Skip to main content

WAZIRI LEILA AWAPA KONGOLE WANAFUNZI NG'OMBENI 'A' MKOANI KWA UFAULU


NA SALIM HAMAD, PEMBA @@@@

 Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Leila Mohamed  Mussa amewapongeza wanafunzi wa Skuli ya Msingi  Ngo’mbeni  'A'  Wilaya ya Mkoani waliofulu vizuri  michepuo ya Darasa la saba waliofanya mitihani yao mwaka 2023.

Waziri Leila aliyasema  hayo huko Mkoani Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba, wakati akizungumza na Walimu,Wazazi na Wanafunzi  katika sherehe ya kuwapongeza wanafunzi  wa Skuli  hiyo waliofaulu michipuo na kuwa  Skuli ya kwanza  katika Mkoa wa Kusini Pemba.

 jumla ya wanafunzi 157  waliofanya Mitihani ya Darasa la saba katika Skuli ya Ng’ombeni (A) na katoa  michipuo 51 ambapo idadi hiyo imeifanya Skuli hiyo kuwa kwanza  kwa ufaulu kwa wanafunzi katika Mkoa wa Kusini Pemba.

Alisema haikuwa kazi rahisi waliofanya wanafunzi hao kwani walipitia mazito wakati wa masomo yao,hivyo hawanabubudi kuzidisha jitihada zaidi katika kuona wanafika mbali na kutimiza ndoto zao.

Alisema suala la kutafuta elimu ni jambo la msingi  ambalo Vijana wanapaswa kuendelea kupambana ili kuweza kujijengea msingi mwema wa maisha yao ya hapo baadae.



Alisema kumekuwa na  Changamoto kadhaa wanazokumbanazo wanafunzi  Mashuleni  ikiwa ni pamoja kufanyiwa Vitendo Vya Udhalilishaji na kupelekea baadhi yao kushindwa kutimiza malengo yao huku Wizara na Wadu wengine wakiendelea kupambana katika kupiga vita Vitendo hivyo.

‘’Ni wapongezeni sana wanafunzi mmefanya Vizuri kwa kuongeza kiwango Cha Ufaulu mmekuwa wa kwanza kwenye Mkoa wa Kusini Pemba ,bila shaka kwenye mafanikio kuna magumu mengi mmepitia ninacho waomba muendelee na jitihada zenu naamini mtaweza kufika mbali’’alisema Waziri Leila.

 Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Khatib Juma Mjaja alisema Mafanikio hayo yaliyopatikana yametokana na Mashirikiano ya  pamoja  kwa Walimu ,wanafunzi Wazee na Jeshi la Polisi Mkoa huo.

Alisema kabla ya wanafunzi hao kufanya mitihani yao kulikuwa na misako maalumu iliyofanywa na kamati za Skuli hiyo, Wazazi na Jeshi la Polisi katika kuwasaka wanafunzi waliotoroka Mashuleni na kufanikiwa kuwarudisha na katia yao ni miongoni mwa waliofau michipuo.



''Mafanikio haya yametokana na Mashirikiano ya Wadau Mbali Mbali ikiwemo Jeshi la Polisi tumekuwa tukipita kila kijiji katika Wilaya hii ya Mkoani kuwasaka watoro tukafanikiwa kuwarejesha lakini jambo la kufurahisha tumeambiwa miongoni mwa waliofaulu ni wale ambao tayari walishatoroka Mashuleni’’alisema Mjaja.

Mapema Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Aamali Pemba,Mohamed Naasor Salum  alimshukuru Mkuu wa Wilaya hiyo Khatib Juma Mjaja kwa juhudi alizozichukua kwa kushirikiana na kamati ya Skuli  hiyo na Jeshi la Pilisi kwa kupambana na watoto watoro jambo lililosababisha kupunguza idadi ya ziro kwenye Wilaya ya hiyo.

Akisoma risala katika hafla hiyo Maalim Mstaafu wa Skuli  hiyo Bi Mwanajuma Hassan Kaduara alisema  pamoja na matokeo hayo mazuri waliyoyapata lakini wanakabiliwa na changamoto mbalimbli katika Skuli hiyo ikiwemo   uhaba vikalio pamoja na vyumba Vya kusomea.



Katika hafla hiyo Waziri Leila aliwazawadia wanafunzi hao kwa Vifaa mbali mbali vya Masomo  ikiwemo mabuku pamoja na Fedha taslim ili kuwa ni mootisha kwa wanafunzi wengine.

MWISHO.

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch