Skip to main content

WAJAWAZITO MWAMBE, WAMBAA, KENGEJA WALILIA BARABARA CHAKAVU

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA

WAJAWAZITO wa shehia za Mwambe, Kengeja, Wambaa na Chumbageni wilaya ya Mkoani Pemba, wameomba kufanyiwa matengenezo ya dharura barabara zao, ili zipitike kwa utulivu wakati wote.

Walisema, wamekuwa na changamoto ya usafiri kwa salama, kutokana na barabara zao kuharibika kwa kuwepo mashimo yenye kina kirefu.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti, walisema wakati umefika sasa kwa mamlaka husika kuwaonea huruma, kutokana na barabara wanazozitumia kuchakaa.

Asha Amini Hilali wa Mwambe alisema, baarabara yao, sasa imekuwa tishio hata kwa garia ya aina gani, kwa kuwepo mashimo yanayohatarisha usalama wao.

‘’Wakati mwengine sisi wajawazito tunalazimika kwenda hospitali ya rufaa ya Abdalla Mzee, lakini wasisi ni kupata mitikisiko kwa ubovu wa barabara,’’alisema.

Nae Hamida Machano Makame, alisema mwanzoni mwa mwaka huu, alijifungulia ndani ya gari eneo la Mahuduthi, baada ya gari aliyokuwa akipelekewa hospitali kuingia shimoni na kukatika.

Alieleza kuwa, baada ya kufika kituo cha uzazi cha Mwambe kesi yake ilikuwa kubwa na usiku huo was aa 7:00 alitakiwa kwenda hospitali ya Abdalla Mzee ingawa hakufika alijifungulia njiani.



‘’Bara bara yetu sio rafiki kwa sisi wananchi na hasa wajawazito, baada hupata mitikisiko na mihangaiko, ambayo wakati mwengine huzidisha maumivu,’’alieleza.

Kwa upande wake Hadia Juma Khamis wa Wambaa, alisema mtoto wake, aliharibu mimba ya miezi mitatu njiani, baada gari aliyopanda kuserereka na kuingia msingini.

‘’Ilikuwa ni siku ya mvua mashimo yamejaa maji, dereva haoni vizuri, lakini wakati analikimbia shimo, ili ndio chanzo cha ajali ndogo na mtoto wangu kumwagida damu papo hapo,’’alieleza.

Muume wa mwanamke huyo Khamis Issa Khamis alisema, wameguwa wakitoleshwa fedha kati ya shilingi 50,000 hadi shilingi 40,000 kutoka Wambaa hadi hospitali ya Abdalla Mzee.

‘’Madereva ukienda kuwataka usafiri wanaifikiria mara mbili barabara ya Wambaa- Mzingani, hivyo wanapiga fedha kubwa, ili ajihakikishie mafuta na matengenezo,’’alieleza.


Ali Mkubwa Khamis ambae ni dereva, alisema wamekuwa wazito kuzitoa gari zao hasa nyakati za usiku kutokana na ubovu uliokithiri wa barabara yao.

Sheha wa shehia ya Chumbageni Mgeni Othman Shaame, alisema kila anapoandika ripoti, kwenye eneo la changamoto ubovu wa barabara yao huingiza.

‘’Ukieleza wilayani tunaelezwa kuwa barabara zote zimo kwenye mpango wa ujenzi, na sisi tunaamini itajengwa na wananchi waendelee kustahamili,’’alieleza.

Mkuu wa wilaya ya Mkoani Khatib Juma Mjaja, alisema anaelewa vyema kuwa zipo barabara kadhaa ikiwemo ya Mizingani –Wambaa, Mtambile- Mwambe, Mtambile- Kangani na Kenya –Chambani kuwa zimeshachakaa.

Alisema, mpango wa serikali kuu ni kuzijenga upya kwa kiwango cha lami, kama ambayo imekuwa ikiahidiwa na rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi.

Afisa Mdhamini wizara ya Ujenzim Mawasiliano na Usafirishaji Pemba Ibrahim Saleh Juma, alisema barabara hizo zimo kwenye mpango mkuu wenye zaidi ya kilomita 300 ambazo zitajengwa kwa kiwango cha lami.

‘’Kwa sasa hatutumii kifusi tena kujenga barabara za aina yoyote, bali mpango wa serikali ni kujenga barabara kwa kiwango cha lami, ili zidumu,’’alieleza.

Barabara hizo sita za Mzingani- Wambaa, Mtambile- Mwambe, Mtambile- Kangani, Kenya –Chambani, Chanjamjawiri- Tundanua na Chanjaani – Pujini zilifunguliwa mwaka 2012 na aliyekuwa rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein.


Mradi huo wa ujenzi wa barabara hizo, zilijengwa kwa msaada wa Serikali ya Norway, kupitia Shirika lake la Norad kwa ushirikiano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Barabara hizo zilijengwa kwa aina yake, ambapo zilitumia mfumo wa kuwashirikisha wananchi kwa njia ya nguvu kazi na kutumia teknolojia ya lami baridi, na kugharimu dola za Marekani milini 11.4 zilizotolewa na Norway na serikali ilichangia dola milioni moja.

 

                             Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch