Skip to main content

MBUNGE ASIYA AWAKUMBUSHA JAMBO WAZAZI WA QAMARIA WETE

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MBUNGE wa Viti maalum mkoa wa kaskazini Pemba Alhajjat Asiya Sharif Omar, amewakumbusha wazazi na walezi, wenye watoto wao Almadrassatul-Qamariyya ya Wete, kulipa ada za watoto wao kwa wakati, ili kuwapa uhakika waalim kufundisha kwa ufanisi.

Alisema, maendeleo yaliopo katika madarassa hiyo, hayakuja bure, hivyo ili yawe endelevu, hakuna budi kwa wazazi na walezi kujikumbusha namna ya ulipa ada.

Mbunge huyo aliyasema hayo, ukumbi wa zamani wa baraza la wawakilishi Wete, kwenye mahafali yalioambatana na siku ya wazazi kwa madrassa hiyo.





Alisema, maendeleo endelevu katika madrassa hiyo, hayatokuja kwa haraka na kudumu, ikiwa wazazi watapuuzia suala la ulipa ada kwa watoto wao.

Alieleza kuwa, madarassa hiyo haina mfadhili wala ruzuku kutoka serikalini, hivyo na inategemea moja kwa moja ada kutoka kwa wazazi na walezi, wenye watoto wao katika madrassa hiyo.

“Nichukuwe nafasi hii, kuwasisitiza wazazi na walezi kuhakikisha wanalipa ada zao kwa wakati, kwani hizo ndio zinazotegemewa na waalimu, kuendesha madrassa hiyo, na kinyume chake, ni kudhoofisha malengo husika,’’alieleza.

Katika hatua nyingine Mbunge huyo, amewataka wazazi na walezi, kufuatilia kwa karibu maendeleo ya elimu kwa watoto wao, ikiwemo kujenga ushirkiano endelevu kati yao na waalimu na kamati husika.

Aidha Mbunge huyo wa viti maalum, ameikumbusha jamii, kuwa watoto wana haki mbali mbali, ikiwemo kusikilizwa, kupatiwa elimu bora, kucheza pamoja na kulindwa na majanga.

Wakati huo huo Mbunge huyo, aliongoza harambee, kwa ajili ya ununuzi wa bati ya kuezekea madraasa hiyo, na kupatikana shilingi 300,000 nae kisha kuchangia shilingi 500,000 katika hafla hiyo.




Hata hivyo alisema, atachangia bati kadhaa kwa ajili ya kazi hiyo, mara baada ya kamati ya madrassa hiyo, kumpa taarifa rasmi.

Awali alikabidha zawadi mbali mbali kwa washindi wa masomo mbali mbali katika madarassa hiyo, samba mba nae kukabidhi vinywaji aina soda na biskuti kwa ajili ya wanafunzi hao, vilivyogharimu wastani wa shilingi 650,000.

Mapema Mwalimu mkuu wa Madrasaa hiyo ya Qamariyya Fadhila Awadhi Salimu, alimpongeza Mbunge huyo, kwa moyo wake, wa kuwa karibu na mdau mkuu wa maendeleo ya elimu.

Alisema, Mbunge huyo amewakua akishirikiana na jamii kila wakati, bila ya kujali nafasi yake, jambo ambalo linawapa wigo mpana wa kuendesha shughuli zao.



“Tunaomba viongozi wetu wote wawe mfano wa kama alionao Mbunge wetu huyu, kwanza hana majivuno, pili ni mpenda maendeleo ya watoto na amekuwa mdau mkuu wa elimu,’’alieleza.

Akisoma risala ya wanafunzi katika madrassa hiyo, mwanafunzi Saleh Ibrahim, alisema kwa sasa madrassa hiyo, inakabiliwa na uchakavu wa majengo.

Alisema changamoto nyingine ni baadhi ya wazazi na walezi, kuwa wazito wa kulipa ada zao, jambo linalochangia kuongeza uzito wa kuiendesha madrassa hiyo.






Katika hafla hiyo, wanafunzi hao walionesha vipaji mbali mbali ikiwemo, sira, ngonjera, wimbo wa ukaribisho, namna ya kufuata kwa vitendo hadithi za Mtume Muhammad (S.A.W) pamoja na jukumu la wazazi katika malezi ya pamoja.

                               Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch