NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@
UONGOZI
wa skuli ya sekondari ya Fidel Castro, wananchi kijijini hapo, pamoja na
uongozi wa shehia ya Wawi wilaya ya Chake chake, umekubaliana kupiga marufuku
kuanzia sasa, kutoingia kwa mtu yeyote bila ya kazi ya halali, ndani ya eneo la skuli, ili kuepusha
athari ambazo zimeanza kujitokeza.
Wakizungumza
kwenye kikao cha pamoja, kilichofanyika skulini hapo, walisema tayari athari
kama za wizi wa vifaa vya wanafunzi, umeanza kujitokeza, hivyo wamekubaliana kuanzia
sasa kupiga marufuku, uingiaji kiholela.
Mwalimu mkuu
wa skuli hiyo Seif Hamad, alisema ameridhishwa na uamuzi uliofikiwa na pande
mbili hizo, kwani wamekuwa na hofu kubwa ya kutokezea vitendo vya udhalilishaji
hapo baadae.
Alieleza kuwa,
uamuzi huo unaweza kusaidia sana kuondosha uingiaji holela ndani ya skuli hiyo,
ambao kwa kiasi kikubwa, ulikuwa unaanza kutishia hata mali za skuli.
āāMimi nimeridhishwa na uamuzi ambao umefikiwa kati yetu, wazazi na uongozi wa shehia, kwamba sasa tuwazuie watu wote kuingia kiholela eneo la skuli,āāalieleza.

Katika hatua
nyingine Mwalimu mkuu huyo, alisema jambo jingine ambalo limeanza kuwa tatizo,
ni wafugaji sasa kukaribisha mifugo yao karibu na majengo ya skuli.
āāKwa mfano
tulikuwa tumekubaliana kwamba, nje ya eneo la skuli wafunge mifugo yao, lakini
sasa fursa hiyo inaonekana kutumiwa vibaya, maana mpaka maeneo ambayo wanafunzi
wanakaa na kujisomea, wanaishi na mifugo,āāalilamika.
Hata hivyo Mwalimu
mkuu huyo, alisema bado hakuna marufuku kwa wanafunzi wa nje ya skuli hiyo,
wanaotaka usaidizi wa wenzao wanakaribishwa.
āāUtaratibu
ni ule ule wa zamani, mzazi anafika kwa uongozi wa skuli na anajaza fomu maalum
na anakabidhiwa mwanafunzi mwenzake kwa utaratibu na anasaidiwa,āāalieleza.
Mapema sheha
wa shehia ya Wawi Sharifa Abdalla Waziri, alisema uamuzi huo wa kupiga marufuku,
sio wa waalimu pekee bali ni makubaliano pande zote.
āāSisi
wananchi tunaoishi pembezoni mwa skuli ya Fidel Castro, uongozi wa shehia na
uongozi wa skuli, tumekubaliana hili kwa pamoja na niletu sote,āāalieleza.
Aidha sheha
huyo, aliutaka uongozi wa skuli hiyo kuhakikisha unakaa na wananchi wa shehia
jirani ya Vitongoji, kwani wapo baadhi ya watoto hupendelea kuingia ndani ya eneo
hilo.
āāInawezekana
sio watoto wa shehia ya Wawi pekee wala wafugaji, lakini hata shehia jirani ya
Vitongoji, sasa baada ya kikao hichi, nao muwaite ili kuwapa ushauri,āāalieleza.
Mapema msadizi
wa sheha wa kijiji cha Fidel Castro Fatma Jaffari, alisema wazazi na walezi,
ndio wenye jukumu kubwa la kuwazuia watoto wao kutoingia kiholela eneo la
skuli.
Alieleza kuwa,
kwa vile utaratibu upo, ni vyema ukafuatwa ukiwemo kuonana na waalimu kabla ya
kuanza kufanya jambo lolote, ili kuepusha uharibifu skulini hapo.
Akizungumza kwenye
kikao hicho, Msaidizi wa sheria shehia ya Wawi Fatma Hilali Salim, aliwashauri
wazazi na walezi katika eneo hilo, kuwa walinzi wa mwanzo kwa skuli hiyo.
āāWananchi
wanaoishi hapa Fidel Castro, muwe walinzi wa mwanzo kabla ya watu wengine,
kwani uharibifu unapotokezea nyinyi mnaona kwa haraka, kuliko aliyeko nje ya
hapa,āāalishauri.
Mwananchi Haji
Mohamed Hamad, alisema wamefurahishwa na uongozi wa skuli kuwashirikisha katika
kuzuia athari zaidi skulini hapo.
Asha Khamis
alisema, jukumu la kuzuia watoto kutoingia kiholela skuli hapo, ni lao kama
wazazi na kisha uongozi wa skuli ni kupiga marufuku kwa kuweka mabango.
Wakati huo
huo, uongozi wa skuli hiyo umewataka wafanyabiashara wa aina mbali mbali,
kwanza kusitisha uuzaji wa bidhaa zao pembezoni mwa skuli hiyo, hadi taarifa
nyingine itakapotolewa.
Mwisho
Comments
Post a Comment