Skip to main content

BARAZA LA WATOTO WAWI, LAKERWA ADHABU NYEPESI KWA WABAKAJI

 

 
NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

BARAZA la watoto la shehia ya Wawi wilaya ya Chake chake, limesema bado hawaridhishwi na hukumu nyepesi zinatolewa mahakamani, kwa washtakiwa wanaowabaka watoto na wanawake.

Walisema, bado hukumu zinazotolewa na mahakma maalum za kupambana na udhalilishaji, zinawafaidisha wabakaji, jambo ambalo, linatishia kuendelea kwa matendo hayo.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi shehiani hapo, walisema, Baraza la Wawakilishi mwaka 2018, lilipitisha sheria kali kwa watakaotiwa hatiani kwa udhalilishaji, ingawa bado mahakimu hawaitumii ipasavyo.

Walisema, wamesomeshwa kuwa, mahkama ikimtia hatiani mshitakiwa kwa makosa ya ukatili na udhalilishaji, adhabu yake ni kuanzia kifungo kisichopungua miaka 30 au maisha, ingawa hakuna aliyetekelezewa adhabu hiyo.

Mjumbe wa baraza hilo Aisha Mohamed Juma, aliema anashangaa kuona washtakiwa wanafungwa miaka kati ya 10 au 15 tu, jambo ambalo anashindwa kuwaelewa mahakimu.

Alieleza kuwa, hajaona wapi mahakimu na majaji hao, wanapita na kutafsiri na kuacha kuwafunga washtakiwa kifungo cha kuanzia miaka 30 au maisha, na badala yake hutoa raia nyingine.

‘’Kama sheria imeshapitishwa kwamba, atakaetiwa hatiani afungwe kuanzia miaka 30, nini kinawatia hofu mahakimu na majaji wetu,’’alihoji.

Nae mjumbe wa baraza hilo Omar Haji Omar alisema, serikali kwa upande wake, imeshaongeza adhabu kwa wabakaji, ili kukomesha vitendo hivyo, ingawa bado kuna ukakasi wa sheria kutumika.



‘’Kama Majaji wanatafsiri nyingine ya sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018 kwenye vifungu vyake ya 108 na 109 watueleze, ili tuilalamikie tena serikali, kinyume chake watekeleza kama ilivyo,’’alifafanua.

Mratibu wa wanawake na watoto ambae ni Mratibu wa baraza la watoto shehia ya Wawi Fatama Kassim Mohamed, alisema watoto, wamekuwa wakihoji katika mkutano mbali mbali, juu ya adhabu nyepesi zinazotolewa mahakamani.

 


‘’Tulipiga kelele kwa muda mrefu, juu ya marekebisho ya sheria, kwamba ziongezewe makali, lakini sasa zimeshaongezewa, hatuoni matunda yake,’’alilalamika.

 

Nae Mwenyekiti wa baraza hilo Abuu-bakar Massoud Juma, alisema kama sheria haikutumika kama ilivyo, watoto wataendelea kudhalilishwa hapa Zanzibar.

 

‘’Tulitarajia kuwa, kuanzia mwaka 2018 baada ya sheria mpya kupita, wabakaji wataingia woga, kwani sheria hiyo ni kali, lakini cha kushangaaza wanafungwa miaka 10 au 15 na sio 30 kama sheria ilivyo.



 

Msaidizi wa sheria wa shehiya ya Wawi Fatma Hilali Salim, alisema kua, wimbi la ubakaji, lilionekana kubwa hapo zamani na kukaandaliwa mipango kadhaa, ikiwemo kurekebishwa sheria, ili kupunguza matendo hayo.

 

‘’Ni kweli huskii kutokana mahkamani kuwa, kuna mshtakiwa amefungwa maisha au kifungo kisichopungua miaka 30, kama sheria ilivyo, hili ni tatizo upande mmoja,’’alieleza.

 


Akizungumza kwenye moja ya makongamano ya kupinga ukatili na udhalilishaji, Hakimu wa mahakma maalum ya kupinga udhalilishaji Mkoa wa kaskazini Pemba, Muumini Ali Juma, alikiri kuwepo wa tasfsiri tofauti.

 

Alisema, mahakimu wamepewa nguvu kisheria, baada ya kufungwa kwa ushahidi na kumalizika utetezi, kuangalia ukubwa wa adhabu, kwa mashtakiwa.

 

Alifahamisha kuwa, sheria huja kama muongozo wa kutoa adhabu na inaweza isilingane baina ya mshatikiwa mmoja na mwingine, hata kama kosa ni la aina moja.

 

‘’Mahakimu na Majaji ipo sheria yetu inayotuongoza, ambayo imetuwekea utaratibu wa kuendesha mashauri hadi utoaji wa adhabu, katika mahakma husika,’’alifafanua.

 

Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Zanzibar Siti Abassa Ali, amewataka watoto kuendelea kuwaibua wanaotaka kuwadhilishaji, ili sheria ichukue mkondo wake.

 

Mratibu wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said, alisema adhabu ndogo zinazotolewa, ni chanzo cha kuongezeka kwa matendo hayo.

 

Juni 13, mwaka jana mahkama ya Mkoa Wete ilimuhukumu mshitakiwa Ali Sharif Ali, wa Pandani, kutumikia chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka 20, baada ya kupatikana na hatia ya kumlawiti mtoto mwenye miaka 15.

Aidha Disemba mwaka 2022, mshatakiwa Said Abdalla Issa, wa Chanjamjawiri na Kengeja, alifungwa miaka saba, baada ya, kukutwa na hatia ya kumbaka mtoto wake wa kulea mwenye miaka 14.

Mahakama maalum ya kupambana na makosa ya udhalilishaji Mkoa wa kusini Pemba, Disemba 2m mwaka 2022, limswekwa chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka 10, mshitakiwa Khamis Juma Chumu ‘soda’ (76) wa Mtoni Chake Chake, baada ya kukutwa na hatia ya kumbaka mtoto wa miaka 13.

                       MWISHO

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan