Skip to main content

WAANDIKISHENI WATOTO WENYE ULEMAVU SKULI "MDHAMINI ELIMU"

 


NA MOZA SHAABAN, PEMBA

WAZAZI na walezi wenye watoto wenye ulemavu wametakiwa kuwaandikisha watoto hao skuli kwa mwaka wa masomo unaotarajiwa kuanza 2026, ili kuhakikisha upatikanaji wa haki ya msingi ya elimu kwa watoto hao.

Wito huo umetolewa na Afisa mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali  Pemba Mohamed Nassor Salim wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi, alisema zoezi la uandikishaji wanafunzi wapya kwa mwaka wa masomo 2026 linaendelea kwa watoto wote waliofikia umri wakiwemo wenye ulemavu.

Alisema wakati umefika kwa wazazi, walezi jamii na serikali za shehia kuhakikisha watoto wenye ulemavu wanapata haki yao ya msingi ya elimu, kwa kuhakikisha wanandikishwa skuli bila kujali mahala wanapoishi au aina ya ulemavu walionao.

Aliongeza serikali kupitia wizara ya elimu imeandaa mazingira rafiki kwa watoto wenye ulemavu ambao wanaishi katika mazingira magumu, kwa kuwajengea skuli maalumu inayotoa elimu mjumuisho ili kuhakikisha wanapata haki yao ya msingi ya elimu kama ilivyo kwa watoto wengine.

" Ili kuhakikisha kila mtoto wa Zanzibar anapata haki yake ya msingi ya elimu kama zinavyoeleza sheria na sera, serikali inaendelea  kuweka mazingira rafiki kwa watoto wote wakiwemo wenye ulemavu, na tumejenga skuli ya elimu mjumuisho na tunaendelea kusajili wanafunzi wenye sifa, hivyo ni muhimu jamii kuunga mkono hili  kwa kuhakikisha watoto hao wanaandikishwa, " alieleza.

Alisema kwa mwaka wa masomo 2026 ambao uandikishaji wake unaendelea, skuli ya elimu mjumuisho iliopo pujini kwa mara ya kwanza itakua na darasa la elimu ya maandalizi, huku lengo likiwa ni kuhakikisha watoto wote wanapata haki sawa ya elimu.

Aidha alisema kua, ili kuhakikisha jamii inakua na muamko zaidi kuhusu ulazima wa upatikanaji elimu kwa watoto wenye ulemavu, wizara imeanzisha kampeni ya kushajihisha jamii kulitimiza hilo kwa kushirikiana na viongozi wa shehia.

Alisema ni vyema wazazi kitumia fursa hiyo ya uwepo wa skuli ya elimu mjumuisho ya Pujini Chake chake Pemba kwa kuwaandikisha watoto wenye ulemavu, kwani kuna miundombinu rafiki kwa ajili ya kufundishia na kujifunzia.

Nae Mwalimu wa wanafunzi wenye ulemavu wa uoni na uoni hafifu kutoka skuli ya Elimu  Mjumuisho Pujini  Hanifa Abeid Ali alisema, kuelekea mwaka wa masomo 2026 wameshasajili wanafunzi wapya 30 ambao wanaulemavu wa aina mbali mbali.

Akitoa wito kwa wazazi wenye watoto wenye ulemavu ambao hawajawaandikisha na umri umesharuhusu mwalimu huyo  alisema, ni vyema kuwaandikisha watoto wao skuli ili kupata haki yao ya msingi ya elimu, kwani ulemavu si sababu ya mtoto kutosoma.

Nae mwalimu Anipae Amiri Manallah kutoka skuli hio  aliiomba wizara ya elimu kuendelea kuboresha miundombinu ya skuli hiyo kwa kuongeza vifaa vya kujifunzia na kufundishia pamoja na waalimu ili lengo la utoaji elimu bora liweze kufikiwa.

Skuli ya elimu Mjumuisho Pujini imajumla ya wanafunzi 76 wenye ulemavu wa aina tano, ukiwemo ulemavu wa uoni /uoni hafifu, Uziwi, Viungo, Albino na Matamshi, na hadi sasa inawanafunzi wa darasa la kwanza hadi la tano.

Aidha kwa mujibu wa sera ya elimu ya Zanzibar inasema wizara ya Elimu itahakikisha haki na fursa za elimu inazotoa kwa wazanzibari wotewote,  zinatolewa kwa misingi ile ile kwa watu wenye ulemavu.

                                                                     MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...