Skip to main content

'WARATIBU WA UCHAGUZI PITIENI SHERIA, KANUNI KWA UMAKINI': JAJI MSTAAFU



NA MOZA SHAABAN, PEMBA

WASHIRIKI wa mafunzo ya uratibu wa Uchaguzi kisiwani Pemba wametakiwa kuzipitia na kuzifuata vyema sheria, kanuni, taratibu  na miongozo ya uchaguzi ili kutekeleza ipasavyo majukumu yao.

Wito huo umetolewa leo Julai 21, 2025 na  Jaji mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mbarouk Salim Mbarouk ambae pia ni mgeni rasmi katika mafunzo hayo yaliofanyika Wawi Chake  chake Pemba.

Alisema ni vyema kwa waratibu hao kutumia muda wao kuzisoma na kuzifuata katiba, sheria, kanuni na miongozo ya uchaguzi ili kutekeleza kwa ufanisi majukumu yao katika kipindi chote cha usimamizi wa uchaguzi Mkuu.



Alieleza kua uchaguzi ni mchakato unaojumuisha hatua na taratibu mbali mbali za kisheria, zinazopaswa kufuatwa ili kuimarisha utendaji wa kazi hizo pamoja na kuimarisha amani nchi.

"uchaguzi ni mchakato unaojumuisha hatua na taratibu mbali mbali za kisheria zinazopaswa kufuatwa ili kuimarisha utendaji wa kazi  na kujua na kuzifuata sheria hizo kutasaidia  kuimarisha amani nchi, " alieleza.



Alisema kua jukumu la kusimamia ucjaguzi ni kubwa, hivyo aliwasihi washiriki wa mafunzo hayo kuyafuata mafunzo hayo pamoja na sheria na  miongozo ili kujipatia ufafanuzi wa masuala mbali mbali yanayohusu uchaguzi.

Aidha aliwataka washiriki wa mafunzo hayo kujiepusha na migogoro na kua vyanzo vya malalamiko, hivyo ni vyema kufuata kanuni na sheria zilizowekwa, huku akiwasisitiza kutoa taarifa za uchaguzi kwa tume ya uchaguzi na si sehemu nyengine isio husika.

Hata hivyo aliwataka washiriki hao kusimamia vyema jukumu la kusimamia shughuli zote za uchagazi kwa ngazi ya Uraisi na ubunge wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania, ili kuhakikisha linamalizika kwa weledi.

Mapema akiongoza kiapo cha uadilifu kwa washiriki hao Hakimu wa Mahakama ya mwanzo Chake chake Nassor Suleiman Nassor aliwataka washiriki hao kutunza siri, kua waadilifu, kujiamini na kujiepusha na migogoro ili kutunza amani iliopo.



Akieleza kaulimbiu ya Uchaguzi mkuu wa 2025 Kaimu Mkurugenzi  Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi 'INEC ' Adam Mkina alisema, kaulimbiu ya mwaka huu inaeleza kua 'Kura yako haki yako jitokeze kupiga kura " alisema kua kaulimbiu hiyo inalenga kuwasisitiza wanachi wenye sifa za kupiga kura kujitokeza kwa wingi ili kutimiza haki zao za msingi.

Nao washiriki wa mafunzo hayo walisema mafunzo hayo yatawawezesha kutimiza majukumu yao kwa ufanisi na  kuahidi kuyafanyia kazi mafunzo hayo ili kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa ufanisi.

Mafunzo hayo  yalioratibiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi INEC, yamehusisha jumla ya washiriki 59 wakiwemo waratibu wa Uchaguzi, waratibu wa uchaguzi wa Chuo cha mafunzo, wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya majimbo kwa mikoa ya kusini na Kaskazini Pemba na yanatarajiwa kudumu kwa siku tatu.

                                                 MWISHO

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...