Skip to main content

WANACHAMA WAMCHAGUA TENA MLAY KUWA RAIS MCT

 

 



NA HAJI NASSOR, ARUSHA@@@@


WANACHAMA wa Baraza la Habari Tanzania MCT, wamemrejesha tena Rais wa Baraza hilo, Jaji Mstaafu: Juxon Isaac Mlay kwa miaka mengine mitatu ijayo, kupitia mkutano mkuu wa 25, uliofanyika Septemba 28, 2023 mkoani Arusha.

Mkutano huo, pia umemchagua Yussauf Khamis Yussuf kuwa Makamu wa rais  na wingine waliochaguliwa katika mkutano huo ni wawakilishi wa vyombo vya habari, akiwemo Tido Mhando.

Wawakilishi wingine ni Rose Rouben, Ali Haji Mwadini samba mba na kupatikana kwa wawakilishi watatu, kundi la umma wakiongozwa na CPA: Happiness Nkya, Jaji Robert Makaramba na Mwajaa Said.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi huo, rais aliyerejea tena madarakani Juxon Isaac Mlay, alisema kasi na ari iliyokuwepo kwa miaka mitatu, ni vyema ikaongezeka.

Aliwataka viongozi wenzake, waliorudi kutetea nafasi zao, kuhakikisha wanaendelea kufanya makubwa, wakiwa ndani ya Baraza la Habari Tanzania, ili kuwalipa wanachama waliowachagua.

‘’Niwaombe wale viongozi wenzangu, tuliochaguliwa kuhakikisha tunafufua ari na kasi mpya, ili kuendelea kulipatia maendeleo endelevu na wanachama wake Baraza letu,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Rais huyo wa Baraza la Habari Tanzania alimtangaaza Ernest Sungura, kuwa ndie anayetarajiwa kubeba mikoba ya nafasi ya Katibu Mtendaji mpya.

‘’Kwani miezi mitatu ijayo, Katibu Mtendaji wa  sasa Kajubi Mukajanga, anatarajiwa kustaafu, hivyo tayari Bodi ya wadhamini imeshamteua mtu, wa kushika nafasi hiyo,’’alieleza.

Katibu Mtendaji wa MCT anayemaliza muda wake Kajubi Mukajanga, alisema anajivunia umoja na mshikamano, aliyoupata kutoka kwa wafanyakazi wenzake, katika kipindi cha utumishi wake.

Aidha alisema, sasa anashukuru, wakati anamaliza muda wake, tayari MCT inayofisi, na huku vyombo vya habari na waandishi wake, wakiwa wamepata uwelewa wa mambo kadhaa.



‘’Lakini kubwa zaidi, ni kuendelea kufanikisha uwepo wa utamaduni wa mashindano ya umahiri wa waandishi wa habari, kwa miaka 14 mfululuzo sasa,’’alieleza.

Hata hivyo Katibu huyo Mtendaji, alieleza kuwa, anaendelea kusononeshwa na wanachama wa MCT, wasiolipa ada zao, akisema wanadhofisha baadhi ya harakati za kimaendeleo.

Akiwasilisha ripoti ya utendaji ya MCT, Afisa kutoka baraza hilo Saumu Mwalimu, alisema kwenye ufuatiliaji wao wa vyombo vya habari, wamegundua vyombo vya habari vya magazeti, vimekuwa vikijibebesha kazi ya kutoa hukumu, kwenye vichwa vyao vya habari.

‘’Kwa mfano, vipo vichwa vya habari vinavyoandikwa na wahariri, hutoa jawabu au hukumu kwa aina habari iliyoripotiwa, lakini na kuendesha mazungumzo yasio na tija kwa watangaazaji wa redio,’’anaeleza.

Nae Afisa wa MCT Paul Mallimbo, alisema wanachofanya baada ya kuona chombo cha habari, kinakengeuka kanuni, sheria na sera za uandishi wa habari, ni kuviandikia barua.

Wakichangia ripoti za fedha na za utendaji, washiriki wa mkutano huo akiwemo Jabir Idrissa, alilipongeza Baraza kwa kazi kubwa wanazozifanya, hasa za utatuzi wa migogoro.

Mwandishi Nevile Meena, alisema kama waandishi wa habari hawafanyi habari za uchambuzi wanaweza kuachwa nyuma na wasiosomea uandishi wa habari.

Wakati huo huo, Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Kajubi Mukajanga, alisema, bado kuna uminywaji wa habari, na kuwakosesha taarifa wananchi, kujua kinachoendelea serikali.

Katib huyo Mtendaji, alitoa taarifa hiyo kwa vyombo vya habari, ukumbi wa Kibo, jengo la Mahkama ya Afrika, mkoani Arusha ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku ya kujua duniani.

Alisema ujumbe wa mwaka huu, wa unakwenda sambamba na kauli ya Waziri mkuu wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Majaaliwa Kassim Maajaliwa.

‘’Ujumbe wa mwaka huu unaosema ‘umuhimu wa matumizi ya mitandao ya kijamii katika kupata taarifa’ jambo ambalo linakwenda samba mba na sheria kadhaa za habari,’’alieleza.



Kwa upande wake Mhadhiri wa Chuo cha Kiislamu Murorogo, Rehema Twahiri, alisisitiza umoja na mshikamano wa vitendo baina ya waandishi wa chombo kimoja na chingine,’’alishauri.

Ne Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria Tanzania ‘OUT’ Vicent Mpepo, alisema hata kama vyanzo watu vya kutoa habari, ifikiriwe namna kwa MCT.Z2/

atika mkutano huo mkuu wa 25 wa Baraza la Habari Tanzania MCT, ulihudhuria na wanachama hai 54, kati ya 61 ambao hawana deniAAAA hadi mwaka 2023.

Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch