Skip to main content

DODO PUJINI WATOA RAI KUMALIZA UDHALILISHAJI

 


 NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANANCHI wa shehia ya Dodo wilaya ya Mkoani Pemba, wamesema njia moja ya kupunguza matendo ya udhalilishaji ndani ya jamii, ni wakati sasa kwa sheria kubadilishwa, ili mwanamke naye aliyechangia kutokea kwa tendo hilo, atiwe hatiani.

Walisema, wapo wanawake wameshasababisha kufungwa kwa wanaume wengi, nae akiendelea na shughuli zake mtaani, jambo ambalo linaweza kuwapoteza wanaume hapo baadae.

Wananchi hao, waliyasema hayo leo Juni 24, 2024 Dodo Pujini, wakati wa mkutano, ulioandaliwa na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, kwa kushirikiana na Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka, kwa ufadhili wa ‘UNDP’ kupitia mradi wake wa upatikanaji haki Zanzibar.

Walisema, bado makosa ya ubakaji yanawaelekea wanaume pekee, hata kama mwanamke mwenye umri unaopindukia miaka 18, nae alichangia kwa njia moja ama nyingine.

Haji Shaibu Hamad miaka (70), alisema ubakaji ambao uko wazi ni ule wa mwanamme kumtumia nguvu mwanamke, lakini ule wa kuridhiana ni vyema sheria ikawaangalia wote.

‘’Mwanamke anatoka Wete zaidi ya kilomita 40 anamfuata mwanamme Pujini, kisha wanapokosana kibei, huchukuliwa mmoja na mwanamke kuachwa, hapa hatutofika,’’alifafanua.



Nae Tatu Juma Othman (60), alisema kama wanawake nao hawakutiwa hatiani kwa ubakaji, makosa hayo yataendelea kutoka siku hadi siku.



‘’Kama ni mtoto wa kike, au mwanamke amebakwa kwa nguvu, au ameleweshwa ni kesi nyingine, lakini kwa hawa wanaokubaliana, na kisha mwanamke kugeuza kibao, wanaume wote wataishia kufungwa,’’alilalamika.

Kwa upande wake Sahiya Abdalla Khamis (50), alieleza kuwa, wapo wanawake wamekuwa wakitengeneza mazingira ya kujipatia fedha kiholela, akisingizia kubakwa.



Nae Juma Ali Juma, alisema bado tafsiri ya maana ya ubakaji, haijaeleweka vyema ndani ya jamii, na ndio maana, walioko chuo cha mafunzo wengi ni wanaume.

Mwananchi Ambari Khamis Ambari na mwenzake Adam Said Omar, walisema kama kwenye vituo vya mapunziko vya askari na Jeshi ‘mesi’ havikuwekewa udhibiti, vinaweza kuchangia kutokea kw amatendo hayo.





Akizungumza kwenye mkutano huo, Mwanasheria wa serikali Mohamed Ali Juma, alisema wazo la mwanamke nae kutiwa hatiani, linahitaji marekebisho ya sheria.

Alieleza kua, njia nyingine ya kutokomeza matendo hayo, ni wananchi kufika mahkamani na kutoa ushahidi wao.

‘’Hakuna hatia katika kesi yoyote pasi na sisi wananchi kutofika mahkamani kutoa ushahidi, na zipo kesi kadhaa zimeshafutwa kwa changamoto hiyo,’’alieleza.

Nae Mwanasheria wa serikali Mussa Ali Khamis, alisema kwa eneo kubwa kisheria, mwanamme ndio anayeingia kwenye kosa la ubakaji.


‘’Kisheria mwanamme ndie anaebaka, maana hicho cha kubakia anacho, ingawa mwanamke anaingia, ikiwa amechangia tendo la ubakaji kutokea, kwa mfano kutoa nyumba yake,’’alifafanua.

Mapema Mkuu wa Divisheni ya Katiba na Msaada wa Kisheria Pemba, Bakar Omar Ali alisema, mkutano huo ni kwa ajili ya wananchi, kutoa maoni yao.




‘’Wananchi leo, tumekuja kukutana na nyinyi, mtueleze ni kifanyike ili kuondoa matendo ya udhalilishaji, na pale yanapotokezea ni kuyaripoti,’’alifafanua.

Akifungua mkutano huo, Naibu sheha wa Dodo Abdalla Mkubwa Mohamed, alipongeza hatua ya taasisi hizo, kuichangua shehia yake, kupewa elimu hiyo.




Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria kwa kushirikiana na Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka  kwa ufadhiliwa UNDP inaendelea na mikutano ya wazi kwa wananchi, ili kuwahamasisha kutoa ushahidi na kuyaripoti matendo ya udhalilishaji.

Tayari wananchi wa shehia Ukutini, Dodo wilaya ya Mkoani wameshafikiwa, na kesho Julai 25, itakuwa ni zamu ya wananchi wa Gando wilaya ya Wete na Micheweni.

                             Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan