Skip to main content

MWENYE ULEMAVU WA VIUNGO AOMBA KUPATIWA KITI MWENDO



IMEANDIKWA NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@

Mohamed Omar Mohamed mkaazi wa Machomane Chake Chake Pemba mwenye ulemavu wa miguu, ameiomba Serikali na jamii kwa ujumla kumsaidia kupata kiti cha magurudumu (wheelchair) kitakachomuwezesha kuendeleza shughuli zake za kijamii na kiuchumi kwa wepesi zaidi.

Akizungumza na ZanzibarLeo hapo nyumbani kwake Machomane, Mohamed amesema kiti ambacho amekuwa akikitumia kwa sasa kina zaidi ya miaka mitano na kimechakaa vya kutosha kiasi cha kushindwa kutembelea kwa mwendo unaoridhisha.

Amesema kiti alichonacho hivi sasa kimepoteza nguvu na kimekuwa kikiharibika mara kwa mara, hali inayosabisha kubaki muda mrefu bila ya kiti hicho kutokana na ughali wa matengenezo yake.

Amesema mara nying kiti hicho huharibika betri ambayo imekuwa ikiuzwa kwa bei ya Tsh. 80,000, kiwango ambacho si rahisi kwake kukimudu kutokana kipato chake kidogo.

"Najiona dhaifu mno.  Kiti mwendo ndio miguu yangu nilojaaliwa na Allah. Kutokana na hali ngumu ya kimaisha, nashindwa kununua chengine.  Kiti changu kinatumia betri nne na kila betri moja ninainunua elfu thamanini, ni ghali sana," alifafanua Mohammed.



Amesema kipato chake ni kidogo sana kiasi ambacho hakimtoshelezi wala hakikidhi baadhi ya mahitaji yake kutokana na hali ya ugumu wa kimaisha na ukiangalia ana familia na watoto wanaomtegemea.

Aliendelea kusema haina haja ya kukaa barabarani akawa omba omba jambo ambalo halipendezi kutokana na taswira ya miji yao, hivyo aliziomba Taasisi husika kumsaidia kuendeleza genge lake linalojishughulisha na biasha ndogo ndogo za vyakula vikavu ili kujikwamua kimaisha.

Muhamed alitoa wito kwa Serikali na Taasisi na Mashirika binafsi kumuangalia kwa macho mawili kutokana na hali yake ya uhitaji wa watu maalumu angalau kumpatia kiti cha magurudumu(wheelchair) au kumuendelezea kigenge hilo linalompatia ruzuku zake za kila siku.

Kwa upande wake sheha wa Wara Masoud Mohamed Khamis amethibitisha kuwepo kwa Mohamed  shehiani mwake kutokana na uhitaji wake wa watu wenye ulemavu amekuwa akimpatia fursa kubwa zinazotokea shehiani mwake.


"Nipo nae bega kwa bega pakitokea fursa ya aina yoyote ya ikiwa  watu wenye mahitaji maalumu hata isiwe ya makundi maluum simuachi nyuma hata mafunzo na neema zinapokuja namuangalia kwa uono mpaka kutokana na hali yake" alifafanua sheha.

Alisema ndani ya shehia yake kupitia watu wenye mahitaji maalum kutokana na uhitaji wao amekuwa akiwashirikisha kwa kila fursa zinazotokea  kupitia  vikundi vya wajasiria mali, ili kujikwamua kiuchumi.


" Mpka sasa Watu wenye mahitaji maalumu tumekuwa tukishiriana nao juu ya mahitaji yao ili wajione na watambue wana haki ya kufanya kila kitu kama mtu mwengine". alivyoa alieleza sheha.

                                                       MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...