Skip to main content

SHEHA CHUMBAGENI LEO KUWAONGOZA WANANCHI KIDUTANI UPITISHWAJI KANUNI ZA KIJIJI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

SHEHA wa Chumbageni wilaya ya Mkoani, Mgeni Othman Shaame, jioni ya leo anatarajiwa kuwaongoza wanachi wa kijiji cha Kidutani, kuzipitisha sheria ndogondogo, zitakazowaongoza wananchi hao, ili kujenga tabia njema.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Katibu wa kamati ya elimu na maadali ya kijiji hicho Machano Ali Makame, alisema jioni ya leo, kijijini hapo watakuwa na ugeni wa shehia yao.

Alisema kuwa, sheha huyo pamoja na ujumbe wake akiwemo askari wa shehia, watakutana na wananchi hao, na kuzijadili kwa mara ya mwisho kanuni, hizo kabla ya kuzipitisha rasmi.

Alieleza kuwa, kijiji hicho kimeamua kuanzisha kanuni hizo, ili kuwasawaidia vijana kuwaelekeza kwenye maadili mema, ili wawe raia bora wa taifa hili.

‘’Ni kweli jioni ya leo, Sheha wa Chumbageni ataungana na wananchi wa kijiji cha Kiduatani, ili kuzipitisha kanuni, ambazo zilianzishwa na wananchi wenyewe,’’alisema.

Mwenyekiti wa kamati hiyo Mwalimu Saleh Abdalla Mohamed, alisema moja ya kanuni ambazo zitarajiwa kupitishwa, ni kusitisha muda wa kuranda ovyo mitaani hapo nyakati za usiku.

Alieleza kuwa nyingine ni kupiga marufuku matumizi ya sigara kwa watoto, pombe, upigaji ngoma, wizi, uvaaji wa nguo za mbano, ukataji nywele usio wa maadili.

‘’Kanuni nyingine ambayo jioni ya leo sheha atazikagua na kuzipitisha pamoja na wananchi wenyewe, ni uvaaji za suruali juu ya magoti kwa wanaume, vigenge hatarishi na kuwarejesha masomoni walioacha,’’alifafanua.

Kwa upande wake Katib wa sheha wa shehia  hiyo, Abdalla Salim Juma, alisema maandalizi yote kwa ajili ya mkutano huo wa jioni ya leo, yameshakamilika.

Alisema, tayari wajumbe wa sheha, askari wa shehia na sheha mwenyewe, wameshaarifiwa kwa ajili ya kuhudhuria mkutano huo wa leo.

‘’Ni kweli wananchi wenzetu wa kijiji cha Kidutani, waliamua kuanzisha kanuni, ambazo leo uongozi wa shehia ya Chumbageni, unakwenda kukutana na wananchi na kuzipitisha kwa pamoja,’’alifafanua.

Baadhi ya wananchi wa Kidutani, akiwemo Juma Abassi Ali, alisema wanatamani haraka mkutano huo, ufanyike na kanuni hizo, zianze kazi.

Nae Time Pandu Makame, alisema kijiji hicho ingawa kina wananchi kidogo, lakini kimekuwa kikitumbukia kwenye wizi wa mifugo, utoro wa wanafunzi pamoja na tabia nyingine chafu.

Hivi karibuni Mkuu wa wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki, aliwataka wananchi, kuendelea kuzifufua polisi jamii, ambazo huwa ni masaada mkubwa wa kuzuia uhalifu.

                Mwisho  

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...