo- Mgemelea hadi Wambaa yenye urefu wa kilomita 9.3 inamalizika kwa kiwango cha lami, katika bajeti kuu ya mwaka 2022/2023.

Kauli hiyo imetolewa na Afisa Mdhamini wa wizara hiyo Pemba Ibrahim Saleh Juma, wakati akizungumza na mwandishi w ahabari hizi, juu ya maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo.

Alisema, wizara imeshajipaga kikamilifu ili kuona ndani ya bajeti yake kuu ya mwaka 2022/2023, fedha zilizotengwa zinatumika na kukamilika kwa kiwango cha lami.

Alieleza kuwa, kwa sasa tayari jumla ya kilomita 5.5 za barabara hiyo imeshawekea lami nyepesi ‘primer’ yenye leya tatu, ambayo ni kutoka Kipapo hadi Mgelema.

 ‘’Kutoka ilipoanzia eneo la Kipapo hadi kijiji cha Mgelema, yari kumeshawekewa lami nyepsi na ambapo sasa iko tayari kuwekewa lami moto na kikokoto zake nyembamba,’’alieleza.

Hata hivyo Afisa Mdhamini huyo alisema, katika barabara hivyo zipo daraja nne, ambapo mbili ni kubwa na moja imeshakamilika ujenzi wake na nyingine ikiendelea.

Kuhusu kilimita zilizobakia, alisema kilomita 1, imeshasafishwa kutoka eneo la kijiji cha Mgelema hadi Wambaa, ambapo kazi hiyo kwa sasa imesimama kutokana na ujenzi unaoendelea wa daraja.

 Hata hivyo amesema kwa sasa wanaendelea na matengenezo ya mtambo wa kusagia kokoto, ambao uliharibika hivi karibuni, na mara utakapotengenea wataanza kazi ya uwekaji kokoto nyepesi kwenye barabara hiyo.

‘’Lakini pia kazi nyingine ambayo tunaweza kuirudia ni uwekaji wa lami nyepesi ‘primer’ kwa yale maeneo ambayo yamesharibika kutokana na kukaa kwa muda mrefu,’’alifafanua.

Baadhi ya wannachi wanaoitumi barabara hiyo, wameiomba wizara kuharakisha ujenzi wake, ili waitumie kwa uhakika kuanzia Kipapo, Mgelema hadi Wambaa.

Maimuna Ali Hamad wa Wambaa, alisema sasa wanapokuwa na safari zao kutoka Wambaa kwenda Chake chake, hawaitumii tena barabara ya Mizingani, na badala yake huitumia ya Mgelema.

Othman Mjaka Nassro wa Mgelema walisema, bado changamoto ni kutomalizika kwa wakati, hali ambayo inampa hofu wa kusimama kwa ujenzi wake na kurudi tena kwenye shida.

Kaije Ali Said na Mwanahama Amour Ali walisema ni vyema ujenzi ukaharakishwa, ili waweze kuitumia hadi Wambaa hata kipindi cha mvua.

 Akiwasilisha malengo ya bajeti ya mwaka wa fedha 2021/2022, waziri wa wizara hiyo Khalid Salum Mohamed, alisema mradi huo ulipangiwa kutumia zaidi ya shilingi bilioni 2.203, ambapo hadi kufikia mwezi Machi, 2022 kulikuwa na shilingi bilioni 1118 sawa na asilimia 50.

Hata hivyo alisema, mwaka huu wa fedha wa 2022/2023, alisema Wakala wa barabara Zanzibar, imepanga kuzijenga na kuzifanyia matengenezo barabara mbalimbali kwa kiwango cha lami za Unguja na Pemba.

Alieleza kuwa barabara hizo, zitakazogharamiwa na Mfuko wa barabara Zanzibar ni ujenzi wa barabara ya Tumbatu yenye urefu wa kilomita 9, kuendelea na ujenzi wa barabara ya Kipapo – Mgelema – Wambaa yenye urefu wa kilomita 9.3 pamoja na uwekaji wa lami katika barabara ya Kijangwani – Birikau Pemba yenye urefu wa kilomita 4.2.

                        Mwisho 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...