Skip to main content

KAMATI USTAWI 'BW' YARIDHISHWA UCHAPAKAZI KAMATI ZA KUPINGA UKATILI PEMBA

                                         


                                       

NA HAJI NASSOR, PEMBA

KAMATI ya Ustawi wa Jamii ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, imesema kazi inayofanywa na kamati za kupambana na ukatili na udhalilishaji kisiwani Pemba, ni nzuri na zinafaa kuungwa mkono na wananchi, ikiwa wanataka kuondoa matendo hayo.

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo Mohamed Ahmada Salim, wakati akighairisha kikao maaluma cha kupokea na kujadili ripoti za miezi mitatu za kamati hizo, kilichofanyika ukumbi wa Kiwanda cha Mafuta ya Makonyo Wawi Chake chake.

Alisema suala la kufuatilia au kuibu matendo ya ukatili na udhalilishaji kwa jamii, ni jambo zito na huandamwa na changamoto kadhaa, ingawa kwa kamati hizo, zinaonesha mafanikio makubwa.

Mwenyekiti huyo alieleza kuwa, matendo hayo hufanyika kwa siri kubwa, hivyo huwa kunahitaji ujuzi na uweledi wa hali ya juu kuyaibua na kisha kuyafuatilia.




‘’Kwa niaba ya kamati hii, lazima wajumbe nyinyi wa kamati zote nne za Pemba tuwapongeze, maana kazi mnayoifanya ni kubwa na bado hamjakata tamaa, licha ya changamoto mnazokumbana nazo,’’alieleza.

Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo wa Kamati ya ustawi wa Jamii, alisema kamati hasa zinazohitaji umakini mkubwa ni zile kama ya wilaya ya Chake chake na Wete ambazo, zinamkusanyiko mkubwa wa watu.

Kwa upande Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mwantatu Mbarka Khamis, alizitaka kama hizo, kuzidisha ushirikiano miongoni mwao, ili kusaidiana maarifa, wakati wanapowahudumia wananachi.

Alieleza kuwa, hilo linaweza kujenga uthubu kwa kule kubadilisha uzoefu miongoni mwao, na hasa kwa vile zipo baadhi ya kamati zimefanikiwa kupunguza idadi ya makossa ya ukatili.




Mjumbe wa kamati hiyo, Zawadi Amour Nassor, alisema lazima mkazo uweke katika wilaya, ambazo zimearipoti matukio ya ulawiti, kwani haziashiria mwisho mzuri kwa watoto wa kiume.

Nae Bihindi Hamad Khamis, alisema bado kuna hatari za uwezekano wa watoto wa wilaya ya Micheweni wanaofanya kazi ya ajira za kubanja kokoto, kutendewa vitendo vya ulawiti na ubakaji, kama mkazo haukuwekwa.

Akiwasilisha ripoti ya utendaji kazi kwa kipindi cha mwezi wa Aprili hadi Juni mwaka huu, Katibu wa kamati ya kupambana na ukatili na udhalilishaji ya wilaya ya Chake chake Kassim Ali Omar, alisema wamekuwa wakijikita zaidi kutoa elimu kwa jamii.

Alieleza kuwa, hilo liemfanikiwa na ndio maana, kunaongezeko la matukio yalioripotiwa kufikia 24 kutoka 14 ya kipindi cha miezi mitatu kama hiyo, kwa mwaka uliomalizika.

‘’Inawezekana matukio yanaongezeka, lakini sisi kadiri yanavyoripotiwa, huona ndio elimu kwa wananchi na watoto imewafikia, na ndio maana wapo wanaowaripoti hadi wazazi au waalim wao,’’alieleza.



Katibu tawala wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki, alisema kwa kipindi cha miezi mitatu, walipokea matukio 37 yakiwepo ya ubakaji matano, utelekezwaji 21, ulawiti matukio mawili na makosa ya mvutano wa malezi matatu.

Hata hivyo amesema changamoto kubwa, ni jamii kutobadili mtazamo na kuendelea kuzifanyia sulhu kesi hizo, jambo ambalo huwarejesha nyuma katika jitihada zao.

Nae mjumbe wa Kamati ya kama hiyo ya wilaya ya Wete, Siti Suleiman Juma, alisema wamefanikiwa kuwafikia wananchi 1,760 kutoka shehia za Mchanga mdogo, Kojani, Mpambani na Kambini juu ya elimu ya kupinga ukatili na udhalilishaji.

                                       Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch