Skip to main content

WAJUMBE WATORO KAMATI YA SIKU 16 KUPINGA UDHALILISHAJI WAOMBWA JAMBO PEMBA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:::::

WAJUMBE wa kamati ya kuelekea kilele cha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kisiwani Pemba, wameombwa kuacha dharura zisizo za msingi, na kushiriki kikamilifu katika vikao vya matayarisho.

 

Kauli hiyo, imetolewa Oktoba 20, mwaka 2022 na Katibu wa muda wa kamati hiyo, Safia Saleh Sultan kwenye kikao kazi cha kupanga mikakati na namna ya kufanikisha kilele hicho, kilichofanyika Kituo cha Huduma za sheria Zanzibar ‘ZLSC’ tawi la Pemba.

 

Alisema jambo hilo ni jepesi mno kulifanikisha, ikiwa wajumbe waliojikubalisha kuingia kwenye kamati hiyo, watahudhuria kwenye vikao vinavyoitwishwa.

 

Alieleza kuwa, kutokana na mpangilio walivyofikiria kufanikisha siku 16 za kupinga udhalilishaji, unaweza kufanikiwa ikiwa wajumbe hawatokatisha vikao vinavyoitwisha kila muda.

 

‘’Moja ya changamoto kubwa ni wajumbe kujaa dharura wakati tunapoendesha vikao vyetu, sasa kwanza waje kisha tuone tunafanikisha shughuli yetu kwa wepesi,’’alieleza.

 


Katika hatua nyingine, Katibu huyo wa muda, alisema wanakusudia kuonana na mkuu wa mkoa wa kusini Pemba, ili kuona wanapata baraka na ushauri kwa baadhi ya mambo waliokwisha yapanga.

 

‘’Siku zote tunapokuwa na shughuli zetu mbali mbali, mkuu wa Mkoa amekuwa sehemu ya ufanikishaji, sasa tunakusudia kumfuata, baada ya kumaliza kupanga kwa hatu za awali sisi kamati,’’alifafanua.

 

Kwa upande wake mjumbe wa kamati hiyo Khalfan Amour Mohamed, alisema kimsingi uwepo wa wajumbe waliokudusudia ni njia rahisi ya kufanikisha shughuli hiyo.

 

Akizungumzia kuhusu muelekea wa shughuli hiyo, alipendekeza kuwa, kinachoweza kupunguza gharama ndio kiangaliwe, ingawa lengo ni kufikisha ujumbe wa jamii.

 

Nae mshika fedha wa kamati hiyo Siti Habib Mohamed, alisema bado bajeti rasmi ya shughuli haijapitishwa kutokana na baadhi ya wajumbe kutohudhuria.

 

Kwa upande wake mjumbe kutoka ‘KUKHAWA’ Hafidh Abdi Said, alisema ni vyema wakaangalia zaidi kutoa elimu ya kujiepusha na udhalilishaji kwa wanafunzi wa skuli na madrassa.

 

‘’Tukielekea siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, tusisahau kuwa watoto ndio waathirika wakubwa, hivyo hata kama kuna mabonanza, lakini utoaji elimu skuli na madrassa upewe kipaumbele,’’alipendekeza.

 

Wiki iliyopita kamati hiyo, tayari imeshaonana na Mkuu wa wilaya ya Chake chake Abdalla Rashid Ali, ambae alitaka kuona vile vijiji vyenye matukio mengi ya udhalilishaji, kufikiwa kielimu.

 

Hata hivyo mkuu huyo wa wilaya, alipongeza wazo la kamati hiyo, kutaka kusaidiana na serikali, katika azma yake ya kupunguza na kuondoa kabisa matendo hayo.

 

Hadi Oktoba 20, mwaka huu ratiba pendekezwa ni kuanza shughuli hizo Novemba 24, kwa wajumbe kuzungumza na wananchi kupitia vyombo vya habari.

 

Novemba 26, kuwepo kwa matembezi ya uzinduzi wilaya ya Mkoani, kutoa elimu kwa wananchi kupitia redio Jamii Mkoani, Novemba 27, kuanza kuruka kwa vipindi vya redio na tv.

 

Aidha ratiba hiyo ya awali, ilipendekezwa kuwa, kuanzia Novemba 28 ni kutoa elimu ngazi ya skuli na madrassa za kur-an, Novemba 29 hadi Disemba 3 kufanyike makongamano kwa wilaya zote nne za Pemba.

 

Aidha wajumbe hao walipendekeza kuwa, Disemba 4, mwaka 2022 iwe ni siku ya bonaza la mpira wa miguu eneo la Tumbe, na michezo mengine kwa ajili ya watu wenye ulemavu, katika viwanja hivyo.

 

Vipindi vya redio na tv, vitarudi tena kuanzia Disemba 5 hadi 9, na Disemba 10, ndio siku ya kilele kinachotarajiwa kufanyika kiwanda cha Makonyo Wawi Chake chake.

 

Hadi sasa taasisi zinazounda kamati hiyo na kuhudhuria kwenye kikao cha mwisho ni ZLSC, CHAPO, My hope Foundation, KUKHAWA, blog ya Pemba today, ZAPDD, PEGAO ambazo zote na nyingine zimetakiwa kuwasilisha nembo (logo zao) kwa kamati.


Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ni kampeni ya kimataifa ya kupinga ukatili dhidi ya wanawake, ambapo kampeni hii hufanyika kuanzia tarehe 25 Novemba na kumalizika tarehe 10 Desemba ya kila mwaka.

 

Siku hiyo ilianza kuadhimishwa rasmi mwaka 1991, siku hii inaongozwa na Kituo cha kimataifa cha Wanawake tarehe 10 ilichaguliwa rasmi kuwa siku ya kilele cha maadhimisho haya ikiambatana na siku ya haki za binadamu duniani.

 

 

                           MWISHO   

 

                       

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch