Skip to main content

TUME YA TAIFA UNESCO YAWAFARIJI WAHANGA AJALI YA MOTO ZANZIBAR



 NA HAJI NASSOR, ALIPOKUWA UNGUJA

TUME ya taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzanian imesema iliguswa mno na ajali ya moto iliyoteketeza nyumba za familia 19 mwezi August mwaka huu eneno la mji Mkongwe Zanzibar na mtu mmoja kufariki.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu mtendaji wa tume hiyo katika hatuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Kaimu Katibu Aboud Idd Khamis kwenye hafla ya kukabidhi ubani wa fedha taslim kwa wahanga hao hafla iliyofanyika nyumba za wazee Sebleni mjini Zanzibar.

Alisema UNESCO ni sehemu ya familia ya mji Mkongwe na jamii kwa ujumla hivyo iliguswa na kuhuzunishwa mno na ajali hiyo ambayo pia mtu mmoja alifariki dunia.




Kaimu Katibu huyo mtendaji alieleza kuwa ajali hiyo ilipoteza pia mali za wakaazi wa shehia ya Kiponda kufuatia kukosa muda wa kuziokoa ingawa hilo ni mipango ya Muumba.

'"Sisi tulipopata taarifa hii kwa kweli tulikosa amani na kuwakumbuka mno binadamu wenzetu na hasa kwa vile kulikuwa na kifo na majeruhi,"alisema.

Katika hatua nyingine Kaimu Katibu huyo mtendaji wa tume ya taifa ya UNESCO ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Aboud Idd Khamis aliwakumbusha wananchi umuhimu wa kuchukua tahadhari katika majanga kama hayo.



Kwa upande wake Katibu mkuu ofisi ya Makamu wa Pili wa rais Zanzibar Thabiti Idarus Faina alisema wakati umefika sasa kwa wananchi kujiunga na mashirika ya bima.

Alisema wananchi kujiunga na mashirika hayo kunasaidia kwa kiwango kikubwa pale inapotokezea majanga kupata usaidizi wa kureresha mauimivu ya awali.

Aidha alieleza kuwa serikali haitomuacha mtu nyuma na kudhalilika na hasa ikiwa amekumbwa na majanga.

"Kama tulivyowaahidi mara baada ya kutokezea ajali hii kuwa serikali itawasaidia lakini pia tutawatafuta na wenzetu na leo wapo tume ya taifa ya UNESCO itawapatia chochote alisema,""alisema.

Akizungumza katika hafla hiyo Katibu mkuu wizara ya Maendeleo ya Jamii jinsia wazee wanawake na watoto Zanzibar Maryam Juma Sadala aliipongeza tume hiyo kwa kuwakumbuka wahanga hao.

Alisema tume hiyo pamoja na kwamba ni mdau wa Mjimkongwe lakini imekuwa karibu mno na makundi mbali mbali katika jamii.






Baadhi ya wahanga wa ajali hiyo akiwemo Riziki Idd Mwalim alisema msaada huo wa fedha ni faraja kwao.

Nae Amina Rashid Abass na mwenzake Abass Rajab Issa walisema hasara walioipata ni kubwa ikiwa ni pamoja kuyahama makaazi yao.



Ajali hiyo ya moto iliyotokezea shehia ya Kiponda eneo la Mjimkongwe wilaya ya mjini Unguja August 30 mwaka huu familia 19 zilikosa makaazi na mtu mmoja kufariki dunia.

                                                       Mwisho.........

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch