Skip to main content

'CONNECTING CONTINENT' YAWAONESHA NJIA WAZAZI KUONGEZA UFAULU

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

UONGOZI wa skuli ya sekondari ya Connecting Continent iliyopo Mgogoni wilaya ya Chake chake, umesema kama wazazi na walezi wataongeza ushirikiano, kati yao na waalimu, uwezekano wa kuondoa daraja la nne na la tatu kwa kidato cha nne upo.

Mwalimu mkuu skulini hapo, Mwache Juma Abdalla, alisema waalimu wanaosomesha skuli hiyo, wamekuwa na moyo mmoja wa kuondoa daraja la nne na la tatu kwa wanafunzi wa kidato cha nne, hasa kwa mitihani ya taifa.

Alisema, hilo linaweza kuwa rahisi mno, ikiwa kuanzia sasa  wazazi na walezi, watajenga msingi madhubuti ya ushirikiano kati yao na waalimu, skulini hapo.

Alieleza kuwa, wapo wazazi na walezi, hawapiti skulini hapo jambo ambalo linalowapa ukakasi waalimu na kuhisi wameachiwa majukumu peke yao ya ulezi.

Mwalimu mkuu huyo, aliyasema hayo Julai 6, 20204 kwenye kikao cha kwanza kwa mwaka huu, cha kuwasilisha matokeo ya muhula wa kwanza kwa wanafunzi wa kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne.

Alifahamisha kuwa, kimsingi matokeo hayo kwa muhula huu, sio mazuri ingawa siyo mabaya ya kuvunja moyo, ingawa kitu cha kuzingatia ni kwa wazazi kuongeza juhudi za kufuatilia masomo ya watoto wao.

‘’Leo (jana) tumewasilisha matokeo haya ya majaribio kwa muhula wa kwanza, lakini ufaulu wetu umeshuka, ikilinganishwa na miaka mingine,''alifafanua.



Katika hatua nyingine, Mwalimu huyo mkuu Mwache Juma Abdalla, aliwataka wanafunzi kushughulikia zaidi masomo yao, kuliko jambo jingine, lolote.

‘’Muelewe kuwa wazazi na walezi wenu, wanawekeza rasilimali kubwa kwenu na wakati mwingine wanajinyima kwa ajili yenu, sasa acheni anasa na msome kwa bidii,’’alifafanua.

Mapema Mjumbe wa bodi ya wazazi ya skuli hiyo Omar Mjaka Ali, alisema kama juhudi za waalimu hazikuungwa mkono na wazazi, kusitarajiwe kupanda kwa ufaulu.

Hata hivyo, amesifu mbinu, juhudi, mikakati na dira zinazofanywa na waalimu skuli hapo, katika kukuza uwelewa na ufaulu kwa wanafunzi.

Mwalimu Nassor Mohamed Omar wa skuli hiyo, aliwakumbusha wazazi na walezi, kuwa wasiishie kwenye huduma za chakula, mavazi na kulipa ada pekee, bali wawe karibu na watoto wao.

Mwalimu Haji Othman Haji, alisema jambo moja ambalo linawapa mshangao ni baadhi ya wazazi kujilimbikiza ada, kwa zaidi ya miezi sita, na kisha kupuuza kufanya malipo.



Akiwasilisha muhutasari wa matokeo hayo, Mwalimu Fadhila Rashid Khamis alisema, ufaulu kwa mitihani hayo ya majaribio, kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne, sio mazuri sana.

Alisema, kwa mfano kati ya wanafunzi 82 wa kidato cha nne, waliofaulu ni 16, ambapo kati yao wanawake ni tisa na wanaume saba, sawa na asilimia 19.5 ya wanafunzi wote.

‘’Hili darasa mwishoni mwa mwaka huu, wataingia kwenye mitihani ya taifa, lakini haya ya kuwapima hali hairidhishi, lazima tuendelee kushirikiana kati yetu,’’alifafanua.

Baadhi ya wazazi wa wanafunzi hao, walisema mkazo uwekwe ili somo la kiingereza, kama msingi wa masomo mingine lifahamike kwa upana.





Mzazi Nassor Kai, aliwashauri waalimu kuendelea kubuni mbinu na mikakati endelevu, ili kukabiliana na wanafunzi wavivu na wasiopenda kazi.

Subira Suleiman, aliwataka wazazi wenzake, kupunguza mapenzi ya kupitiliza kwa watoto wao, na kuwasimamia kwa dhati, ili kuhakikishan wanatimiza malengo yao.

Ali Salim Ali, aliwashauri waaalimu, kuweka majaribio kila kipindi, ili wanafunzi hao kupima uwezo wao pamoja na kutoka woga mitihani, jambo ambalo huchukua nafasi kubwa ya kufeli.

Wanafunzi 82 wakiwemo wanawake 52 na wanaume 30 wanataeajiwa kufanya mitihani yao ya taifa ya kidato cha nne mwaka huu skulini hapo.

                            Mwisho


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan