Skip to main content

WANANCHI SHUNGI: 'MAJI YA ZAWA ''BUL BUL'

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANANCHI wa shehia ya Shungi wilaya ya Chake chake Pemba, wamesema kwa muda mrefu sasa, hawana shida tena ya huduma ya maji safi na salama, kufuatia urekebishaji mkubwa uliofanywa na Mamlaka ya Maji Zanzibar ZAWA, tawi la Pemba.

Walisema kwa sasa wanapata nafasi ya kujipangia muda wao wa shughuli za kilimo, biashara, wajasiriamali na wanaokwenda ofisini, baada ya kuwepo kwa huduma hiyo ya uhakika.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi shehiani hapo, walisema haijawahi kutokea, kwa mud mrefu kuwa na huduma hiyo kwa uhakika, ingawa sasa miaka karibu mitatu hawana wasi wasi.

Walisema, kuwa shughuli zao za kujitafutia huduma za chakula na safari nyingine sasa, zimekuwa zikipangika vyema, kwani hapo awali walikuwa wakisuumbuka kutokana na huduma hiyo.

Mmoja kati ya wananchi hao Asma Said Abdalla wa Chanjamjawiri, alisema kwa upande wake sasa, amepata utulivu wa kujipangia shughuli zake, kutokana na uwepo wa uhakika wa huduma yam aji safi na salama.

Nae Zulekha Nassor Hilali, alieleza kuwa hata kwa waliojipanga kuyatumia maji hayo kwa ajili ya kuendelea kilimo, wamekuwa na uhakika kwa sasa.



Kwa upande wao wananchi wa kijiji cha Misooni, Mbarouk Idrissa Omar, Asha Suleiman Hamad na Amina Suleiman Juma, walisema hata kijijini kwao, kwa sasa huduma hiyo inafika.

Walieleza kuwa, baada ya kutoa kilio cha muda mrefu, hatimae ZAWA walirekebisha kisima chao kilichopo Matuleni na sasa huduma yam aji sio shida tena shehia mwao.

‘Kwa sasa tunafua na kutumia kwa shughuli nyingine maji hayo muda tuutakao, maana kama umeme upon a hakuna hitilafu kwenye kisima chetu, maji yanatoka saa 24,’’walisema.

Hata hivyo, waliishauri ZAWA kuangalia uwezekano wa kuwajengea minara ya tanki ya kuhifadhia maji hayo, ili umeme unapokatika au ikitokezea hitilafu mfano wa mashine kuharibika wawe na uhakika.

Sheha wa shehia ya Shungi Hamad Ramadhan Soud, alikiri kuwepo kwa huduma yam aji safi na salama saa 24, ambayo ilitokana na mikakati thabiti ya ZAWA, ya kukifanyia matengenezo kisima chao.

Alieleza kuwa, ni kweli wananchi walikuwa wakilalamikia kuzorota kwa huduma hiyo, ikiwemo kupatikana nyakati za usiku, au kutoka wiki mara moja, ingawa kwa sasa hali imebadilika.

‘’Ni kweli ndani ya shehia ya Shungi, hakuna kijiji ambacho kinamiundombinu ya huduma ya maji safi na salama na kisha kukosekana kwa huduma hii,’’alieleza.

Wakati huo huo sheha huyo, aliwataka wananchi kuwendelea kuwa walinzi wa miundombinu ya maji safi na salama, ili iendelee kuwanufaisha wao na vizazi vijavyo.

‘’Wananchi waelewe kuwa, wapo baadhi ya wananchi wingine kwenye shehia mbali mbali wanaililia huduma hiyo, sasa kama Shungi ipo wahakikishe wanaitunza ili iwe endelevu,’’alieleza.  

Mkuu wa Mtandao wa maji Pemba kutoka Mamlaka ya Maji Zanzibar ZAWA tawi la Pemba Juma Omar Khamis, alisema siri ya wananchi wa shehia hiyo na vijiji vyake kupata huduma kwa saa 24, ni kuwepo visima viwili kwa ajili yao.

Alisema wananchi hao wanapata lita 70,000 kwa saa moja, ambapo ni sawa la lita 1,680,000 kwa siku ambazo zinazalishwa kwenye visiwa viwili, huku kimoja kikizalisha lita 36,000 na chingine lita 17,000 kwa saa moja.

Hata hivyo alisema wanampango wa kuwajengea tanki maalum la kuhifadhi maji, ili inapotokezea hitilafu ya kuzimwa kwa umeme au kuharibika mashine huduma iendelee.

Shehia ya Shungi iliyopo wilaya ya Chake chake Jimbo la Chonga, inao wananchi 3,884 ambapo inaundwa na vijiji vya Missoni, Shungi, Kiziwani, Chanjamjawiri, inayomiundombinu ya elimu, afya na barabara.

                 Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch