Skip to main content

KAMATI KITAIFA 'GEF' YAZITAKA TAASISI ZA UWEZESHAJI WANANCHI KUTATUA VIKWAZO UFIKIAJI USAWA KIUCHUMI

 

NA MWANDISHI WETU, ZANZIBAR @@@@

KAMATI ya Kitaifa ya Ushauri kuhusu utekelezaji wa Programu ya Kizazi chenye usawa, imezitaka taasisi zinazohusika na uwezeshaji wananchi kiuchumi kuweka mkakati wa kuungana kufanya kazi kwa pamoja, ili kuzitafutia ufumbuzi changamoto zinazokwaza ufikiaji wa haki na usawa wa kiuchumi kwa wanawake.

Wito huo umetolewa kufuatia ziara ya wajumbe wa kamati, yenye lengo la kufuatilia utekelezaji wa Programu hiyo Zanzibar kubaini kuwepo kwa baadhi ya changamoto zinazowakwaza wanawake kupata haki na usawa wa kiuchumi.



Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni Naibu Spika wa Baraza la wawakilishi Zanzibar, Mhe. Mgeni Hassan Juma, alieleza licha ya wananchi hasa wanawake kuonesha utayari wa kujishughulisha na shughuli za kiuchumi hasa kilimo cha mwani lakini wanakabiliwa na vikwazo vingi vinavyowakatisha tamaa zaidi.

Alibainisha kutokana na changamoto hizo kugusa sekta mbalimbali ni muhimu  taasisi husika kama Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Zanzibar (ZEEA), Uchumi wa Buluu na nyingine zote kuweka mashirikiano ya kwenda kwa pamoja kutatua changamoto hizo  ili lengo la haki na usawa wa kiuchumi lifikiwe.

"Kuwe na mashirikiano ya kitaasisi kwa kufika chini ngazi ya halmashauri huko, hii itatusaidia kuwafikia wananchi wengi zaidi na kuwawezesha katika masuala mbalimbali kwenye  kujenga kizazi chenye  usawa wa kiuchumi," alieleza Mhe. Mgeni.

Aliongeza, “huko akinamama wengi tumeona wana shida nyingi za bei, kibiashara na mazingira magumu hasa wakulima wa mwani lakini ukiwaona wana moyo na wanahitaji sana kufanya shughuli hizo,” alieleza Mhe Mgeni.

Kwa upande wake Dkt. Monica Mhoja, mjumbe wa kamati hiyo alishauri serikali na wadau kuweka kipaumbele cha kutoa elimu kwa wanawake kutambua haki zao na kuchukua hatua sitahiki pale zinapokandamizwa.



"Tuweke mkakati wa kutoa elimu ya utambuzi wa masuala ya kisheria kwa wanawake katika kila eneo ili waweze kutambua haki zao na namna gani wanapaswa kufanya ili kupata haki hizo,” alieleza Dr. Mhoja.

Katika kukabiliana na changamoto hizo, Najma Hussein Abdallah, alishauri taasisi za uwezeshaji wananchi kuwa na utaratibu wa kufanya utafiti ili kubaini mahitaji ya wananchi na kutafuta mbinu sahihi za kusaidia kutatua changamoto hizo.

Alieleza, " tunatakiwa kufanya utafiti wa kina kutambua wakulima wote wa mwani walipo ili kutusaidia kujua namna gani tunaweza kuwafikia wote na kuwasaidia kutatua changamoto zinazowakabili. Hatuwezi kwenda kama bado hatujaitambua hali halisi ya wakulima.”

Katibu Mkuu Wizara ya Uchumi wa Buluu, Cpt. Hamad Bakar Hamad alipogeza kamati hiyo kubaini uwepo wa changamoto hizo na kuahidi kushirikiana na taasisi zote ili kuhakikisha sekta ya uchumi wa buluu na uwezeshaji wananchi kiuchumi inakuza uchumi wa wananchi hasa wanawake ambao ndio wadau wakubwa wa kilimo cha mwani Zanzibar.

Alikiri licha ya juhudi kubwa zinazochukuliwa na taasisi mbalimbali kukuza uwezeshaji wananchi kuchumi kwenye sekta tofauti, changamoto kubwa iliyopo ni kukosekana mashirikiano ya kisekta na kupelekea kila taasisi kufanya kivyake.



Alisema, "Cordination ya kusimamia uchumi wa buluu haitaishia hapa Zanzibar tu, tutakaa na wenzetu Bara kwani wakulima wa mwani wanaoathirika sio wa Zanzibar tu hata wa bara kukitokea changamoto kwenye bahari nao wanaathirika, hivyo lazima tukae pamoja tuone namna gani tunaweza kushirikiana kutatua changamoto hizo.”

Kamati hiyo ya kitaifa inaendelea na ziara Zanzibar inayolenga kufuatilia utekelezaji wa Programu hiyo na jitihada za kukuza haki na usawa wa kiuchumi kwa wanawake nchini.
MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan