Skip to main content

IDARA YA KATIBA: ''WANAWAKE MSIOGOPE TALAKA TOWENI USHAHIDI MAHKAMANI'

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

IDARA ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar, imewataka wanawake wa Junguni wilaya ya Wete, kutoacha kuzisimamia kasi za udhalilishaji hata kama mtendaji ni muume wake, kwa hofu ya kutishiwa talaka.

Kauli hiyo imetolewa leo Julai 25, 2024 na Afisa sheria kutoka Idara hiyo Ali Haji Hassan, wakati akizungumza na wananchi wa shehia ya Junguni wilaya ya Wete, kwenye muendelezo wa mikutano ya wazi, ya kuihamasisha jamii, kutoa ushahidi na kuziripoti za kesi za udhalilishaji, ulioandaliwa kwa ushirikiano na Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar.

Alisema, kama muume amebainika kwa kosa ubakaji, mwanamke lazima ashirikiane na vyombo vya sheria na kuondoa hofu ya talaka, ikiwa ni njia moja wapo ya kutokomeza matendo hayo.

‘’Hakuna hatia pasi na mwananchi kufika mahkamani kutoa ushahidi, sasa niwaombe wanandoa, wasiogope kuachika na wasimamie haki ya mtoto mahkamani,’’alishauri.

Katika hatua nyingine, Afisa huyo sheria, alisema bado jamii haijakuwa tayari katika mapambani hayo, kwani bado zipo familia, wanazifanyia sulhu kesi hizo.



Katika eneo jingine, alisema rushwa muhali imekuwa ikitawala ndani ya jamii, hasa ikitokezea anayeshutumiwa kwa ubakaji ni mwalimu wa madrassa, sheikh wa mtaani au mtu maarufu.



Kwa upande wake, Mwanasheria wa serikali Shaame Farhan Khamis, alielezea kusikitishwa na wananchi wanaoiandikia barua Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka kutaka kufutisha kesi za udhalilishaji.

Aidha aliwaeleza wananchi hao kuwa, hadi sasa sheria nambari 6 ya mwaka 2011, inaendelea kumtambua mtoto kuwa, ni mtu yeyote aliyechini ya umri wa miaka 18.



‘’Hivyo mwenye miaka 15, 16 na hata 17 hata kama atamfuata mwanamke masafa marefu, likitokezea tendo la kukutana kimwili, huhesabika ni ubakaji,’’alifafanu.

Kwa upande wake Mwanasheria wa serikali kutoka Afisi hiyo Rahima Kheir Iddi, alisema jamii ndio pekee, iliyona nafasi kubwa ya kutokomeza matendo hayo.

Alieleza kuwa, njia moja ni kufika mahakamani kutoa ushahidi, pili ni kuanzisha ulinzi dhidi ya watoto pamoja na kuwafichua waliotenda jinai hiyo.



Akifungua mkutano huo, sheha wa Junguni Hamad Yahya Hussein, alisema fursa hiyo ni vyema wananchi wakaitumia, ili kutoa maoni yao.

Mwananchi Hassan Kombo Khamis, alisema bado adhabu iliyoandikwa kwenye vitabu vya sheria, ni ndogo wanayopewa washatakiwa.



‘’Adhabu iliyotajwa ni kuanzia miaka 30 hadi chuo cha mafunzo maisha, lakini bado mahkama wanawafungwa washtakiwa miaka 15 au 20, jambo linalochangia, kuendelea kwa matendo hayo,’’alifafanua.

Nae Mafunda Hamad Saleh, alieleza kuwa kama jamii haikukubali kuyarejesha malezi ya pamoja, suala la udhalilishaji linaweza kuchelewa kupungua ndani ya jamii.



Mzazi Mmaka Hamad Nassor alisema, vyombo vya habari na hasa mitandao ya kijamii, kama picha chafu hazikudhibitiwa, mmong’onyoko wa maadili utaendelea.

‘’Jingine linalokwamisha matendo hayo kutopungua, ni uwepo wa harufu ya rushwa katika vyombo  vya sheria, jambo linalorejesha nyuma, mapambano hayo.



Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar kwa kushirikiana na Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka kwa ufadhili wa UNDP, imekamilisha mikutano ya wazi katika shehia za Ukutini, Dodo, Junguni na Micheweni kisiwani Pemba.

                                               Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan