Skip to main content

WAZIRI MASSOUD: MAPINDUZI YA ZANZIBAR NDIO MATOKEO YA MAENDELEO YALIOPO SASA

 


 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WAZIRI wa Uvuvi na Uchumi wa Buluu Zanzibar, Massoud Ali Mohamed, amewataka wananchi kuendelea kuyathamani Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, kwani ndio msingi wa maendeleo yaliopo.

Waziri Massoud, alitoa raia hiyo jana, wakati alipomaliza shughuli za ufunguzi wa kituo cha kisasa cha ununuzi wa karafuu, eneo la Kiwani wilaya ya Mkoani Pemba, ikiwa ni sehemu ya shamra shamra za miaka 62 ya mapinduzi.

Alisema kuwa, mapinduzi sio hadithi ya kuvutia pekee, bali ni kuwepo kwa maendeleo kila sekta, kama ilivyokuwa azma ya waasisi wa taifa hili.



Alieleza kuwa, kwa mfano Kiwani iliyokuwepo kabla ya mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 na ya sasa ni tofauti, kwa kuwepo miundombinu ya kisasa, kwenye sekta ya afya, elimu, maji safi na salama na barabara.

Alieleza kuwa, hayo ndio thamani na umuhimu wa kufanyika kwa mapinduzi hayo, na sasa ipo haja kwa wananchi na hasa wapenda maendeleo, kuyathamini na kuyaenzi kwa nguvu zao zote.

‘’Niwatake wananchi wa Zanzibar, kwamba upo umuhimu wa kuyaenzi mapinduzi haya, kwani sio hadithi pekee, bali ni uwepo wa maendeleo makubwa, kila sekta,’’alifafanua.



Akizungumzia uwepo wa kituo hicho Kiwani, aliwataka wananchi kukimbilia hapo, kwa ajili ya kuuza karafuu zao.

Alieleza kuwa, usafirishaji magendo wa zao hilo, usiwe na nafasi, kwani sasa yale matakwa ya wakulima, ikiwemo vipimo vya kisasa visivyopunja, vimeshapatikana.









‘’Sasa wakulima wa zao la karafuu, ule mtindo mbaya wa kulitorosha zao hilo nje ya nchi muuache, maana kwanza bei ni nzuri na sasa tunavituo na mizani za kisasa,’’alifafanua.

Aidha Waziri Massoud, aliwapongeza ‘ZSTC’ kwa hatua yao ya kuja na mfumo wa mabadiliko ya ununuzi wa zao hilo, ambao kwa kiasa kikubwa, umeshandosha malalamiko.

Mapema Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Taifa la Zanzibar ‘ZSTC’ Soud Said Ali, amesema ufunguzi wa kituo hicho, ni dhamira ya serikali ya awamu ya nane, katika kuliimarisha zao la karafuu.

Alieleza kuwa, ujenzi huo umeakisi falsafa ya mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, ambayo imejikita katika kuwafikia maendeleo endelevu, wananchi wote.






Aidha alifafanua kuwa, ujenzi wa kituo na vyingine ni utekelezaji wa mpango kazi wa ZSTC, kusimamia, kuratibu, uimarishaji wa mifumo ya soko la zao la karafuu.

‘’Lengo kuu ni kuongeza ufanisi, uwazi, kuimarisha upatikanaji wa haki na usawa katika ununuzi, usafirishaji wa zao hilo, na kulibakishia na ubora wake, katika soko la dunia,’’alifafanua.

Katibu Mkuu wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda Dk. Habiba Hassan Omar, alisema kituo kama hicho kilichopo Kiwani, vitajengwa shehia za Kengeja na Ngwachani hapo baadae.

Mkuu wa wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki, alisema kazi inayofanywa na ZSTC, inafaa kuungwa mkono na wakulima wa zao la karafuu, kwa kuziuza karafuu hizo, kwenye vituo vya serikali.



‘’Ifike pahala sasa, karafuu zote wakulima waache kuzitorosha na sasa kuzileta ZSTC, maana mifumo ya ununuzi kuanzia majengo hadi vipo, vimeshaondoa shaka kwao,’’alifafanua.

Mradi wa ujenzi wa kituo hicho, ulianza utekelezaji wake mwaka wa fedha 2023/2024, baada ya ZSTC kutangaaza zabuni, kama sheria za manunuzi, ilivyo.

Ambapo hadi kukamilika, umegharimu shilingi milioni 406.418 ikijumuisha na ongezeko la thamani ‘VAT’, na zabuni yake ilitangaazwa Machi 12, 2025 kupitia mfumo wa serikali wa manunuzi.

Kisha baada ya mchakato wa ushindani, kampuni ya Kin Investment LTD, ilikabidhiwa jukumu la ujenzi, huku usimamizi na ushauri elekezi, ukiwa chini ya Wakala wa majengo Zanzibar ZBA.


Mkataba wa ujenzi, ulikuwa ni wa miezi 12, na kutekelezwa kwa awamu tatu, ikiwemo ya usanifu wa jengo la upatikanaji wa ithibati, ujenzi wa kituo chenyewe na awamu ya tatu ni ujenzi wa miundombinu saidizi, ikiwemo vyoo na uzio.

                         Mwisho

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...