Skip to main content

WADAU ZANZIBAR WAUNGANA KUADHIMISHA SIKU 16 ZA KUPINGA UDHALILISHAJI

                                                             
                                                      

                                                                                                           27/11/2025

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 

 

 Taasisi za kutetea haki za wanawake, vijana, watu wenye ulemavu na watoto Zanzibar,  zinaungana kwa pamoja kuadhimisha Siku 16 za Kupinga udhalilishaji. 

Maadhimisho haya yameanza rasmi tarehe 25 Novemba, Siku ya Kimataifa ya Kutokomeza udhalilishaji dhidi ya Wanawake, na yatahitimishwa tarehe 10 Disemba, 

Siku ya Haki za Binadamu Duniani. Taasisi hizo ni pamoja na Jumuiya ya Wanawake Wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA), Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA), Jumuiya ya Mazingira, Jinsia na Utetezi Pemba (PEGAO), Jumuiya ya Kupambana na Changamoto za Vijana Zanzibar (ZAFAYCO), Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar (ZLSC), Jukwaa la Vijana Zanzibar (ZYF), Pamoja Youth Initiatives (PYI) na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania , Zanzibar (TAMWA -ZNZ). 

 Mfululizo wa shughuli za maadhimisho unajumuisha kutayarisha makala na jumbe za kuelimisha jamii, kushiriki maadhimisho ya Siku ya watu wenye ulemavu tarehe 3 Disemba, maadhimisho ya siku 16 za kupinga udhalilishaji itakayofanyika tarehe 6 Disemba pamoja na kutoa taarifa ya pamoja ya hitimisho tarehe 10 Disemba ambayo ni Siku ya Haki za Binadamu. Shughuli ya tarehe 6 Disemba 2025 itakua ni maalum kwa ajili ya kujadili masuala ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 kwa mtazamo wa usawa wa kijinsia.

Kikao hiki kinalenga kuonesha mafanikio, changamoto na mwenendo wa haki za wanawake, vijana na watu wenye ulemavu katika mazingira ya kisiasa na ya kidijitali, sambamba na kutoa mapendekezo yanayolenga kuimarisha ushiriki jumuishi kwa makundi haya. 

 Kwa upande mwengine, taasisi hizi zinaeleza wasiwasi wake kutokana na kuwepo vitendo vya udhalilishaji wa mitandaoni, ikiwemo kusambaza picha na video za faragha bila ridhaa, udukuzi wa taarifa, lugha ya chuki na vitisho vinavyolenga kuwanyamazisha wanawake katika siasa, uongozi, na majukwaa ya umma. 

Vitendo hivi vimeripotiwa kusababisha madhara makubwa ya kijamii na kisaikolojia, huku baadhi ya waathirika wakikumbana na unyanyapaa, kuacha masomo au kukosa fursa za kiuchumi kutokana na unyanyasaji huu wa mtandaoni. 

Tafiti mbalimbali na ripoti kutoka vyombo vya habari zinaonesha kuwa waathirika wengi, hasa wanawake na wasichana, hurekodiwa au husambaziwa taarifa za faragha bila ridhaa, jambo linalopelekea aibu ya hadharani na kuongezeka kwa vitendo vya kuwatapeli mtandaoni (cyberblackmail).

Taasisi hizi zinatoa wito kwa mamlaka husika kuhakikisha kesi zinachunguzwa kwa ufanisi, na kuanzisha mifumo rafiki ya utoaji taarifa inayowalinda waathirika kwa usiri, usalama na heshima. Sambamba na hilo, jamii inahimizwa kukuza utamaduni wa kuheshimiana na matumizi salama ya teknolojia ili kujenga mazingira jumuishi yanayowawezesha wanawake na wasichana kushiriki kikamilifu katika majukwaa yote. 

 Kaulimbiu ya Kimataifa mwaka huu ni “TUUNGANE Kukomesha Ukatili wa Kidijitali Dhidi ya Wanawake na Wasichana”, huku ujumbe wa kitaifa ukiwa ni “Mitandao Salama ni Haki: Maliza Ukatili wa Kimtandao kwa Wanawake na Watoto.” 

 Kwa zaidi ya miongo mitatu, Kampeni ya Siku 16 za Kupinga udhalilishaji imeendelea kuwa jukwaa muhimu kwa serikali, asasi za kiraia na wadau mbalimbali kuhamasisha mabadiliko ya sera, elimu ya jamii, tafiti na hatua za pamoja ili kukomesha aina zote za udhalilishaji ikiwa ni pamoja na ukatili wa kimwili, kiuchumi, kisaikolojia, kijinsia na sasa ukatili wa kidijitali unaozidi kuongezeka. 

 Imetolewa na: 

 Jumuiya ya Wanawake Wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA) Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) Jumuiya ya Mazingira, Jinsia na Utetezi Pemba (PEGAO) Jumuiya ya Kupambana na Changamoto za Vijana Zanzibar (ZAFAYCO) Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar (ZLSC) Jukwaa la Vijana Zanzibar (ZYF) Pamoja Youth Initiatives (PYI) Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA) Zanzibar

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...