Skip to main content

KUMBE VIMELEA VYA 'TB' VINAUWEZO KIASI HIKI.....

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:::

KIFUA kikuu ni ugonjwa wa kuambukiza, unaosababishwa na vimelea aina ya bakteria, kitaalamu vinaitwa ‘Mycobacterium tuberculosis’.

 

Vimelea hivi kikawaida havionekani kwa macho matupu, mpaka muhusika atumie kifaa maalum kinachoitwa darubini.

 

Ugonjwa wa kifua kikuu kitaalamu unaoitwa ‘Tuberculosis’ TB’ ni miongoni mwa magonjwa 10, yanayosababisha vifo kwa wingi duniani kote.

 

Pamoja na kwamba, ugonjwa huo umeenea ulimwenguni, lakini kutokana na hali ya kiuchumi kwa nchi za bara la Afrika ulivyo, ndio nao umekuwa hatari zaidi.

 

Tafiti zilizofanywa na Shirika la Afya Ulimwenguni ‘WHO’ zinaarifu kuwa, inakisiwa watu milioni 10 wameugua kifua kikuu ‘TB’ duniani kote, hadi kufikia mwaka 2020, na kati ya hao watu milioni 1.5 wamefariki dunia.

 

Utafifi huo ukagundua kuwa, kwa Zanzibar inakisiwa kuna wagonjwa 124 katika kila watu 100,000 ambapo hii ni  sawa na wagonjwa  1,612 kwa mwaka.

 

Hadi mwaka 2021, Zanzibar kuligundulika jumla ya wagonjwa 1,090 ambapo hao ni sawa na asilimia 68 ya lengo lililowekwa la kuwafikia wananchi kuwafanyia uchunguuzi, ingawa kulikuwa na vifo sawa na asilimia 6 katika mwaka 2020.

 

DALILI ZA KIFUA KIKUU

Mtaalamu kutoka kitengo shirikishi cha maradhi ya ukoma, kifua kikuu na Ukimwi Zanzibar, Said Khamis Ahmada, anasema kila ugonjwa unazo dalili zake, kama ilivyo kwa kifua kikuu.

 

Moja kati ya hizo nyingi ni kikohozi cha muda mrefu, kuanzia wiki mbili ‘2’ au zaidi, ambapo mtu anaweza kukohoa mfululizo au kukatisha katisha.

 

‘’Kila mmoja na afya yake, inawezekana mwengine akapata wiki moja kikohozi hicho, na mwengine akapindukia wiki mbili, na kisha wakifanya vipimo wakagundulika,’’anasema.

 

Dalili nyingine ni kukohoa makohozi ambayo wakati mwengine huchanganyika na damu, ambayo huanza mapesi mepesi mfano wa mafuta ya nazi na kisha kuwa mazito mfano wa mafua mapevu.

 

‘’Haina maana kuwa, kila anayetoka makohozi na damu ana dalili ya kifua kikuu, bali tunaweza kumuita mhisiwa na kisha baada makohozi kuoteshwa, jawabu litatoka,’’anaeleza.

 


Hapa chakijifunza ni kuhakikisha kila mwenye homa kali na kikohozi cha muda mrefu, ni kufika kituo cha afya na kuomba kupewa chombo maalum, ili kuchunguuzwa makohozi.

 

Lakini hata kutokwa na jasho jingi wakati wote na hasa nyakati za usiku, hata kama hali ya hewa ni ya baridi, ambapo mtu huyo hushauriwa kufanya vipimo.

 

Dalili nyingine kwa mtu ambae ni mhisiwa wa ugonjwa wa kifua kikuu ni kukonda na kupungua uzito bila ya kuwepo kwa sababu maalum.

 

Maana inawezekana, mwengine amekonda kwa kufukuzwa kazi, kuachwa, kuolewa, kubaguliwa, kunyanyapaliwa au kuishi na ugonjwa na mwengine.

 

Anabainisha kuwa, kwa baadhi ya watu ambao ni wahisiwa wa kifua kikuu, huwa na dalili ya homa za mfululizo wiki mbili na wengine Zaidi, hasa wakati wa jioni.

 

VIPI UCHUNGUUZI WA KIFUA KIKUU UNAFANYIKA?

Wataalamu wanasema, uchunguzi wa kifuakikuu unafanyika kwa njia tatu kuu, ikiwa ni pamoja na kupima makohozi kwenye maabara kwa kutumia kipimo cha ‘Gene Expert’.

 

Njia nyingine ni ya kutumia darubini, kuotesha makohozi katika maabara, kwa ajili ya ugunduzi wa vimelea na pia kubainisha dawa zinazofaa kuua vimelea vilivyooteshwa.

 

Njia nyingine ni ya uchunguuzi wa kifua kwa kupiga picha ya kifua ‘x-ray’ pale ambapo, vimelea havijaonekana kwenye darubini.

 

LIPI LENGO LA MATIBABU?

Wataalamu wa afya ya mwanadamu wanasema kuwa, kila aina ya matibabu yanayofanyika hospitalini na vituo vya lengo ni kuponyesha mgonjwa husika.

 

Pamoja na lengo hilo kuu, lakini kwa upande wa ‘TB’ pia ni kuzuia maambukizi yasienee katika jamii au ya watu wengine hata mfano wa wanafamilia.

 


Ndio maana, Mratibu wa Kikfua kikuu na Ukoma kanda wa Pemba Dk. Hamad Omar Hamad, anasema wamekuwa wakihimiza jamii wasisubiri kutibu, bali wakimbilie kwenye kinga.

 

‘’Kila siku tunazungumza kuwa kinga ni bora kuliko tiba, ndio maana tunataka kila mmoja, kila baada ya muda afanye uchunguuzi wa afya yake,’’anashauri.

 

Mratibu huyo akafafanua kuwa, lengo jengine la matibabu ni kuzuia usugu wa dawa ‘TB sugu’ maana kama mtu atajihisi ana dalili za kifua kikuu, na kukosa dawa kwa wakati atazalisha ‘TB sugu’.

 

Kumbe hata lengo kuu la matibabu pia ni kuona kunazuiwa kwa vifo vitokanavyo na kifua kikuu, ambapo kwa sasa inakadiriwa watu milioni 10, wameugua ugonjwa huo duniani kote, na hadi mwaka 2020, na kati ya hao, milioni 1.5 wamefariki dunia.

 

MATIBABU YA TB YANAKUWAJE?

Mtaalamu wa magonjwa ya kifua kikuu na ukoma kutoka kitengo shirikishi Zanzibar, Valeria Rashid, anasema matibabu ya ‘TB’ huchukua kati ya miezi sita (6), hadi mwaka mmoja.

 

Ambapo mgonjwa anatakiwa kula dawa chini ya usimamizi ‘nyumbani au kituo cha afya’ kilichokaribu naye, ili kupata uhakika wa dozi vizuri.

 

‘’Haina maana kuwa jamii hatuiamini, lakini kwa umakini na tahadhari, tunapendelea iwe hivyo, ili kuona dozi anayotumia imemponyesha ama laa,’’anasema.

 

Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui, anasema vituo vyote vya afya vya watu binafsi na serikali, vinatoa matibabu bila ya malipo, kwa wagonjwa wote wa ‘TB’.

 

‘’Ni fursa kwa wananchi kufanya uchunguuzi wa afya zao, na ikiwa wamegundulika na ‘TB’ wanapewa matibabu bure katika vituo na hospitali zote za serikali na watu binafsi,’’anaeleza.

 NJIA ZA KUZUIA KUENEA KIFUA KIKUU

Jamii imekuwa ikishauriwa, hata kupungua ama kuondoka kwa ugonjwa wa Corona, lakini bado njia moja kubwa ya kuzuia kifua kikuu ni kufunika mdomo na pua, wakati wa kukohoa au kupiga chafya.

 

Njia nyingine, ni kuhakikisha kwamba watu walio karibu na mgonjwa wa kifua kikuu ambao wanakohoa, wanachunguzwa afya zao ili kuangaliwa kama wana kifua kikuu ama laa.

 

Jingine ni kila mmoja kujiepusha na misongamano ili kuruhusu hewa ya kutosha mfano sokoni, kwenye usafiri wa umma, maeneo ya kielimu na nyumba za ibada.

 

LIPI JUKUMU LA VYOMBO VYA HABARI

Septemba 18 mwaka huu, Kitengo shirikishi cha Kifua kikuu, homa ya ini, Ukiwmi na Ukoma kilikutana na waandishi wa habari wa vyombo mbali mbali, ili kukisaidia kitengo hicho.

 

Hapa waandishi hao wa habari, pamoja na mambo mengine walitakiwa kuielimisha jamii, athari za unyanyapaa kwamba zinaweza kuzuia mapambano dhidi ya magonjwa hayo.



Akifungua mkutano huo, Meneja Mpango wa Shirikishi wa magonjwa ya Ukimwi, Kifua kikuu na Ukoma Pemba Khamis Hamad Khamis, alisema vyombo vya habari, ni nyenzo pana ya kutoa elimu ya kupambana na magonjwa hayo.

‘’Tafiti zinaonesha kuwa, hadi mwaka 2020 duniani kulikuwa na watu milioni 10, waliopata ugonjwa wa kifua kikuu na kati yao, milioni 1.5 waliripotiwa kufariki dunia,’’alifafanua.

‘’Kama vyombo vya habari vitafanyakazi kazi zake kwa kina juu ya kutoa elimu ya umuhimu wa kuchunguuza afya na athari za unyanyapaa, idadi ya wanaochunguuza itaongezeka,’’anasema.

Baadhi ya waandishi wa habari akiwemo Mchanga Haroub Shehe aluyekuwa wa Shiria la Utangazaji Zanzibar ZBC, na mwenzake kutoka Sauti ya Ist-qama Salim Ali Msellem, walisema mikakati endelevu inahitajika ili kutokomeza magonjwa hayo.

             mwisho

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch