Skip to main content

ZAINAB SHOMARI: ‘CCM ITAENDELEA KUHUBIRI AMANI, UTULIVU’

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MAKAMU Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake wa CCM Tanzania ‘UWT’ Zainab Khamis Shomar, amesema CCM, itaendelea kuhubiri amani na utulivu, maana ndio mwalimu wa vyama vingine vya siasa nchini.

 

Alisema, CCM baada ya kuwahudumia wananchi wote wa Tanzania bila ya ubagauzi, msingi wake mwingine ni kuhubiri umoja, mshikamano, amani na utulivu kwa nia ya kuwaunganisha watu wote.

 

Makamu huyo Mwenyekiti ameyasema hayo jana, uwanja wa Umoja ni Nguvu wilaya ya Mkoani Pemba, kwenye mkutano wa hadhara uliowajumuisha wana ‘UWT’ wa wilaya za Mkoani na Chake chake, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuimarisha chama kisiwani humo.

 

Aliwataka viongozi wa UWT, kuanzia ngazi ya shina hadi taifa kuendelea kuhubiri jambo hilo, kwani ndio msingi mkuu wa kwa chama hicho na vyama vingi vingine.

 

Alieleza kuwa, hata chama kinachopanga kufanya machafuko, kamwe hakiwezi kufanikisha lengo lao, kama nchi hii haina amani na utulivu.

 


‘’Sisi UWT na jumuia nyingine za chama, tumekuwa tukihimiza kila siku, kuwa ajenda yetu ya kwanza iwe ni kuhubiri amani na utulivu, kisha kuleta maendeleo kwa kila mtu,’’alifafanua.

 

Aidha Makamu Mwenyekiti huyo wa UWT taifa Zainab Khamis Shomar, aliwapongeza rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan na Dk. Hussein Ali Mwinyi wa Zanzibar, kwa kuchapuza miradi ya maendeleo.

 

Alieleza kuwa, tayari Dk. Mwinyi kwa upande wa Zanzibar ameshavuuka lengo la utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025, katika miradi kadhaa, aliyowaahidi wananchi wakati akiomba raidhaa.

 

‘’Kwa mfano, aliahidi ujenzi wa vyumba 1,500 vya madarasa, wakati wa kampeni ingawa ndani ya miaka yake mitatu ya utawala ameshajenga vyumba 2,273 hapa ameshavuuka lengo kwa asilimia 150,’’alifafanua.

 

Katika hatua nyingine, Makamu huyo Mwenyekiti wa UWT Taifa Zainab Khamis Shomari, aliwataka vijana ambao hawajasajili vikundi vyao vya ushiriki, kufanya hivyo haraka.

 

Alisema, tayari UWT imeshafanya mazungumzo na wahusika, moja wapo ni kulegeza mashrti ili kuhakikisha kila mwenye sifa anapata mkopo.

 

‘’Wakati nazungumza na baadhi ya wajasiriamali hapa Pemba, nimegundua kuwa uhitaji ni mkubwa, lakini masharti yanawarejesha nyuma waombaji,’’alifafanua.

 

Hata hivyo, amewagauikia wanaume, wenye sifa kufunga ndoa na kuacha udhalilishaji kwa watoto, kwani kufanya hivyo ni kuwazimia ndozo zao.

 

Mapema Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Leila Mohamed Mussa, alisema kasi ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, imekuwa kubwa katika sekta mbali mbali.

 


Alifamisha kuwa, Dk. Mwinyi ameridhia kuwa shilingi bilioni 550, kati ya shilingi bilioni 830, zitumike katika miundombinu ya elimu.

 

‘’Ndani ya fedha hizo zinatumika ujenzi wa skuli za ghorofa, ukarabati na ununuzi wa samani, ili kuhakikisha watoto wa Zanzibar wanasoma kwenye mazingira rafiki,’’alifafanua.

 

Akitoa taarifa za utekelezaji wa Ilani kwa mkoa wa kusini Pemba, Mkuu wa wilaya ya Mkoani Khatib Juma Mjaja, alisema kasi ya Dk. Mwinyi imekuwa kubwa ikilinginishwa na watu wanavyoizungumza.

 

Katib wa CCM mkoa wa kusini Pemba Ramadhan Kapeto, alisema CCM Mkoani humo, inathamini kwa vitendo juhudi za Dk. Mwinyi ambazo zimewafikia, watu wote bila ya ubaguzi.

 


Akimkaribisha Makamu Mwenyekiti huyo, Mwenyekiti wa UWT mkoa wa kusini Pemba Zuwena Khamis Abdalla, alisema kwa utekelezaji imara wa Ilani ya CCM uchaguzi wa mwaka 2025, unaweza kuwa mwepesi.

 

Makamu Mwenyekiti wa UWT taifa akiwa na ujumbe wake alitembelea soko la Machomane, kuzungumza na wajasiriamali juu ya namna ya kupata mikopo hiyo.

Mwisho    

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...