Skip to main content

MIAKA MITATU YA DK. MWINYI PEMBA WAJENGEWA KIWANDA CHA USARIFU MWANI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

NOVEMBA 3 ya miaka mitatu iliyopita, ilikuwa ndio siku ya kwanza ya Rais mpendwa wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, kuwasili ndani ya Ikuklu ya Zanzibar.

Kwa wakati huo, hakuwasili akitokea nchi jirani..laaahasha alitokea kwenye viwanja alivyokula kiapo, kushika hatamu ya uongozi.

Maana Dk. Mwinyi, baada ya kumalizika kwa kampeni za zaina yake, zilizotajwa kama za kisayansi kwa kule kukutana na makundi mbali mbali, kisha wananchi walimpigia kura.

Baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa vyama vingi, Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ZEC, ilimtangaaza Dk. Mwinyi kuwa rais wa Zanzibar kwa kupata asilimia 76.27 na kuwaacha mbali wagombea wenzake.

‘’Nimepokea ushindi kwa mikono miwili na nawashukuru wananchi wa Zanzibar kwa kunichagua mimi na chama changu, kwa miaka mitano ijayo,’’alisema wakati huo.

Kwa wananchi Zanzibar, kama alivyosema Mwenyekiti wa CCM mkoa wa kaskazini Pemba Mberwa Hamad Mberwa, kuwa duniani viongozi kama aina ya Dk. Mwinyi ni wachache.

Maneno kama haya, yaliwahi kusemwa pia na Mbunge viti Maalum mkoani humo, Asya Sharif Omar, kuwa Zanzibar mwaka wake wa kuneemeka ni awamu ya Dk. Mwinyi.

Haya, yanakuja kudhihirishwa leo akiwa ndani ya miaka mitatu ya uongozi wake, maana baada ya kuwaahidi wananchi, juu ya utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025.

KULIINUA ZAO LA MWANI

Alikuwa, akinukuu mara kwa mara juu ya kuliimarisha na kilipima eneo la Chamanangwe kwa Pemba, pamoja na ujenzi wa kiwanda cha kusarifiwa mwani

Na haya pamoja na mengine, kumbe yamo ndani ya Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025, kwenye Ibara ya 156 (e) na (m), ambayo imeelekeza kuanzishwa viwanda vya kusarifia biadhaa ikiwemo za mwani.

Kwenye hili Dk. Mwinyi hakuwa tu akisema kwa matakwa yake, kumbe hata lile la uchumi wa buluu lipo kwenye Ibara ya 162 kwenye vifungu vidogo vya (c) na (e) ilielezea namna bora ya kuyatumia mazao ya baharini kama mwani, kuwa chachu ya maendeleo.

Haya wakati anayanadi, wapo wasiomfahamu Dk. Mwinyi kuwa wala asingeweza kulipandisha hadhi zao la mwani, kama vile alivyoahidi wakati wa kampeni.



LEO NDANI YA MIAKA MITATU

Mkurugenzi mkuu Kampuni ya mwani Zanzibar Massoud Mohamed Rashid, anasema ujenzi wa kiwanda hicho, umekamilika.

Ujenzi huo ambao ulikuwa unajengwa na Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo Zanzibar ‘KMKM’ kwa awamu ya kwanza, kati ya zile tatu, umeshakamilika wote.

Zuri ni kuwa, ujenzi huo wa kiwanda cha kusafiria mazao yatokanayo na mwani, unasimamiwa na Mshauri elekezi, kutoka Wakala wa Majengo Zanzibar.

Mkurugenzi anasema kuwa, awamu ya kwanza ilijumuisha ujenzi wa jengo kuu la kiwanda, ujenzi wa ghala pamoja na uzio maalum, kwa ajili ya kulihifadhi eneo hilo.

Na awamu hii ya kwanza, kumbe imepangwa kukamilika ndani ya mwaka huu, kabla ya kuanza kwa awamu ya pili, ya ujenzi wa kiwanda hicho.

Maana awamu hii ya kwanza, ilishaanza tokea mwezi Julai mwaka 2022, ambapo kwa sasa umefikia asilimia 100.



‘’Awamu pili ulijumuisha ujenzi wa maeneo ya bustani, ufungaji wa mitambo husika na awamu ya tatu ni kuanza uzalishaji bidhaa, zitokanazo na zao la mwani,’’anafafanua.

Yeye anasema, ndani ya miaka mitatu ya Dk. Mwinyi, wakulima wa zao la mwani kisiwani Pemba, waanze kukaa mkao wa kula, kwani sasa mwani utaongezeka thamani.

‘’Kwa hakika aliyofanya Dk. Mwinyi hapa Chamanangwe ni utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025 kwa vitendo, sasa huku ndio kuwainua wananchi kiuchumi kwa vitendo,’’anasema.

Baada ya kukamilika kwa ujenzi huo, shughuli za kutafuta na kufunga mashine zinatarajiwa kuanza, na kukamilika kwa kazi hiyo, kutawezesha kazi za kusarifu mwani, kuanza.

Kwa wakati huo ujenzi huo wa awamu ya kwanza, ukitarajiwa kutumia shilingi bilioni 8.2 ingawa wakati ulipotembelewa na mwenge wa uhuru, ulishatumia shilingi bilioni 4.024 na utakapomalizika wote, utagharimu shilingi bilioni 13.

‘’Mradi huu wa kiwanda, utakapomalizika utakuwa na uwezo wa kusarifu mwani tani 30,000 kwa mwaka, ambapo umiliki wake kwa asilimia 55 utakuwa serikalini na asilimi 45 utakuwa wa kampuni ya Nutri-san,’’anasema Mkurugenzi.        

Hapa Mkuu wa wilaya ya Wete Dk. Hamad Bakar Omar, anaamini kuwam, mradi huo mkubwa na wa aina yake, utakuwa na tija mara mbili.

Moja ni ajira za muda na kudumu, sambamba na zao la mwani, sasa kupata hadhi, kwa kule kuongezeka bei, ikilinganishwa na iliyopo sasa.

‘’Naamini, kiwanda hichi kinakuja kuwa mkombozi kwa wakulima wa mwani, ambao wengi wao ni wanawake, hivyo ni wajibu kukitunza,’’anasema.



Anasema ambae haoni aliyoyafanya Dk. Mwinyi ndani ya miaka mitatu, afike ndani ya wilaya yake na hasa eneo la Chamanagwe, ataona kazi iliyofanywa kwa vitendo.

Mkuu huyo wa wilaya anasema, kasi aliyokuja nayo Dk. Mwinyi na akimaliza kipindi cha miaka yake mitano, hakutakuwa na eneo, ambalo hajaligusa kwa uwekezaji mkubwa.

‘’Sisi wananchi wa wilaya ya Wete, na hasa wakulima wa mwani, sasa tumefarajika mno, maana yale aliayoaahidi Dk. Mwinhyi, sasa yanaonekana kwa vitendo, hongera miaka mitatu,’’anasifia.

Hivi karibuni, Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, akizungumza na vyombo vya habari, alisema mradi huo, haujawahi kutokea hasa kwa ukubwa na umuhimu wake.

‘’Kila mmoja ni shahidi kuwa, wakati rais wa sasa wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi akipeperusha bendera ya chama chake, aliahidi ujenzi wa kiwanda hicho, leo upo,’’anafafanua.

WAKULIMA WA ZAO MWANI

Salama Makame Mchakwe wa Tumbe, anasema sasa ni jambo la kujivunia, kwa mradi huo mkubwa ndani ya mkoa wa kaskazini Pemba, kwa miaka hii mitatu ya Dk. Mwinyi.

Anasema, wapo baadhi yao na kwa wakati huo, walishindwa kuamini, juu ya ujenzi wa kiwanda hicho, kwani walishazoea kuelezwa, ahadi kama hizo.

‘’Leo tukiwa ndani ya shamra shamra za kutimia miaka mitatu ya uongozi wa Dk. Mwinyi, nasisi wakulima wa zao la mwani, tunalo tena kubwa la kujivunia,’’anasema.



Hata Maryam Haji Bakari na mwenzake Aisha Issa Ali wanaolima mwani Tumbe, wanaona kama vile sasa, wamepata mkombozi, pindi kiwanda hicho kitakapomalizika kufungwa mashine.

‘’Kwa hakika, kiongozi mkweli hupimwa kwa kauli zake na vitendo, leo ndani ya miaka mitatu, tokea Dk. Mwinyi aingie ikulu, sasa Chamanagwe panan’gaa maana kiwanda kinasubiri ufungaji wa mashine tu,’’wanasema.

Afisa Uvuvi Wilaya ya Micheweni Abdalla Issa Nassor, anakiri kuwa wakulima zile changamoto kadhaa na nyingine zilizokuwa zikiwakabili wakulima hao, sasa watafutwa jasho ndani ya miaka hii mitatu ya Dk. Mwinyi.

‘’Walishapita viongozi wengine, lakini hawakuumwa na zao la mwani, lakini Dk. Mwinyi ndani ya miaka mtatu, mambo yanang’aaa,’’anasema.



Eneo jingine imeelezwa na Kaimu Mratibu wa kampuni ya mwani ya Serikali Zanzibar (ZSCO)Pemba Khadija Zahran Mohamed kuwa, kampuni ya mwani ya serikali, imekuja kuondosha manyanyaso wanayoyapata wakulima wa zao hilo.

Anasema wapo wakulima walifika kuambiwa mwani wao ni mpeta, sababu sio wakulima wanaosaidiwa vifaa na kampuni hiyo, hali iliyopeleka kushindwa kununuliwa.

“Wapo waliopatiwa vifaa vya kulimia na kubeba mwani, hawa sasa wanapaswa kulima kwa wingi, wale ambao bado tutahakikisha kupitia kampuni hii, nao wanapatiwa,’’anaeleza.

Aliwataka wakulima hao kuhakikisha wanashirikiana na serikali, pale itakapoanza kunua mwani, huku suala la bei linaweza kubadilika, kama ilivobadilika awali kutoka shilingi 700 hadi shilingi 1000 na inaweza kufikia hata shilingi 2000 kwa kilo moja

Wakati huu kiwanda kikiwa hakijaanza kusarifu bidhaa za mwani, usafirishaji wa zao la hilo, nje ya nchi umeongezeka, kutoka tani 11,383 mwaka 2020 hadi tani 12,124 mwaka 2021 sawa na ongezeko la asilimia 6.1.

Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, imeanisha kuwa, uzalishaji wa zao la mwani, umeongezeka kutoka, tani 10,531 kwa mwaka 2021, hadi tani 12,594 kwa mwaka 2022 sawa na ongezeko la asilimia 20.

Taarifa ikafafanua kuwa, usafirishaji wa mwani nje ya nchi umeongezeka kutoka tani 12,124 kwa mwaka 2021 hadi tani 13,972 mwaka 2022, sawa na ongezeko la asilimia 15.

Kama hivyo ndivyo, hongera Dk. Mwinyi, hongera miaka mitatu ukiwa ikulu na hongera CCM kumpa kijiti Dk. Mwinyi.

                   Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch