Skip to main content

UN WAGUSWA UTENDAJI KAZI TAMWA-ZANZIBAR

 




Na Muhammed Khamis,TAMWA-ZNZ

 

Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya Wanawake (UN Women) Bi. Sima Sami Bahous amesema kazi inayofanywa na  Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA-ZNZ) kuhamasisha wanawake wengi zaidi kushiriki kwenye nafasi za uongozi ni ya kupongezwa na kuthaminiwa na kila mmoja kwa lengo la kufikia usawa wa kijinsia baina ya wanaume na wanawake. 

 

Bi Sima, ameyasaema hayo katika ofisi za TAMWA-ZNZ zilizopo Tunguu Wilaya ya kati Unguja aipofanya ziara maalumu kuzungumza na uongozi wa chama hicho pamoja na baadhi ya wawakilishi wa asasi za kiraia,viongozi wa dini na wawakilishi wa vyama vya siasa kufuatia utekelezaji mradi wa wanawake na uongozi. 

 

Amesema amefurahishwa na mbinu mbalimbali zilizotumiwa na TAMWA-ZNZ katika kutekeleza mradi huo kwa kushirikisha makundi mbalimbali yaliyopo katika jamii ikiwemo viongozi wa dini ambao wamefafanua misingi ya dini na nafasi ya Mwanamke kushika uongozi hali ambayo imesaidia kuleta  ulewa kwa jamii  na kuonedokana na mitazamo potofu iliyojengeka.

 

Sambamba na hilo kiongozi huyo wa Umoja wa mataifa alionesha kufurahishwa kwake na ubunifu mkubwa uliofanywa na TAMWA-ZNZ kuwashirikisha wanaume kwenye uhamasishaji jamii jambo ambalo kwa kiasia kikubwa lilichangia kuibadili jamii na kuona umuhimu wa wanawake kuwa viongozi jambo ambalo awali halikua likipewa nguvu kwenye maeneo mbali mbali ya Unguja na Pemba.

 

 




Aidha Msaidizi huyo wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambae pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya Wanawake (UN Women) Bi. Sima ameelezea adhma ya shirika lake ni kuendelea kufanya kazi na taasisi mbalimbali ikiwemo TAMWA- ZNZ  katika kuleta maendelo endelevu kwa wanawake abayo yanaenda sambamba na Malengo ya Milenia ya 2030 yanayosisitiza usawa wa wanawake na wanaume katika vyombo vya maamuzi.

 

Awali akimkaribisha Bi Sima, Mkurugezi wa TAMWA –ZNZ Dkt Mzuri Issa  amesema mradi wa wanawake  na uongozi umeleta mabadiliko chanya katika jamii kwani wanawake wengi wameweza kuwa na uthubutu na kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi mkuu uliopita.

 

Mradi wa Wanawake na Uongozi uliokuwa ukitekelezwa na TAMWA-ZNZ kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ulilenga kuwajegea uwezo wanawake kushiriki harakati za siasa na uongozi ili kuhakikisha wanawake wanapata fursa kwenye uongozi katika ngazi zote za maamuzi na kuondoa changamoto mbalimbali zinazowakabili wanawake ikiwemo mifumo kandamizi, tafsiri potofu ya baadhi ya misingi ya dini, udhalilishaji katika siasa na rushwa.

 

Akieleza ushuhuda mmoja miongoni mwa waliowahi kuwa wagombea katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 jimbo la Malindi kupitia chama cha ACT Wazalendo Halima  Ibrahim alisema asingeweza kuwa mgombea na kunadi sera mbele za watu kama sio ujasiri aliojengewa na TAMWA-ZNZ.

 

Alisema kupitia mradi huo ulimfanya yeye binafsi na wengi kuwa miongoni mwa wanawake wanaojiamini kwa kusimama mbele za watu na ndio maana haikua shida kwake kugombea jimbo kama la Malindi ambalo linatambulika kuwa miongoni mwa kitovu cha siasa kwa miaka mingi.

 

Hata hivyo alimuomba kiongozi huyo kufikiria kuendeleza tena mradi huo kwa kuwa bado anaamini kuna idadi kubwa ya wanawake wanahitaji kujengewa uwezo zaidi ambao awali hawakubahatika kupata fursa hiyo.

Kwa upande wake kiongozi wa dini, Khamis Abdulrahman, alisema kuwa dini haijakata wanawake kuwa viongozi bali wanatakiwa kufuata taratibu zilizipo katika imani za dini.

 

Alisema wakati wakitoa elimu kupitia mahubiri yao kuhusu nafasi ya mwanamke katika ungozi walipitia changamoto nyingi ikiwemo maneno mazito kutoka kwa jamii kutokana na mfumo dume uliojengeka kuwa mwanamke ni mlezi wa familia.

 

Alisema mradi huo umesaidia kubadilisha mitazamo hasi ya jamii kuhusu nafasi za uongozi kwa wanawake na kusema ipo haja ya mradi huo kuendelea ili kufikia asilimia ya 50 kwa 50 ya wanawake katika vyombo vya maamuzi ikiwemo Baraza la wawakilishi na Bunge.

 


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch