Skip to main content

TIMU YA SOKA YA MKOANI QUEENS BADO IPO IPO SANA, MATUNDA KIDUCHU CHANGAMOTO LUKUKI

 


NA HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@

‘HAMASA kubwa ilifanyika tokea pale ilipoanzishwa timu ya Mkoani Queens mwaka 2014 na hadi sasa kuweza kusimama’.

‘Pamoja na dharau, kejeli ambazo tumepewa lakini bado tunaendelea mbele kuhakikisha timu yetu inakata mawimbi na kusonga mbele’.

Ni kauli ya baadhi ya wachezaji wa timu ya mpira wa miguu wanawake Mkoani qunes, walipokuwa wakizungumza na makala haya kuhusiana na uhai wa timu yao.

Timu hiyo iliyoanzishwa mwaka huo wa 2014, ikiwa na wachezaji 26, imepitia madhila makubwa kwa jamii husika ila bado inaonekana kuwepo.

Wanasema pamoja na wanajamii kuwachukulia wanawake wanaocheza soka, wanafanya uhuni wao hawakujali hilo, maana nia walikuwa wanaijua wenyewe.

Wachezaji hao wanatumia fursa ya vipaji vyao kuhakikisha wanaingiza kipato na kuhudumia familia zao, kujiajiri na kufanya mambo mengine ya kimaendeleo  kutokana na kipato wanachopata kupitia vipaji vyao.

Mmoja wa muanzilishi wa timu hiyo ambae sasa ni kocha wa timu hiyo ya Mkoani Qunes Ramla Juma Khamis, anasema soka la wanawake kwa sasa, limekuwa ni tofauti na pale zamani, ambapo jamii ilikuwa inasema kujishirikisha katika michezo kwa watoto wa kike ni uhuni.

‘Nakumbuka wakati naanza kuchezesha timu hii, nilibezwa na jamii mimi na wenzangu, hadi kuambiwa mchezo wa mpira wa miguu kwa watoto wa kike, hakuna mafanikio, tuliambiwa mengi lakini leo hii faida tujionea,’’anasema.

Wazazi walitaka nishughulikie masomo tu na hawakutaka kusikia kwa mtoto wa kike, kucheza mpira wa miguu ingawa sikukata tamaa.

“Sasa nimekuwa  kocha wa timu hii ya Mkoani Qunes, ambapo najipatia riziki kupitia michezo ni jambo la kujivunia”anasema.

WACHEZAJI WANASEMAJE

Tatu Mohamed Ngwali ambae ni mchezaji wa timu hiyo anasema, hamasa kwenye soka la wanawake imeanza kuonekana ushahidi wa hilo nipale timu yao inavyoendelea kuwepo tokea ilipoanza.

Kupitia timu hiyo, tayari ameshapata mafunzo mbalimbali yanayohusiana na mchezo huo, ambapo kwa sasa anajiamini kuucheza popote.

“Kusema kweli tunahitaji pongezi hadi tulipofikia kwani hatukufikiria kama timu yetu hii ingeweza kudumu tulikuwa na chanagamoto kubwa kwa jamii ya Mkoani,’’anaeleza.

 Hamida Juma Amani, anasema pamoja na gumzo kubwa kuanzishwa timu ya wanawake Mkoani na kufanikiwa kuwepo, bado kuna chanagamoto ya timu ya wanawake kucheza ligi.

Anaona kumekuwa na mabadiliko kwa jamii, kuhusiana na mchezo huo kwa wanawake kwani ni tofauti na zamani sasa wanacheza kwa amani.

“Tunalolihitaji ni usawa wa kijinsia kwenye michezo lakini, ili usawa huo uweze kupatikana ni lazima serikali, itusaidie lakini na jamii ipate elimu ya kutosha”,alisema.

Riziki Ali Khamis ambae alipata nafasi ya kushiriki kuchezea timu ya taifa ya Zanzibar, anasema wanawake wanaweza kucheza mpira wa miguu sawa na wanaume, hakuna haja ya kubaguliwa.

Anasema kipaji cha michezo kwa watoto wa kike ni vyema vikaendelezwa, kwani huwezi kujuwa ni wapi ndiko kutakakomg’arisha maisha yake.



Kuwepo kwa timu moja kwa wilaya ya Mkoani, inawaweka katika hali ngumu, kwani inabidi wacheze na wanaume chini ya miaka kati ya 15,17 na18.

Pamoja na kuwa na ufinyu wa kucheza kirafiki timu hiyo haijawahi kuwa ya mwisho, pale wanapocheza ligi ambapo wachezaji hao wanasema timu ambayo imewahi kuwapa vikwazo ni timu ya New generation, iliwahi kuwafunga mabao 3 ila nao walichungulia goli lao kwa kuingiza wavuni goli moja.

Timu hiyo imekuwa ikipata shida hasa pale inapopata mwaliko ama inapofika wakati wa kuchezaligi kwani imekuwa na uhaba wa wafadhili.

Na ndio maana timu hiyo kwa mwaka 2024/2025 ikashindwa kushiriki ligi kuu ya soka la wanawake Zanzibar, kwani ndio inajitegemea wenyewe kujiendesha.

“Kwenye ligi kunahitaji kula, malazi, nauli ingawa niliomba lakini sikufanikiwa kubahatika, kwani hatuna wafadhili huwa natowa fedha zangu mkononi kuendeleza timu,”anasema kocha.

Wakitaja mafanikio katika timu yao kocha Ramla, anasema pamoja nakuitambulisha jamii kama timu ipo lakini ni kujiunga na timu ya taifa, kupata ajira kwa vijana wanne serikalini.

 Mengine ni kutowa vijana wawili kwenda Tanzania bara kwa kucheza mpira wa miguu katika timu za huko, kupata mafunzo ya mpira wa miguu kupitia ZFF na kujiunga na timu ya taifa ya Zanzibar.



MATARAJIO YAO NI YEPI

Wachezaji wanasema ni kuendeleza timu ili kuweza kufikia mbali kimichezo na kujipanga kwa msimu unaofata, kuunganisha watoto kujiepusha na vishawishi ambavyo vimeikumba jamii.

Matarajio ya timu hii inakwenda sambamba na malengo ya mradi wa michezo kwa maendeleo  wa kuongeza ushiriki kwa wanawake  na watoto wa kike, ambao unatekelezwa na jumuiya ya wanasheria wanawake Zanzibar ZAFELA, kituo cha mijadiliono kwa vijana CYD, pamoja na TAMWA Zanzibar kwa ufadhili wa shirika la maendeleo la Ujerumani.

Katika kuhakikisha timu hiyo inasonga mbele, ni jukumu la viongozi wa Wilaya, Mkoa taasisi za maendeleo wajitokeze kusaidia ili kuhakikisha inasonga mbele na isibaki nyuma .

ZFF

Mwenyekiti wa chama cha mpira wa miguu ZFF Mkoa wa Kusini Pemba Nassor Hakim anasema ingawa kuna chanagamoto kubwa ya fedha kusimamia ligi za wanawake  katika Wilaya na Mikoa.

Inasema husaidia timu hiyo pale panapotokezea ruzuku ndogo ndogo hata kuwaombea kwa wafadhili na wahisani.

Kwa vile huwa ni bahati nasibu kupata pale wanapoombewa na ndio hufika mahala wakakosa na wao huwalazimu kusaidia kutoka mikononi mwao ili mambo yaende sawa.

“Kutokana na hilo sasa ZFF iwe ni chombo kikuu kutowa motisha kwa vilabu vya wilaya kwani wao wanapata ruzuku kutoka sehemu mbalimbali ikiwemo PBZ, FIFA, CAF na kwenginejambo amabalo sisi wilaya na mikoa tunazikosa”alisema.

TAMWA INASEMAJE?



Afisa mradi wa kukuza usawa wa kijinsia na ujumuishi kwenye michezo unaofadhiliwa na shirika la maendeleo  la kimataifa la Ujerumani Khairat Haji,  anasema kila mtu anayo haki ya kushiriki katika michezo na hakuna sababu ya  wanawake kubakia nyuma.

Ndio maana anasema kupitia mradi huo TAMWA Zanzibar itahakikisha usawa wa kijinsia, unapatikana katika michezo ya aina mbali mbali.



Pamoja na kuwa  wanawake wako nyuma katika ushiriki wa michezo, aliwataka wasirudi nyuma na washiriki kwa hali ya kuridhisha.

Kubwa zaidi anasema pamoja na kucheza huko, ni vyema wakazingatia mavazi ya stara, kama inavyoelekeza kanuni kwamba watoto wa kike wavae nguo za heshima.

Ni jukumu la wazazi sasa katika jamii ya Mkoani na nyingine kutokuwa na wasiwasi ya kuwa mchezo huo ni uhuni hasa ukizingatia wadada hao huvaa treki na flana na vishungi wala hawavai bukta tupu.

                 mwisho

 

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan